1000 digits
JF-Expert Member
- Oct 16, 2012
- 7,201
- 9,529
Ni lazima iwe hivyo kwa sababu Wajanja wachache wanawatumia wajinga wengi kama Ngazi. Tanga watu hawachagui wawakilishi bali wanachagua wafadhili. Hilo ni jambo linalowasumbua sana.
Tanga imezungukwa na mito na maji mengi lakini kuna maeneo watu wanakunywa maji machafu tena ya bomba na wanalipa bili. Ukiangalia kuanzaia Mwenyekiti wa serikali za mitaa , Diwani ,Afsa mtendaji ,Mbunge na kila mtu kwenye idara ni kada wa Kupeleka majungu CCM matokeo yake hata akija kiongozi watu hawaulizi kuhusu mambo ya msingi kama maji ,barabara za vijinini n.k wanabaki kuchongeana kwa majungu na kutishiana uchawi. Eti ni nchi inayotegemea kupata maendeleo iwe dona kantri labda Sembe kantri.
Dunia ya leo Utajiri ni kuwekeza kwenye teknolojia sio vinginevyo sasa Tanga CCM imewekeza kwenye Kugawa kanga wakati wa uchaguzi badala ya Kuwatoa watu kwenye akili za kuwategemea Watawala watoe pesa wakati wa uchaguzi kununua kura wapite kirahisi au bila kupingwa . Lushoto Kuna mgombea mmoja wa CCM aliwapa tu wajumbe pesa ili apite kirahisi mana hana mida wa kampeni. Wale wasiopenda dhulma wakajikuta hawana mtu wa kumpigia kura jambo ambalo limewakera sana .
Facebook pekee inaingiza mabilioni ya Pesa kuliko migodi yote ya madini tumayojivunia. Facebook haiharibu mazingira wala nini lakini inakusanya pesa dunia nzima. Teknolojia tu.