Zitambue fursa za kiuchumi katika Mkoa wa Njombe

Zitambue fursa za kiuchumi katika Mkoa wa Njombe

Econometrician

JF-Expert Member
Joined
Oct 25, 2013
Posts
16,879
Reaction score
31,253
Mkoa wa Njombe: Mkoa wa Njombe una Halamashauri 6 ambazo ni Njombe Mjini, Vijijini, Ludewa, Makete, Wangingombe na Makambako.

Wenyeji wa Mkoa wa Njombe 70% ni wabena, ambao wanapatikana Wilaya za Njombe mjini,Vijijini, Makambako, Wangingombe na wakinga-Halamashauri ya Makete na Halamashauri ya Ludewa wapo Wapangwa na wanyasa.

Sifa muhimu za kiuchumi katika Mkoa wa Njombe
  • Ndio Mkoa unaongoza kwa Idadi ndogo ya watu kwa takwimu za awali za sensa ya 2022 Mkoa huo unakadiriwa kuwa na watu 889,946
  • Mkoa wa Njombe ni miongoni mwa Mikoa top 5 iliyo na watu wa vipato vikubwa zaidi kuliko Mikoa mingine.
  • Mkoa wa Njombe-Makambako kuna upepo wa kiwango kikubwa ambao unaweza kuzalisha umeme wa megawati zaidi ya 300
  • Unaongoza kwa uzalishaji wa mbao-Asilimia 60-70 ya mbao zote zinazotumika Tanzania zinatoka katika huo Mkoa-na zinalimwa karibu Halamashauri zote za Mkoa huo.
  • Unaongoza kwa uzalishaji wa zao la viazi mviringo 70% ya viazi vyote Tanzanua vinalimwa huko.
  • Unaongoza katika uzalishaji wa zao LA parachihi Tanzania nzima.
  • Ndio Mkoa unaongoza kwa madini ya Chuma na Makaa ya mawe. Kwa Tanzania akiba kubwa ya madini hayo yapo Mkoa huo na yanapatikana kule Luganga na Mchuchuma Wilayani Ludema.
Sifa nyingine:
  1. Unaongoza kwa wafanyabiashara wakubwa Tanzani a.k.a Wakinga
  2. Ndio Mkoa unaongoza kwa baridi Tanzania nzima hasa Njombe Mjini na Makete
  3. Mkoa wa Njombe ndio Mkoa pekee kwa kipindi cha miaka 5-10 unaongoza kwenye top 3 ya maambukizi ya HIV
  4. Mkoa wa Njombe ina Idadi kubwa ya Wanawake kuliko Wanaume kuliko Mikoa yote Tanzania.
N.B. Kama mtu upo interested kuishi mazingira kama ya Ulaya ulaya yenye baridi na green-Mkoa wa Njombe ndio jibu sahihi. Huko Mbu na nzi ni kama hakuna. Maelezo mengine kuhusu investment opportunities katika Mkoa huo tembelea Ofisi ya Mkuu wa Mkoa

 
Ni mkoa ulio connected na lami kwa halmashauri zake zote sita
FoXuisnWAAI3VMU.jpg
sddefault(0).jpg
13-8.jpg
3-30.jpg
 
Write your reply...ukiacha liganga chuma kinapatikana maeneo gani mengine ndani ya ludewa au ndani ya mkoa huo.
 
Viwanda vya madawa ya binadamu ndani ya mkoa wa njombe
15.jpg

FB_IMG_16745448312569380.jpg
 
Write your reply...hayo maeneo yamechukuliwa nataka ambayo bado nataka nije niwekeze kwenye sekta hyo.
 
Write your reply...hayo maeneo yamechukuliwa nataka ambayo bado nataka nije niwekeze kwenye sekta hyo.
 
Ndo mkoa wenye eneo dogo nyanda za juu kusini Yani iringa ,songwe mbeya ,ruvuma na rukwa na ndo mkoa ambao upo katikati nyanda za juu kusini ko ndio maana hata bidhaa zake ni rahisi kupata soko
A-map-showing-the-study-districts-and-their-respective-wards-in-Njombe-region-Tanzania~3.jpg
3-0.jpg
 
Back
Top Bottom