Zitto aanika siri nyeti za Mbowe! Adai hatakufa kama Chacha Wangwe
Ila hii saga CDM inabidi waliendee kwa ustadi sana, manake hawa akina Lissu na Mnyika kuropoka ropoka kutafanya watu wafunguke zaidi na madudu kibao yatajulikana halafu kutakuwa hamna mshindi zaidi ya CCM!
 
Siyo vibaya kupewa pesa na Kikwete au CCM ~ Freeman Mbowe.

Kwi kwi kwi kwi!

Ishara ya kukamatwa pabaya,hivi mpinzani wako anakupa fedha halafu mnaenda kwenye kinyang'anyiro kimoja kweli usi dought?ha ha ha ha kwi kwi kwi kwi wacha nicheke....ha ha ha
Ule waraka wa ushindi una siri sana ule-unakumbuka Mh mbowe aliambiwa hawezi kujenga hoja?elimu kitu muhimu sana nimeamini ule usemi wa too local Mtendaji mkuu
 
Kweli siasa ni mchezo mchafu kabisaa, bora nilime tuu tena kwa jembe la mkono kuliko kuwa mwanasiasa, kweli hii ni hatareeeee
 
mbowe naye ajibu tuhuma zake,kama kweli amekuwa akichukua hella za ccm apigwe chini kwa speed ya ajabu.
 
Hiyo siri yake ni nyeti zaidi ya nyeti yenyewe? Na alikua wapi siku zote? Aache mipasho na kama haachi ntamwombea nafasi Isha Mashauzi
 
mbowe na zitto ondokeni chadema,majibu ya mbowe mepesi sana.
 
uzalendo usikieni tu kwa kina Mandiba na Nyerere,hakuna uzalendo karne hii,
cdm wote ni mafisadi wanaochipukia,hakuna mwenye afadhali bora ccm walishakula sasa wanatuonea huruma
.Zitto,Mbowe,Lissu,Mtei,Slaa wote hawana maana bora ccm endeleeni tu kutimuana kutokana na utendaji sio hawa cdm wanatimuana kwa sababu za kitoto na udictator
 
Mkuki kwa nguruwe sio??

Mwenyekiti CHADEMA anatia aibu,aje akanushe tuhuma zake sasa na yeye

Tundu lisu anacheza ngoma ambayo haijui,wanamtanguliza tu kichwa kichwa yeye hajui kama anajidhalilisha!

Ni ujinga mtu mwenye elimu kama ya tundu kupelekwa pelekwa na kujazwa uongo na mbowe...

Mbowe atoke atuachie chama chetu alishashindwa kabla hajaanza

Na Dr Slaa ajiangalie naona anapotea taratibu

Elimu sio busara ndugu yangu.ana akili fupi kweli na anaongozwa tu na mihemko na jazba!rahisi sana kumfanya akosee!!
 
Baada ya Dr Kitila na Mwigamba kuondolewa ndani ya chama. Kuna wajumbe wengi wa CC wanalalamika kuwa ZZK angeshafukuzwa siku nyingi lakini Mbowe alikuwa analizuia jambo hilo.

Kama ni kweli Mbowe kamkingia kifua ZZK wanaomshutumu Mbowe hoja zao ziko wapi. Nafikiri Mbowe apongezwe kwa kumpa ZZK muda wa kutosha wa kujirekebisha lakini ZZK kapuuzia.

Pengine ZZK angeshafukuzwa siku nyingi kama si Mbowe.
 
Hakyamama hii ni mimba kwa CDM tunasubiria tuone mtoto atakayezaliwa baada ya hapa . Teh teh....
 
Mbowe hakuongwa bali alikuwa akichangisha hela za kampeni.....zitto ana tapata tapata....tu

Yaani anawachangisha mpaka Mafisadi waliotajwa na Dr Slaa kule Mwembe Yanga?Hivi unajua kuwa hakuna msaada usiokuwa na masharti?Je Mbowe na hawa Mafisadi waliahidiana nini baada ya kupeana fedha siri hii inaijua Mbowe peke yake,Kamanda namba moja wa harakati za kumng'oa mkoloni mweusi!
 
Nakumbuka Naibu katibu mkuu bara wa chama cha Wananchi CUF ndugu Julius Mtatiro aliwahi kulalamika kwanini Mwenyekiti wa PAC anafanya kazi katika mitandao ya kijamii?? Ilikuwa kuhusu tuhuma za vyama vya siasa kutowasilisha mahesabu yao kwa CAG alidai mwenyekiti wa PAC hajawapelekea taarifa kuhusu ishu ya kukaguliwa bali kila taarifa yeye alikuwa anaandika katika mitandao ya kijamii, Mtatiro aliongelea sana ishuu hii sasa hapa ndio naanza kuelewa kuwa ndugu Zuberi anapenda sana kufanya kazi katika mitandao ya kijamii hata kwa ishu ambayo haistahili kuwa huko, Binafsi nadhani kwa sasa anatafuta huruma kutoka kwa umma.
Yote kwa yote tuendelee kusubiria mwisho wa sakata hili utakuwaje.
 
Nimeamini maneno ya CDM kuwa saccos ya baadhi ya watu.... kimenuka..
 
Mbowe utachukuaje pesa kwa Kinana ambaye siku zote mnamshambulia humu jukwaani kwamba anamaliza tembo wetu?

Aaah Mbowe?!! Indirectly kama ni kweli Mbowe unashiriki kuua tembo wetu?!
 
Back
Top Bottom