Uchaguzi 2020 Zitto 2015 ulikataa UKAWA, why leo utake Coalition?

Uchaguzi 2020 Zitto 2015 ulikataa UKAWA, why leo utake Coalition?

Kama Zirto alimkataa Lowasa basi alikuwa sahihi lakini kama aliukataa muungano kama muungano hilo ni jambo jingine.
Sisi tuliyempigia Lowasa alhali tulijua ni fisadi tuliongozwa na unafiki.
 
Na hakukaribishwa kwa sababu alikuwa haaminiki, ni wajibu wake sasa kuthibitisha kwa vitendo imani kwa waliokuwa na shaka nae.
Mkuu Zitto hana chakuthibitisha kwa mtu yeyote wote wenye akili tunafaham ile ilikuwa power struggle iliyokuwa ndani ya CDM. Sasa niwajibu kila chama kiangalie maslahi yaushirikiano na mwenzake Kama yapo washirikiane Kama hayapo wasishirikiane. Lakini tu nikufahamishe kama hawatoshirikiana basi mtarajie ccm kupita kwa ushindi wakishindo ukizingati nafigisu wanazofanya. Na pia CDM ikimsimamisha Nyalandu ndio kabisa, watu tunamuhitaji Lisu na kwa bahati nzuri Zitto alishatamka wazi kuwa Lisu akigombea watamuunga mkono. Sasa niviongozi kuangalia watanzania tunataka nini lakini wakileta umimi basi wote hawatoambulia kitu.
 
Na kwa upepo wa sasa ACT wanaenda kuunda Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni japo ni habari chungu kwa Chadema...Ni swala la muda tu ja

Kukiwa na uchaguzi kwa maana ya uchaguzi, tunaweza kuwa na tathmini sahihi, ila sio kwa tume hii. Ndio maana kwangu bado naamini kupigania tume huru ya uchaguzi kulipaswa kuwa kipaombele cha wapinzani, kuliko hizi nafasi tunazotajiana humu. Nikikumbuka uhuni kwenye chaguzi za marudio, na hitimisho kwenye uchaguzi wa SM, nikiona wapinzani wanataka kushiriki bila shinikizo stahiki la hii tume, naona wapinzani wakishiriki kutakatisha uhuni wa ccm.
 
CHADEMA wasijiunge na ACT, bora ijiunge na PONA, ukiwakataa wenzako, nao watakukataa.

Zitto abaki peke yake na hata bungeni kila chama kiunde kambi yake.
 
We jamaa nimjinga sana, kwenye thread yako unasema alikataa kujiunga na ukawa, hapa una comment kuwa alikataliwa, sasa sisi wapenda mageuzi tukuelewe vipi?. Kama una agenda za ccm tunaomba uziache , Zitto alisema kabisa yuko tayari kwa ushirikianoo hata mgombea akiwa Lisu sasa tatizo lake liko wapi?.

Unajua watu wengine wenye mawazo kama yako niwajinga sana, hebu jichukulie wewe ni Zitto na upo katika nafasi aliyopo utaacha kujenga chama kisa utaonekana unatumiwa na ccm?.

Sisi tunachohitaji ACT & CDM washirikiane ili wagawe majimbo Kisha uraisi asimame Lisu tutawapigia Kura, Sasa kwa bahati mbaya wote hatuna uhakika kama Lisu atarejee kulingana na mazingira yaliyopo. Kwahio lazima vyama vyote iwe CDM au ACT kila chama kiendelee na mipango yake mpaka pale ushirikiano viongozi watakaporidhia uwepo. Huwezi kuacha kukiaandaa chama na uchaguzi kisa unasubiri kesho ambayo huifaham.

Wewe ndo mpuuzi, kukataa masharti ni sehemu ya kukataa kujiunga. Kama upo tayari utakubaliana na masharti. Akili zenu mnaweka wapi? Huyo Zitto wako hana mpango na Lissu hata kidogo, wait to be surprised soon. Lissu ndo chaguo sahihi la CDM na si ACT
 
Wew naona 2015 ulikuwa chekechea na hivyo hujui politics zilivyokuwa 2015. Zitto hakukataa UKAWA, ni kwamba hakukaribishwa. Alitamka mara kwa mara kwamba anataka kujiunga lakini kwa sababu ambazo hazikuwekwa wazi hakukaribishwa.

Pole sana, Mwambie akuwekee wazi sababu anazozificha ndo ujue ubinafsi wake uko wapi.
 
Mlikataliwa kwa sababu mlikuwa Wabinafsi. Na ndiyo maana Chadema waliwaona nyie ni adui namba moja. Mwaka 2019 ndipo uliporuhisiwa kujiunga na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni baada ya kuanza kujiandaa kwa Movie hii tunayoiona sasa, na kumbuka wakati Mbatia akielezea kuruhusiwa kwako alisema sasa utapaswa kufuata taratibu zao tofauti na awali ambapo ulikuwa ujafanya kama unavyotaka. Na mostly ulitusaliti wapinzani wenzako kwenye movements kibao Bungeni. Chonde Chonde CHADEMA msiingie mtego huu mtanasa vibaya sana.
Wewe si mwan siasa, ni mpiga debe wa CCM,
Kazi yako kufukua makaburi,
Unakumbuka kuwa CUF mwaka ilipofanya Muwafaka na CCM ,chadema walisema kuwa CUF ni CCM -B na akwa na minyukano mikali,kumbe ile ilikuwa faraja kwa CCM,
Wewe bado hujasoma tuu,siasa za nchi hii
Miaka kadha baadae Chadema na CUF wakawa marafiki wa chanada na pete ,hasa kwenye Ukawa.
Hakuna uadui wa kudumu kwenye siasa, kuna maslahi ya kudumu, sisi sote ni watanzania,lengo letu ni kuingoa CCM li kuleta mabadiliko stahili ya demokrasia.
Kwa hili lazima tuache mivutano ya kichama na umimi,
Kwa pamoja tutaingoa CCM na kuleta mabadiliko ya kweli. Kila uchauzi kuna kitu tunajifunza na kujiweka sawa.
Wapinzani wa kweli wanzidi kujipambanua kila uchao, vyama vingi haviko pale kufanya siasa,ba kuisindikiza CCM katika ushindi wake akina TLP ya mrema, AFP,CHAUSTA, NLD na Jahazi, na sasa CUF ya Lipumba imeunga tela.
 
Na kwa upepo wa sasa ACT wanaenda kuunda Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni japo ni habari chungu kwa Chadema...Ni swala la muda tu ja
kwa majimbo ya pemba na bara mawili matatu uwezekano ni mdogo bado chadema imejiwekezea mtaji wa wanachama wa bara hata kura zauraisi wazizoa nyingi tuu huo ndio ukweli idawa kazana tu hapo Tunduma upate na wewe ubunge kwa kupitia ACT
 
Kama Zirto alimkataa Lowasa basi alikuwa sahihi lakini kama aliukataa muungano kama muungano hilo ni jambo jingine.
Sisi tuliyempigia Lowasa alhali tulijua ni fisadi tuliongozwa na unafiki.
Mnafiki ulikuwa wewe ,usiyejua ulifanyalo.
Lowasa ana kosa gani Ukawa?
mbona alituwakilisha vizuri tuu pamoja na hali yake aliyokuwa nayo ya kiafya,
Lowasa kurudi CCM hakukuiathiri upinzani any way. Mbona akina Nasari ndio wasaliti! Wanatuacha pale unapowahitaji zaidi?
Lowasa tulijuwa angetusogeza kupata ushindi, na tulikaribia kushinda na wabunge tuliongeza some how,
Kajiondokea kwa maslahi yake kuona yanavurugwa na Nduli mkandamizaji wa upinzani.
Alifanya uwazi usiokuwa na athari kwetu.
 
alikataa kwa uwazi kabisa tena si mara moja au marambili akijinadi kwenye vyombo vya habari why now
Nyiyi wapiga debe wa CCM tunawajuw,kazi yenu kuleta mfarakano upinzani kwa maslahi ya CCM yenu,Tunawatambua.
Hata kama alisema ,sasa ameamua kubadilika, so whats wrong with it?
Hii ni siasa na zama hubadilika, usilinganishe siasa za Kikwete na Magu,
Jiwe ,Jiwe kweli ukijikwaa tuu umepoteza maisha, Lazima nguvu ya kumg'oa iwe kubwa na ya pamoja.
 
Zitto Kabwe ni Mwanasiasa mnafiki, mbinafsi, mwongo na mtu wa kumuogopa kama ukoma. Mara zote amekuwa akilenga mambo yanayompa maslahi binafsi na si umma mkubwa wa Watanzania.

Mwaka 2015 wakati Watanzania tukitaka mabadiliko ya kweli, na kuunda Coalition ya UKAWA Zitto alikuwa kinyume chetu kabisa, na hakutaka hata kushirikiana nasi. By that time chama chake hakikutaka kabisa kumpigia kampeni Mgombea wa CHADEMA aliyeviwakilisha vyama vya Upinzani chini ya UKAWA ndugu yetu Lowassa, na badala yake ACT-Wazalendo walisimmamisha mgombea wao Mama Anna Mghwira na kuzigawa kura za Upinzani. Aidha ACT-Wazalendo walisimamisha wagombea wao wa Ubunge na Udiwani na kuzigawa kura majimboni na kwenye Kata

Kwa kipindi chote cha 2016-2017 Zitto alikuwa totally kinyume na movements ambazo Wabunge wa UKAWA walizichukua wakiwa Bungeni; wakitoka nje, yeye alibaki ndani na hata kuwaponda mara nyingine

This time around ACT-Wazalendo wanataka Mgombea wanayemsimamisha wao, Ndugu Bernard Membe, aungwe mkono na vyama vingine vyote vya Upinzani. Wanataka kukiimarisha chama chao kuwa Chama kikuu cha Upinzani kwa mgongo wa Mgombea wao mmoja kwenye Uchaguzi Mkuu. Wanajua fika wakiungwa mkono na vyama vingine wanaweza ongeza idadi ya Wabunge kwani katika Bunge la 11 alikuwa Zitto peke yake, na hivyo kuongeza kiasi cha fedha wanachopokea kama ruzuku

Nitashangaa sana, CHADEMA iliyokuwa na Wabunge na Madiwani wengi ikiingia kwenye mtego uliotegeshwa na ACT-Wazalendo yenye Mbunge Mmoja na Madiwani kiduchu. That will be the offical death of Opposition in Tanzania.
Why do you think so, is opposition about political parties only? I thought opposition in terms of divergent views on how things should work is natural with human beings. Parties are just vehicles and formal means to disburse our thoughts. Which means even if a party dies in your interpretation another vehicle will come in to occupy the vacuum.

My point is we should, in politics not be myopic by tying ourselves to personalities instead of issues. ACT-Wazalendo is an organisation, it has people including Zitto himself. At times decision is not only about Zitto but the people inside the party. In politics also things don't remain stagnant, they change. Circumstances change people change also and Zitto can't be immune to such.
 
Wewe ndo mpuuzi, kukataa masharti ni sehemu ya kukataa kujiunga. Kama upo tayari utakubaliana na masharti. Akili zenu mnaweka wapi? Huyo Zitto wako hana mpango na Lissu hata kidogo, wait to be surprised soon. Lissu ndo chaguo sahihi la CDM na si ACT
Kwahio wewe ulitaka Zitto afanyeje?.aache siasa kisa anaogopa chadema watasema anatumika, kila mtu katika maisha yake anandoto, nakama anafata ndoto zake hakuna wakumzuia ,either CDM washirikiane au wasishirikiane wote hawatanufaika na ushauri wako lkn mnufaia mkuu atakuwa ccm. Sasa nieither wakubali au wakatae hilo nijuu yao, sisi wananchi tutawaadhibu tu wakifanya ujinga, na maccm yatapata pakufanyia propaganda zao.
 
Na kwa upepo wa sasa ACT wanaenda kuunda Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni japo ni habari chungu kwa Chadema...Ni swala la muda tu ja
Wasiwasi wako tu, ACT ni mbadala wa CUF, hakuna tofauti. Labda hapo kwa Membe tu. Lakini pia walikuwa na Lipumba...Bado wanaweza kukubaliana kuwa atakayeshinda, washirikiane kuunda serikali. Sayansi ya mipango.
 
This is Politics Buda, ni kama vile ambavyo CDM baada ya kuungwa mkono na vyama vingine na kupata kura nyingi na wabunge wa kutosha, Leo wanakula Ruzuku pekee yao.

Kwani mgawanyo wa ruzuku ulikuwa kwenye makubaliani?
 
ACT wanamtaka Membe jomba, na ndio maana Zitto anapigana kwa nguvu zote kuwa na coalition ili mgombea wao aungwe mkono na wengine.

Itakuwa vigumu kumuamini membe haraka haraka watu hawajasahau ya lowasa leo anasema ccm watumie umoja kuuangamiza upinzani inawezekana na yy akiukosa uraisi akifinywa kidogo akirudi atasema hivo hivo bora akae chini ya uangalizi kwa muda aonje uchungu wa upinzani akisha komaa ndio apimwe
 
Back
Top Bottom