Uchaguzi 2020 Zikiwa zimebaki siku 20, wapinzani wanashindana huku akili na mioyo yao ikiamini mshindi ni Magufuli

Uchaguzi 2020 Zikiwa zimebaki siku 20, wapinzani wanashindana huku akili na mioyo yao ikiamini mshindi ni Magufuli

Magufuli amejitahidi sana kudhibiti mfumuko wa bei. Baadhi ya vitu kama sukari vinafanyiwa hujuma na baadhi ya wafanyabiashara
 
Hofu yao ni juu ya kuibiwa kura na kubadilishwa matokeo!
Wengi hawaamini alichosema Lissu kuwa hawatakubali kuibiwa kura.
Rejea kauli hii,"Nimekupa gari na nyumba harafu umtangaze mpinzani"!
 
Yap ukweli unaujua na nnaamini Mama ako alikufundisha Uwe mtoto Mzuri na daima useme Ukweli!! Mungu akusamehe na aukujalie maisha baada ya 28 october 2020[emoji120]
 
Hata ww ungekuwa mgombea wa ccm ungeshinda tu bila shaka au unhetangazwa mshindi....ushindani wa siasa Tz utakuwa ni siku mfumo mzima wa NEC ukibadilishwa yani tume iwe huru kabisa
Wapinzani wangapi wametangazwa kaka? Halafu kama tume haiko huru na itawatangaza wagombea wa CCM ni kwanini wapinzani wanashiriki uchaguzi huu? Simngeugomea?
 
Sijui ni kujifariji au kujidanganya au kujitia upofu.

Unasema mkuu angepunga mkono tu, mbona hakupunga huo mkono?

Nadhani figisu zote zinazoendelea kama kuenguliwa wagombea, tume na kupendelea upande mmoja, Lissu kubugudhiwa n.k mnaziona.

Kama mnakubalika kiasi hicho kwa nini nguvu kubwa itumike? Kamapeni zenu zimekuwa maigizo tu na hakuna uhalisia watu wanaudhuria kwa wingi kwa ajili ya wasanii au usafiri wa bure na posho kidogo.

Niko mkoa fulan, wilaya fulani wakati mkuu anakuja watu huku wilayani kwa maelfu walisombwa na mabasi kwenda town kujaza uwanja, sasa najiuliza nguvu yote ya nini kama mnakubalika?

Najua kama una akili timamu unajua kabisa nini kinaendelea, nadhani ni maslahi binafsi ndo yanakufanya ujitie upofu, ila ukweli mnaujua na uko wazi.
 
Magufuli amejitahidi sana kudhibiti mfumuko wa bei. Baadhi ya vitu kama sukari vinafanyiwa hujuma na baadhi ya wafanyabiashara
Unakumbuka wakati anaingia madarakani sukari ilikuwa bei gani na sasa hivu ni bei gani mkuu?
 
Magufuli ashinde kwa kura kutokea wapi? Kule chato kwenyewe hawamkubali, hakuna Mtanzania mwenye Akili timamu ataipigia kura mtukufu magufuli bali Tumeccm na Polisiccm ndiyo watapindua meza kwa njia haramu za kishetani, mtukufu kawatendea nini watanzania? Miradi yote ni pesa za walipa kodi siyo pesa zake binafsi tokea mfukoni, maendeleo siyo Hisani za CCM, maendeleo ni lazima kwa watanzania, kama CCM watapata wabunge 20 Safari hii wabadilike na kujua wao ni chama cha upinzani kama KANU ya kenya
 
Na hizi figisu figisu za tumeccm na polisiccm sioni ushindi halali ni wizi tu! Lazima pachimbike na vikwazo vya kiuchumi vya BEBERUS kama KAWA.
Tayari ICC ina list yote ya Polisiccm wanaoshiriki vitendo vya uonevu unyanyasaji kwa wapinzani mara baada ya uchaguzi watafikishwa ICC The Hague akiwemo IGP mwenyewe
 
Nothing can defeat JPM than God.
CCM bila uchakachuaji bila wizi wa kura bila Polisiccm bila Tumeccm bila mahakamaccm bila wakurugenziccm bila Msajiliccm ni weupe sana
 
Ushauri kwa wafuasi wa Tundu humu ndani mkaombe uwakala kwenye chama cheni mshuhudie atakavyopata kura0
Sio mkae ndani halafu mkishindwa mtafute sababu
Hakuna Mtanzania mwenye Akili timamu ataipigia kura CCM bali wale wanufaika wa mfumo kandamizi mfumo wake wa udikiteta, wasaka uteuzi kama akina Tumbili kafulila na wenzao
 
Atashinda kwasababu ametutendea maajabu watanzania
Maajabu yapi? Miradi yote mikubwa imejaa ufisadi wa kutisha kuna 10% za wajanja wachache pesa ya walipa kodi inazunguka inamrudia mwenyewe kwani idadi kubwa ya makampuni yaliyopewa Tenda ni yake ya ndugu zake na rafiki zake, hakuna maendeleo yeyote mapya kwani vingi vilianzishwa na kikwete yeye kaviendeleza kwa kodi za watanzania siyo pesa zake binafsi tokea mfukoni
 
Hakuna Mtanzania mwenye Akili timamu ataipigia kura CCM bali wale wanufaika wa mfumo kandamizi mfumo wake wa udikiteta, wasaka uteuzi kama akina Tumbili kafulila na wenzao
2810 tukutane hapahapa kupeana pole na kupongezana
 
Magufuli amejitahidi sana kudhibiti mfumuko wa bei. Baadhi ya vitu kama sukari vinafanyiwa hujuma na baadhi ya wafanyabiashara
Deni la taifa limezidi kuwa kubwa zaidi kwenye utawala wenu wa uonevu unyanyasaji kuwabambikia kesi kuwapiga risasi wapinzani, hakuna unafuu wa maisha kwani miaka mitano bila nyongeza za mishahara kwa watumishi wa umma ni kilio kisicho na msamaha
 
2810 tukutane hapahapa kupeana pole na kupongezana
2020 ipo kivingine CCM bye bye hakuna mabaya yasiyo na mwisho, walikuwepo akina Bokasa, Gadafi , Sadam Hussein, Abacha, chiluba, mabutu, Elbashiri wa Sudan, Iddy Amin dada leo hii wapo wapi?
 
Back
Top Bottom