Sijui ni kujifariji au kujidanganya au kujitia upofu.
Unasema mkuu angepunga mkono tu, mbona hakupunga huo mkono?
Nadhani figisu zote zinazoendelea kama kuenguliwa wagombea, tume na kupendelea upande mmoja, Lissu kubugudhiwa n.k mnaziona.
Kama mnakubalika kiasi hicho kwa nini nguvu kubwa itumike? Kamapeni zenu zimekuwa maigizo tu na hakuna uhalisia watu wanaudhuria kwa wingi kwa ajili ya wasanii au usafiri wa bure na posho kidogo.
Niko mkoa fulan, wilaya fulani wakati mkuu anakuja watu huku wilayani kwa maelfu walisombwa na mabasi kwenda town kujaza uwanja, sasa najiuliza nguvu yote ya nini kama mnakubalika?
Najua kama una akili timamu unajua kabisa nini kinaendelea, nadhani ni maslahi binafsi ndo yanakufanya ujitie upofu, ila ukweli mnaujua na uko wazi.