Black hermit
JF-Expert Member
- Mar 20, 2017
- 658
- 951
Jamani natafuta wimbo wa OMARI MKALI wimbo wa kitambo kidogo unaitwa Kibuyu, hapa nina uhakika kuna kila aina ya watu natumaini nitaupata mwenye nao nauomba tafadhali.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huu wimbo nimeutafuta toka 2005 mpaka leo sijaupata. vipi ntaupataje?!Yote aliyofanya ndugu yangu Joseph Pauline ni sawaa au amekosea eeeh ni sawa au amekosea a eeeh .
Pauline kafanya mambo katuacha kwenye mataa ee Pauline .....
Katuacha tumeduwaa eeh
Vyombo......
Chorus. ......Jambo la kushangaza Pauline kafanya party la kuuga umasikini eeeh, Pauline oooh oohh laa la la laaa la.
Tumesukuma nae mikokoteni maskani ooohh oohh jama aa Pauline rafiki yetu la la la la
Chorus repeats!
Watu wengi walihudhuria pati hilo ooo
Fred Benjamini alikuwepo
Toto Tundu alikuwepo
Shomari Ally akikuwepo
Shakashia alikuwepo
Suleiman Mbwembwe alikuwepoooo
Mkuu nimekumbuka mistari hiyo japo kwa kujivuruga. Majina ya wanamuziki waliotajwa kwenye wimbo huu walikuwa mahiri sana wakati ule. Na ni katika Album hii Vijana Jazz ilianza kufifia. Wengi waliondoka na wengine walishatangulia mbele ya haki. Ni Album ya msimu wa 1996/97. Baada ya hapo Vijana haikutoa Album iliyohit kwani ilitoa I love you Mpiga debe miaka ya 1999 na Mabaa Maid miaka hiyo ya 1999/2000.
Sababu kubwa ni viongoz wa bendi yaani UVCCM kuipa sapoti kubwa TOT Band.
Album hiyo yenye wimbo ulioutaja ndo ya mwisho katika mtiririko wa Pure Vijana Jazz Air Pamba moto, Saga Rhumba! Ukiondoa wimbo huo, nyimbo zingine nzuri kabisa katka album hiyo ni Mama Samia, Mbuzi yake kamba nk. Naitafuta hii Album katika CD ila naikosa. Ninayo kwenye tape, bahati mbaya vifaa vyangu siyo rafiki tena kwa tape.
Ila Bantalanda ninashida sana na wimbo Kapu la Mjanja na Janja ya Nyani pamoja na Visa vya Mume.
Wimbo huu visa vya mume naupenda sana hasa pale wanaposema- Nikipika wali unasema una mawe e , nikipika ugali unasema una mabuja sema kinachokukera bwana eeeh. Ilikuwa ni combination ya hatari wakina Adam Bakari( sauti ya zege). Daa zaman kulikuwa na Muziki na Vijana Jazz ilikuwa ni noma. Ila nayo ilipata Upinzani mkali kutoka Washirika Tanzania Stars(Watu Njatanjata) na Bimalee.
Sijui unaishi wapi, ila kama unaishi dar, huo wimbo utaupata pale, temeke mwisho, zinaposhusha basi za kusini, Wale wananyimbo nyingi za zamani. nikikosa wimbo mtandaoni naenda pale, nyimbo nyingine mtandaoni huwa haziimbi mpaka mwisho.Huu wimbo nimeutafuta toka 2005 mpaka leo sijaupata. vipi ntaupataje?!
Huu zuhura, ambao Laddy Champion, mzee Zahir alihama nao toka J.KT. Ruvu, uko vizuri mkuu.Pia kuna Washirika Tanzania Stars Band.....
Bendi hii ilikuwa ikimilikiwa na Jumuiya ya Washirika Tanzania na iliundwa na wanamuziki wengi waliojiengua kutoka Orchestra Vijana Jazz,iliundwa mwaka 1989 na ilikuwa ikitumia mtindo wa Watunjatanjata(Watanzania tuondoe njaa Tanzania) na baadae wakajiita Njata one....
Bendi hii ilikuwa ikifanya maonesho yake katika ukumbi wa 92 Hotel pale Sinza Shekilango...Ilikuwa ni bendi kali hasa na ilikuwa ni tishio kwa bendi zilizotamba enzi zake hasa Vijana Jazz...
Bendi hii ilitamba na nyimbo kama Yaliyopita si ndwele(Nimekusamehe lakini sitokusahau),Washirika,Nelson Mandela,Julie,Penzi la ulaghai,Nimebaki nashangaa,Spare tyre,Maeliza,Gubu la wifi zako,Zuhura,Umbea,Watoto wamekuja juu,Masumanda,Kissa,Kayumba na nyingine kali....
Bendi hii iliundwa na wanamuziki wengi waliojiondo Vijana Jazz kama Hamza Kalala 'Komando',Eddy Sheggy,Mhina Panduka 'Toto Tundu',Adam Bakari 'Sauti ya Zege' bila kuwasahau Abdul Salvador 'Father Kidevu',Emma Mkelo 'Lady Champion',Robert Mabrish,Zahir Ally Zorro,Madaraka Morris 'Kiwembe' ,
Baadae mwaka 1991 baadhi ya wanamuziki wakiongozwa na Hamza Kalala na Eddy Sheggy na kwenda kuunda bendi mbili tofauti za Bantu Group Band(wana Kasimbagu Kahabuka) na MCA International(wana Munisandesa) na wengine(Eddy Sheggy na wenzake) walihamia Bima Lee Orch. wana Magnet Tingisha.....Hiii iliifanya Watunjatanjata itetereke kidogo hadi mwaka 1992 ilipompata mtaalam Zahir Ally Zorry ambaye aliifanya ikabaki imara na mtindo wa Watunjatanjata waliouboresha na kuwa Njata One wakiwa na nyimbo kama Gubu la Wifi zako,Maeliza,Zuhura na Umbea
Nisaidie namba zao,,inbox.Sijui unaishi wapi, ila kama unaishi dar, huo wimbo utaupata pale, temeke mwisho, zinaposhusha basi za kusini, Wale wananyimbo nyingi za zamani. nikikosa wimbo mtandaoni naenda pale, nyimbo nyingine mtandaoni huwa haziimbi mpaka mwisho.
"si wazuri binadamu usione wafurahi"Mkuu SI WAZURI BINADAMU imeimbwa na BICHUKA lakini akiwa na OSS sio MLIMANI PARK. "Ninakushukuru Mungu huso mshirikae kuiponya roho yangu ilotaka toweka binadamu madhurumu ana vituko vya sumu anavituko vya sumu kali kushinda ya nyokae si wazuri binadamu usione wachekaa ooh nhon."
Hana wemaa usimwone kucheka oooh"si wazuri binadamu usione wafurahi"
"Mtendee la muhimu hatoridhika, akisha kusalimu moyoni akasirika"
Ooohhh.
Bonge la Wimbo.
Hapa ni wakati wa vijembe. Baada ya kuimba wimbo huu Bitchuka akiwa OSS ndio ukawa mwisho wa vijembe kutoka Juwata.
Daaaah,umenikumbusha mbaaali enzi hizo RTD tu akina Juma ngondae.Twende na wimbo wa "Mtu ni afya mwananchi elewa eeh, tusiwe wavivu kuzijenga vyema afya zetu"
Mwenye kujua ni bendi gani iliyoimba wimbo huu aniambie pliz. Na pia kama kuna mtu anao basi atuwekee hapa tafadhalini.
We acha tu ndugu yangu, kuna nyimbo mtu ukizisikia lazima utoe chozi bila kujijua.Daaaah,umenikumbusha mbaaali enzi hizo RTD tu akina Juma ngondae.
Na hisi na huu utakua unaujua[emoji1787]We acha tu ndugu yangu, kuna nyimbo mtu ukizisikia lazima utoe chozi bila kujijua.
Nautafuta sana mwimbo huu.
Huu wimbo kama sikosei umeimbwa na Washirika Tanzania Stars, Njata one,Vijana wa zamani mnaojua vitu. Bado wimbo wenye maneno haya sijaupata na kama mliutuma sijaziona.
Maneno yake ni hivi
Nakwenda ilula kwa wakwe zangu wakanieleza, na maneno mengi ya kwamba yeye ana uwezo
"Leo isiwe sababu ya kunitangaza mimi eehe na kuniaharibia jina langu ehe toto tundu.
Penzi langu la kusuasua
wakuu umoufia kwenu,naomba please anajua pa kuupata au mwenye nao huu wimbo "chaupele mpenzi"
waniambia niliwache rhumba nami sikuzoea,sitaweza kuliacha rhumba sababu yakooo..aisee mwenye nao anisaidie nimeutafuta sana,nikachoka ila jana bongo radio online wakaupiga ,nimepata mzuka wakuutafuta tena