Zitto aanika siri nyeti za Mbowe! Adai hatakufa kama Chacha Wangwe
Zitto hajajibu mashtaka kwake kuhusu magari aliyopewa na Mkono. Two wrongs do not make a right.

Kabla ya ku deflect mashtaka kwa kuibua uozo wa mpinzani wako, jibu mashtaka kukuhusu wewe. Hata kama ni kwa kukubali tu.This deflection is one of the oldest tricks in the playbook.

Kwa wazoefu wa habari hizi, usipojibu tuhuma maana yake umekubali ni kweli. Kwa hiyo Zitto kakubali kwamba ni kweli kapewa magari na mkono, lakini anasema wanaomtuhumu nao wana yao kama hayo.

Hili saga linathibitisha yale niliyokuwa naandika hapa kitambo.

Hakuna Zitto wala uongozi wa CHADEMA, wote ni wale wale tu.

Nyinyi Wafuasi wa Mbowe mnashangaza sana kwakweli,Hivi mara hii mshasahau kuwa Zitto alianza kutuhumiwa kwanza na Lissu na yeye ikambidi ajibu mapigo?Nani asiyejua kuwa Mbowe yupo nyuma ya yote haya yanayomtokea Zitto akiwatumia vibaraka wake?Kwahiyo msichukie sana jiandaeni kusikia uozo mwingi kuhusu huyo Mungu wenu na safari asiposimama Mahakamani sijui!
 
Zito analeta utoto wake apa,angesema ayo muda mrefu tunge mkubali ila kwa sasa huyu nimfa maji.
 
Haijalishi Zitto amesema wakati gani, lakini je ni sahihi kwa hao viongozi kupita kila sehemu kuita wengine mafisadi huku wanapokea michango ya hao hao mafisadi?

Zitto anaweza kuwa na makosa yake kwa kuficha taarifa hii, lakini kwa sisi kama wananchi amefanya la maana kusema ukweli huu. better late than never. Na sasa tunajua kumbe Mbowe anachukua pesa kwa akina Rostam na Mkono.

Haya maneno ndiyo yanaoyozidi kudhihirisha udhaifu wa Zito. Angekuwa mtu thabiti, asingenyamaza na madhamabi ya namna hii siku zote, ithabiti ni ama kujiuzulu, au kumpinga anayefanya makosa hadharani, siyo ukumbwe na kashafa ndiyo ujitetee kuwa wengine pia wanazo. Siku za nyuma kidogo alianadika kuwa amekuwa munge kwa miaka mingi na aliwahi kuwa kwenye kamati mbalimbali, ndiyo m,aana ana uwezo mkubwa wa kipesa, lao hii anaanza kukiri kuwa pesa hiyo huwa anapata kwa njia za hongo. Watu wa namna hiyo huwezi kuwaamini kuwa viongozi wa taifa.
 

"TOTAL DESTRUCTION THE ONLY SOLUTION"- Robert Nesta-Marley

LOI-Cutting-Branch.jpg
 
Chadema kimekosa muelekeo
hayo madai ya Tundu Lissu mbona hayamo katika yale mashitaka 11 aliyopewa Zitto?.

sidhani kama aliyomtuhumu nayo mbowe yana tija pia.UDHAIFU WAKO NI KUSHABIKIA KULIKOPITILIZA.
 
Zitto Kamjibu Lisu, kama kweli Mkono kamwambia alimpa magari mawili basi Mkono huyohuyo atakuwa kamwambia Na Mbowe alishampa pesa nyingi tu Mbowe mnaanza kuhoji kuwa Zito hakusema siku nyingi, amesema sababu Tundu Lisu kaambiwa aseme ya mkono, kwanini hakusema ya Mbowe kupewa pesa na Mkono?
 
Well noted! Zitto tumemrushia tuhuma za kutosha na binafsi sina mjadala tena juu ya usaliti wa Zitto.

Lakini hizi za Mbowe nazo ni tuhuma.Zijibiwe tupime!

Sheria msumeno tunataka Wapinzani sio Wakinzani!!
 
kama zzk alikuwa mwadilifu kwanini hakuyasema haya mapema kwa masrahi ya wana cdm na watz kwa ujumla?kwanini makosa anayodai yalifanyika toka miaka ya 2005 ayaseme leo?nafikiri cdm wameset precedence nzuri,personality haiwezi kuwa juu ya chama hats sikumoja.

Alikuwa akiwaheshimu Viongozi wenzie ndio maana alikuwa akiwafichia maovu yao ila kwakuwa watu wenyewe hawana wema sasa ndio ameanza kuyasema aliyopaswa kuyasema miaka mingi iliyopita.
 
Chadema kwa Mipasho bwana, chek hii ya Mohamed Mtoi kwa Dr. Kitila Mkumbo

Mohamedi Mtoiposted toKitila Mkumbo

6 hours ago


MJUMBE HAUWAWI.....

Naomba nisaidie kumfikishia ujumbe huu ndugu yangu katika imani Bwana "Zitto Zuberi kabwe"

Ujumbe wenyewe uko hapo chini huku nikitambua kuwa unakumbuka vizuri Swot analysis uliyomfanyia wewe na Mwigamba kwenye Sehemu ya "Udhaifu wa Tunaye mtaka" kipengele "C' na "G"

"Kwa kuwa kwenye majibu yako sehemu fulani uliamua kuongelea masuala binafsi, naomba kukumbusha kutoka kwenye mkakati wenu (Mkakati wa mabadiliko 2013) kipengele "C" cha sehemu ya "Udhaifu wa tunayemtaka", kipengele hicho kinasema "Hali ya ndoa ya tunayemtaka kutoeleweka msimamo wake" na katika mkakati huohuo kipengele "g" kwenye uchambuzi wenu, wenzako wakasema tena "….Kuna mambo ambayo ni haki ya mtu mfano mahusiano binafsi ya kimapenzi, kuwa na marafiki wa damu kutoka upande mwingine wa utawala nk"

Kwa kufuata msingi wa kipengele "g" kuwa mapenzi na mahusiano ni mambo binafsi, naomba nami niache kujalidili hili kama wewe ulivyo lijadili kwa mwenyekiti wako aliye ku-groom na kuchangia sehemu kubwa ya wewe kufika hapo ulipofika kisiasa, kwa kuwa kujadili itakuwa ni kujadili mambo binafsi.

Ila kwa umuhimu wa kipekee wa kutokulijadili mambo binafsi, naomba pia nikunipe fursa ya kumkumbuka Amina Chifupa na Mohamedi Mpakanjia ambao wote ni marehemu (RIP) pamoja na wahanga wengine".


cc Kitwange, #Ritz , Mohamedi Mtoi
 
Zitto hajachelewa kusema ukweli ukizingatia CDM hawapendi kuambiwa ukweli wa udhaifu wao. Kaka Zitto funguka zaidi kuhusu deal la Kinana na Sumaye maana umetuacha njia panda. Pia usisahau lile la NHC na NSSF sisi tunataka kujua ili tuchague pumba na mchele.

Kama unajua Chacha wangwe alichofanyiwa pls tenda Polis ukawape ukweli wote haki ichukue mkondo wake.
 
zitto ni kiongoz hao wachaga ni wezi tu na tukisuputu kumpa mchaga nchi ooooo
 
kutapa tapa kwa mfa maji zitto tuta yaskia mengi....
 
Mbowe ni kweli haya? Kupewa pesa na ma CCM kwenda kufanyia kampeni sio jambo baya?
"Mimi ni mbunge, bungeni nimekuwa nikichangia watu mbalimbali mimi kama Freeman, si ajabu watu wengine kunichangia. Hapa jambo la msingi ni kwamba unapewa pesa kwa sababu gani, kwa nia ipi? Kupewa pesa na Kikwete au CCM si tatizo lakini unapewa pesa kwa sababu zipi, kwa malengo gani?" alihoji Mbowe.
 
Kwa tuhuma hizi nzito alizozitoa mh. Zitto Kabwe dhidi ya Mwenyekiti wa Chadema mh. Freeman Eikaeli Mbowe, Chadema inabidi ijibu coz its very serious na wakikaa kimya ina maana yanayosemwa na mh. Zitto dhidi ya mh. Mbowe ni ya kweli...basi Chadema haitakuwa na locus standi ya kunyooshea watu kwa tuhuma za ufisadi na michezo michafu...tunamtaka mh. Mbowe atoke kukanusha au tuziamini.

Uyo Zitto nae alikuwa wapi kuyasema hayo toka 2005 hadi leo? Mi naona anazidi kutufanya tumjue vizuri zaidi
 
Mbowe hajajibu kitu hapo mbona katoa tu lawama kwa sisi wachambuzi wa mambo tunaona hivyo
 
Back
Top Bottom