ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

28 OKTOBA 2013: SUPER KAMANYOLA kina Roy Mukuna, Parash, Benno & co AT VILLA PARK MWANZA g sengo mpeg1video source: Gsengo wa youtube
 
Last edited by a moderator:

Kaka umenikumbusha my childhood. Hii ngoma niliikariri japo nilikua mdogo. Eddy Sheggy ndo alikua mtunzi na kuimba akishirikiana na Nana Njige
 
Nimekumbuka pamba moto daresalama awamu ya pili
 
Umenikumbusha mbali uncle!!! Daah - iyo historia kwani imeshaisha? Mbona nasikia mavitu yanazidi kuporomoshwa na hivi vichwa kama supu umeitia nazi,Jinamizi la talaka etc Malizia tafadhari!! wanakosa airtime tu kwa media mbalimbali.
 
Umenikumbusha mbali uncle!!! Daah - iyo historia kwani imeshaisha? Mbona nasikia mavitu yanazidi kuporomoshwa na hivi vichwa kama supu umeitia nazi,Jinamizi la talaka etc Malizia tafadhari!! wanakosa airtime tu kwa media mbalimbali.
Tumwagie data za vijana jazz, vijana orchestra, air pambamoto, saga rhumba:
 
Nawatakiwa maandalizi mema ya Krismas na Mwaka mpya 2014

 
Last edited by a moderator:
Watoto wamekuja Juu....

Hayati Adam Bakari ' Sauti ya Zege' na Washirika Tanzania Stars 'Watu njatanjata'

Ningali bado najiuliza usiku na mchana, na mume wangu kanitoka upweke umenizunguka...
Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao, Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao....

Na kila nikifikiria jinsi nilivyotabika, na malezi ya watoto ingawa sikuwazaa...
Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao, Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao....

Ningali bado najiuliza usiku na mchana, na mume wangu kanitoka upweke umenizunguka...
Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao, Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao...

Na kila nikifikiria jinsi nilivyotabika, na malezi ya watoto ingawa sikuwazaa...
Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao, Watoto wamekuja juu, wanadai nyumba yao....

Adam Bakari:

Kila nilifanyalo wao haliwapendezi, na wala hawakumbuki usia wa baba yao;
Kila nilifanyalo wao haliwapendezi, na wala hawakumbuki usia wa baba yao;

Marehemu aliusia wasinitupetupe, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
Marehemu aliusia wasinidharau, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...

Majirani wameshauri eti nirudi nyumbani kwani sina baba wala mama, jama niende kwa nani....
Wengine wameshauri eti niwashitaki wakati nyumbani ni mali yao, Jama nifanye nini....

Marehemu aliusia wasinitupetupe, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
Marehemu aliusia wasinidharau, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...

Marehemu aliusia wasinitupetupe, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
Marehemu aliusia wasinidharau, na wala wasininyanyase mama....ooh mama...
 
Christina Moshi ....

International Orchestra Safari Sound....wana Ndekule

Sina budi mama kukueleza, katika wimbo mpenzi Moshi...
Mchana kutwa huwa nashinda sina raha mkono kwenye shavu...
Sina budi mama kukueleza, katika wimbo mpenzi Moshi...
Mchana kutwa huwa nashinda sina raha mkono kwenye shavu...


Kusema kweli moyo wangu umeridhika kwa penzi lako mpenzi Christina...
Nimeamini penzi ni kiungo kwa wapendanao unanitoa upweke...
Kusema kweli moyo wangu umeridhika kwa penzi lako mpenzi Christina...
Nimeamini penzi ni kiungo kwa wapendanao unanitoa upweke...

Christina Moshi sikiliza maelezo yangu katika wimbo mamaa...
Naelewa penzi li bado ni changa usije tena ukabadilika baadae...
Tulipokubaliana kwa hiari tulikuwa wawili wa tatu Mungu wetu...
Tulipokubaliana kwa hiari tulikuwa wawili wa tatu Mungu wetu...

Christina Moshi sikiliza maelezo yangu katika wimbo mamaa...
Naelewa penzi li bado ni changa usije tena ukaniruka baadae...
Tulipokubaliana kwa hiari tulikuwa wawili wa tatu Mungu wetu...
Tulipokubaliana kwa hiari tulikuwa wawili wa tatu Mungu wetu...

Bridge....

Pendekezo langu kwako liwe kama benki, benki imara kwa usalama...
Pendekezo langu kwako liwe kama benki, benki imara kwa usalama...
Akiba yangu ya mapenzi nakupa wewe Moshi ee mama...
Akiba yangu ya mapenzi nakupa wewe Moshi ee mama...


Uwezo sina ningekujengea nyumba, uwezo sina ningekununulia gari...
Bali matatizo madogo hayatanishinda.....
Uwezo sina ningekununulia mtumbwi, uukabidhi kwa wavuvi wakakuvulie samaki....

Uwezo sina ningekupeleka Arusha, ukapunge hewa nzuri na kutazama wanyama mbugani...
Bali matatizo madogo hayatanishinda...

Nitajipigapiga ili niyatatue, sababu jungu kuu halikosi ukoko, sababu jungu kuu halikosi ukoko...
Mpenzi Moshi lea hili penzi letu, usiliweke juani litakuja nyauka.....

Pendekezo langu kwako liwe kama benki, benki imara kwa usalama...
Pendekezo langu kwako liwe kama benki, benki imara kwa usalama...
Akiba yangu ya mapenzi nakupa wewe Moshi ee mama...
Akiba yangu ya mapenzi nakupa wewe Moshi ee mama...


Kibwagizo:
Hebu sikia maneno ya kuambiwa na wana Ndekule, Moshi ee, ee Ndekule..
Hebu sikia maneno ya kuambiwa na wana Ndekule, Moshi ee, ee Ndekule..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…