ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Hii inakukumbusha wapi? Kamata sauti za dhahabu za Hemed Maneti, Mohamed Shaweji na Mohamed Salum "Gotagota". Katika solo yupo Shaaban Yohana "Wanted". Bendi ni Vijana Jazz, Kibao ni 'Siri ya Ndani' na mwaka ni 1990.

 
Last edited by a moderator:
Hii inakukumbusha wapi? Kamata sauti za dhahabu za Hemed Maneti, Mohamed Shaweji na Mohamed Salum "Gotagota". Katika solo yupo Shaaban Yohana "Wanted". Bendi ni Vijana Jazz, Kibao ni 'Siri ya Ndani' na mwaka ni 1990.



Duh, Mkuu,nimesoma hilo cover nikaona kile kibao cha Nyongise. Bila shaka ni utunzi wa Mzee John Kitine. Yaani kuuona tu huo wimbo, nimekumbuka mbali sana.

Nilikuwa Kigoma naangalia game ya kandanda kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mwanzoni kabisa mwa 1990 (enzi hizo hakuna cha EPL kwenye TV). Kuna rafiki yangu niliyesoma naye Primary anaitwa Kabeya Moses, huku tunaangalia mpira na sikioni amewka karedio kake kadogo anasikiliza muziki Nyongise ukivurumishwa kupitia RTD enzi hizo.
 
Last edited by a moderator:
Duh, Mkuu,nimesoma hilo cover nikaona kile kibao cha Nyongise. Bila shaka ni utunzi wa Mzee John Kitine. Yaani kuuona tu huo wimbo, nimekumbuka mbali sana.

Nilikuwa Kigoma naangalia game ya kandanda kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mwanzoni kabisa mwa 1990 (enzi hizo hakuna cha EPL kwenye TV). Kuna rafiki yangu niliyesoma naye Primary anaitwa Kabeya Moses, huku tunaangalia mpira na sikioni amewka karedio kake kadogo anasikiliza muziki Nyongise ukivurumishwa kupitia RTD enzi hizo.

Mkuu wangu Ibrah....

Habari za miaka mkuu...

Hicho kikosi cha Pambamoto kilikuwa ni kikali sana mkuu...Ni kama Barcelona ya sasa...Kikosi kilikuwa kimesheheni vipaji kama Hemed Maneti Ulaya, Kida Waziri, Adam Bakari, Eddy Sheggy, Hamza Kalala, Kulwa Mlonge, Hamis Mnyupe, Hassan Shaw, Abuu Semhando, Shaaban Yohana, Shaban Dogodogo na wengine...

Nakumbuka mwaka huo wa 1990 ndipo Vijana Jazz walitoa albam yenye vibao kama Ngapulila, Ogopa Tapeli, Mwisho wa mwezi, Chanjo kwa watoto, Penzi haligawanyiki na Telegram (Jamaa alimdanganya boss wake kapokea Telegram inayomjulisha kifo cha kaka yake...Boss akampa pole kwa msiba uliompata,akatoa fedha,gari na wafanyakazi kumsindikiza kwenda kijijini...Kufika kijijini hakukuwa na msiba wala nini....)

John Kitime yeye alijiunga na Vijana Jazz mwaka 1991 kama sikosei, na hii ni baada ya Hamza Kalala, Eddy Sheggy na Adam Bakari kujiondoa Vijana Jazz na kwenda kuanzisha Washirika Tanzania Stars Band 'Watu njata njata'...

Akiwa Vijana Jazz Kitime alitunga vibao vitamu kama Nyongise(Nyongise nigenenene nyongisee......) na Malaine.....

Hakika ya kale yalikuwa zaidi ya dhahabu...
 
jamani mie nautafuta wimbo mmoja wa kina kasaloo na kyanga kama sijakosea unaitwa "NAKUPA TALAKA" kama kuna mtu anaweza nisaidia link au wimbo kamili maana tangu nimeupoteza huu mwaka wa 6 nautafutaga tu
 
leo nimeisikiliza nyimbo ya Urafiki Jazz wana Chaka chuwa inasema...

''biashara ya njugu na korosho haikufai mama wee, Gezaulole mama, Gezaulole Mama wee''

Dah Juma Mrisho Ngulimba wa Ngulimba amefanya kazi sana mle...

" biashara ya kahawa na maji ya barafu kwa sasa haitufai twendeni gezaulole.. Kie kie kie "


Sent via EyePhone
 
Jerry Nashon ameimba Immaculata (Makulata) kwa lugha ya Kijaluo.

Nashukuru mkuu nimeamini jf hakishindikani kitu, siku zote nilidhani kwenye wimbo wa Mwamvua ni kishwahili tupu lkn nilipousikia kwenye kipindi kinachorushwa kila ijumaa na redio flani sipendi kuitaja nikagundua kile sio kiswahili, bahati namba ya muendesha kipindi nnayo maana anapenda kuitaja ili mwenye swali amuulize nami nikampigia lakini alijibu kwa jazba kuwa "kila siku najibu hilo swali akakata simu" nilimsamehe bure na kumtumia msg kuwa umeshajitolea kuwa muelimishaji usiwe na jazba ualimu ni wito, nikaona ngoja niende kwa Balantanda na kweli japo sio yeye aliyejibu nimefarijika kuona wataalamu wapo wengi. Nashauri tuwe tunapita hapa mara kwa mara tusipotee sana. kwenye Mwamvua Jerry anasema
"Pesa yeyeye pesaa pesaaa ye ye ye ye x2 subiri kidogoo mamy haiyeaye mamaa pesa zinazonisumbua ee mama aiyeaye mamaa, usinione hivi mamiii haiyeaye mamaa pesa zinazonisumbua ee mama aiyeaye mama". sasa panapofuata mi nilikuwa nachapia kwa kishwahili kuwa ni "Nyota na mwezi na ardhi mama ooh nyota na mwezi na ardhi mama ooh, nyota na mwezi na ardhi mamamama Mwamvua mamaaa". Ni juzi ndio nimegundua ni kilugha.
 
Mkuu wangu Ibrah....

Habari za miaka mkuu...

Hicho kikosi cha Pambamoto kilikuwa ni kikali sana mkuu...Ni kama Barcelona ya sasa...Kikosi kilikuwa kimesheheni vipaji kama Hemed Maneti Ulaya, Kida Waziri, Adam Bakari, Eddy Sheggy, Hamza Kalala, Kulwa Mlonge, Hamis Mnyupe, Hassan Shaw, Abuu Semhando, Shaaban Yohana, Shaban Dogodogo na wengine...

Nakumbuka mwaka huo wa 1990 ndipo Vijana Jazz walitoa albam yenye vibao kama Ngapulila, Ogopa Tapeli, Mwisho wa mwezi, Chanjo kwa watoto, Penzi haligawanyiki na Telegram (Jamaa alimdanganya boss wake kapokea Telegram inayomjulisha kifo cha kaka yake...Boss akampa pole kwa msiba uliompata,akatoa fedha,gari na wafanyakazi kumsindikiza kwenda kijijini...Kufika kijijini hakukuwa na msiba wala nini....)

John Kitime yeye alijiunga na Vijana Jazz mwaka 1991 kama sikosei, na hii ni baada ya Hamza Kalala, Eddy Sheggy na Adam Bakari kujiondoa Vijana Jazz na kwenda kuanzisha Washirika Tanzania Stars Band 'Watu njata njata'...

Akiwa Vijana Jazz Kitime alitunga vibao vitamu kama Nyongise(Nyongise nigenenene nyongisee......) na Malaine.....

Hakika ya kale yalikuwa zaidi ya dhahabu...

Kwangu mimi naifananisha vijana ya 1991 na Madridi ya kina R Carlos, Zidane, Ronaldo de Lima, Makelele, Figo na Morientes. Nakumbuka walitoa albam ya nyimbo 6 ambazo huwezi kufoward kila inayokuja ni tamu ambazo ni VIP, Tereza, Mama Chichi, shoga, Mvuvi Kinda na ya mwisho imenitoka kidogo ilikuwa sio mchezo, waimbaji walikuwa ni Jerry Nashon "Dudumizi, Seleman Mbwembwe "mzee wa miba", Beno Vila Anton, Mohamed Gotagota "electronic voice", Saidi Hamisi "misukosuko", Fred Benjamin, Abdala Mgonahazeru na Muhina Panduka
 
International Orchestra Safari Sound - Homa Imenizidia

Published on 21 Apr 2012Mid 80's East African Rhumba!
Here's some information about them: IOSS was created in a kind of coup in 1985, when the bandowner, businessman Hugo Kisima, disbanded his Orchestra Safari Sound (OSS) led by Ndala Kasheba and hired six leading members of Mlimani Park to form the nucleus of the new IOSS. Singer Muhiddin Maalim Gurumo and lead-guitarist Abel Balthazar were the new bandleaders, Hassani Bitchuka the leading vocalist and composer.

International Orchestra Safari Sound - Homa Imenizidia


source: soukousman wa youtube
 
Last edited by a moderator:
DDC Mlimani Park - Celina

Inaonesha kipindi hicho bendi zilikuwa kamilifu safu zote kuanzia , wanamuziki, mistari, sauti, ala, vyombo na kitu kizima yaani wimbo unakuwa ukitoka basi utadumu miongo kadhaa:


Vocals ni Muhidin Mwalimu, Hamisi Juma (RIP) na Cosmas Chidumule. Lead guitar Abel Balthazar (RIP), bass Joseph Mulenga (RIP), rhythm Abdallah Gama. Drums Habib Abbas 'Jeff'. listi hii kwa hisani ya Bingwason wa youtube

DDC Mlimani Park - Celina

source : Abdallah Ally a.k.a Tizedboy wa youtube
 
Last edited by a moderator:
Bongo fleva si muziki wetu na hautakuwa muziki wetu japo ma dj wanalazimisha hivyo. Binafsi katika bendi zetu zilizowahi kutamba mimi niliipenda sana Sagha Rhumba. Hawa jamaa kwa sauti walikuwa hawana mfano, yaani tishio na moto wa kuotea mbali. Line Up: Vocals enzi ya Sagha Rhumba: Jerry Nashon, Gotagota, Adam Bakari, Saidi Hamisi, Mgonahazeru, Freddy Benjamin, Momba, Sheggy, Mobali Jumbe, Mbwembwe, Nuru Mhina, Mhina Panduka, yaani hatari tupu.
Solo: Wanted Shaaban Yohan, Miraji Shakashia
2nd Solo: John Kitime
Rythm: Aggrey Ndumbalo
Bass: Baba Watoto 'Manitu Mussa,' Baker Semhando
Tumba: Ali Jamwaka
Drums: Juma Choka 'Kikoko,' Baba Diana 'Abuu Semhando.'
Trumpets: Mnyupe, Mawazo Hunja
Saxo: Professor Rashidi Pembe 'Papaaaa,' Ali Tuba

Kwa kweli hii bendi ilikuwa tishio. Ondoa Msondo ama Nginde kwani hizi bendi zilibaki majina tu ila baba yao alikuwa Sagha Rhumba. Sikilizeni 'Penzi Halina Shule,' 'Malaine,' 'Ushambenga,' 'V.I.P.' 'Theresa,' 'Shoga,' 'Top Queen,' 'Binti Afrika,' 'Visa Vya Mume,' 'Pati Ya Kuaga Umasikini,' 'Baba Samia,' 'Mwanamke Salo,' 'Chivalavala,' 'Mzinga,' 'Kapu La Mjanja,' 'Wapambe Nuksi,' 'Bar Maid, 'Kizaa Zaa Cha Simu Ya Mononi'....jamani nishikeni mkono mzuka unanipanda mwenzenu hapa.....niendelee?:target:
 
Mkuu wangu Ibrah....

Habari za miaka mkuu...

Hicho kikosi cha Pambamoto kilikuwa ni kikali sana mkuu...Ni kama Barcelona ya sasa...Kikosi kilikuwa kimesheheni vipaji kama Hemed Maneti Ulaya, Kida Waziri, Adam Bakari, Eddy Sheggy, Hamza Kalala, Kulwa Mlonge, Hamis Mnyupe, Hassan Shaw, Abuu Semhando, Shaaban Yohana, Shaban Dogodogo na wengine...

Nakumbuka mwaka huo wa 1990 ndipo Vijana Jazz walitoa albam yenye vibao kama Ngapulila, Ogopa Tapeli, Mwisho wa mwezi, Chanjo kwa watoto, Penzi haligawanyiki na Telegram (Jamaa alimdanganya boss wake kapokea Telegram inayomjulisha kifo cha kaka yake...Boss akampa pole kwa msiba uliompata,akatoa fedha,gari na wafanyakazi kumsindikiza kwenda kijijini...Kufika kijijini hakukuwa na msiba wala nini....)

John Kitime yeye alijiunga na Vijana Jazz mwaka 1991 kama sikosei, na hii ni baada ya Hamza Kalala, Eddy Sheggy na Adam Bakari kujiondoa Vijana Jazz na kwenda kuanzisha Washirika Tanzania Stars Band 'Watu njata njata'...

Akiwa Vijana Jazz Kitime alitunga vibao vitamu kama Nyongise(Nyongise nigenenene nyongisee......) na Malaine.....

Hakika ya kale yalikuwa zaidi ya dhahabu...

Bala, za miaka nzuri sana. Hakika Vijana Jazz hiyo uliyoitaja haikuwahi kutokea tena. Nakumbuka Eddy Sheggy, Adam Bakari na Hamza Kalala baadaye walitimkia Washirika Stars-Watunjata njata ambayo iliongezewa kina Abdul Salvador, Madaraka Morris aliyetunga kibao 'Julie' ambacho hata kikipigwa leo utadhani ni cha jana.
 
Msaada wenu wana jf msaada wa rekodi ya nyimbo hizi za zilipendwa online 1. DALILI-MSONDO NGOMA 2. CHEUSI MAGALA NO.1-OTTU JAZZ 3. MALARIA-MSONDO NGOMA 4. NIPELEKE KWA BABA NO.2-OTTU JAZZ 5. SI WAZURI BINADAMU-MLIMANI PARK ORCHESTRA Kama kuna mdau ataweza kuniaploadia online au anafahamu link ambayo nitaweza kuzipata nyimbo hizi, nitashukuru sana
 
Msaada wenu wana jf msaada wa rekodi ya nyimbo hizi za zilipendwa online 1. DALILI-MSONDO NGOMA 2. CHEUSI MAGALA NO.1-OTTU JAZZ 3. MALARIA-MSONDO NGOMA 4. NIPELEKE KWA BABA NO.2-OTTU JAZZ 5. SI WAZURI BINADAMU-MLIMANI PARK ORCHESTRA Kama kuna mdau ataweza kuniaploadia online au anafahamu link ambayo nitaweza kuzipata nyimbo hizi, nitashukuru sana


Hizo nyimbo zote na nyingine nyiiingi mimi ninazo ila nauza.
Una pakee mfukoni ni PM ili nikuite sehemu na kukuchomea kwenye CD...
Napatikana Dar kwa sasa, lakini mwezi ujao ntakwenda home Baidoa.
 
kuna wimbo unasema:-

Naikumbuka siku ileeee ulipokuja asubuhi na mapema,
ukifoka kwa ukali , kwamba ni mimi niliyetaka vunja ndoa yako.

Namshukuru baba mwenye nyumba,
aliyelizua panga lako,
lisishuke maungoni na kunipa kilema cha maisha.

Chorus:-

ukweli ulikuja kwa hasira sana (ehhh bwana ehhh)
bila kufahamu undani wa mambo yenyewe.


wimbo huo nautafuta sana, sikumbuki jina lake wala walioupiga
 
kuna wimbo unasema:-

Naikumbuka siku ileeee ulipokuja asubuhi na mapema,
ukifoka kwa ukali , kwamba ni mimi niliyetaka vunja ndoa yako.

Namshukuru baba mwenye nyumba,
aliyelizua panga lako,
lisishuke maungoni na kunipa kilema cha maisha.

Chorus:-

ukweli ulikuja kwa hasira sana (ehhh bwana ehhh)
bila kufahamu undani wa mambo yenyewe.


wimbo huo nautafuta sana, sikumbuki jina lake wala walioupiga


Hapo kuna sauti ya Marehemu Moshi na Marehemu Zengekala...
Hilo goma lilipigwa na Juwata Jazz Band Msondo ngoma...
 
kuna wimbo unasema:-

Naikumbuka siku ileeee ulipokuja asubuhi na mapema,
ukifoka kwa ukali , kwamba ni mimi niliyetaka vunja ndoa yako.

Namshukuru baba mwenye nyumba,
aliyelizua panga lako,
lisishuke maungoni na kunipa kilema cha maisha.

Chorus:-

ukweli ulikuja kwa hasira sana (ehhh bwana ehhh)
bila kufahamu undani wa mambo yenyewe.


wimbo huo nautafuta sana, sikumbuki jina lake wala walioupiga




NI wimbo wa msondo na unaitwa Kilema Cha Maisha.
 
Back
Top Bottom