Zitto ataka wanaoikosoa ACT-Wazalendo waanzishe chama chao

Zitto ataka wanaoikosoa ACT-Wazalendo waanzishe chama chao

Zitto Kabwe yuko sahihi!

Chadema usoni mnajifanya kukomaa lakini ruzuku ya wabunge wa viti maalumu mnapokea!
Kupokea ruzuku ni sawa na kujiunga na serikali uliosema hauitambui? Ninavyo jua mimi ruzuku inatokana na kodi ambazo hata wanachama wa CDM wanalipa. Kwa mtaji huo, ulitaka CDM wakatae pia kulipa kodi kwa sababu hawatambui serikali iliyopo?

Kupokea ruzuku ni tofauti kabisa na kiongozi wa Chama kusimama na kutambia jinsi anavyopanda gari la kifahari na kulindwa na askari walewale ambao majuzi tu alikuwa anawashutumu kuwa walikuwa wanawakamata na kuwatendea maovu wanachama wa chama chake. Mbaya zaidi anafanya hivi bila kuwaambia namna gani serikali yake itakavyo shughulikia maumivu ambayo wanachama wa chama chake walipata.

Amandla...
 
Nimeshtushwa sana naingia tweeter nakuta hii tweet ya Zitto Kabwe. Sikutegemea kama angeweza kuandika kitu kama hichi.

View attachment 1649184

Kwa mazingira haya, ni wazi kwamba Zitto anaichukulia ACT kama mali yake binafsi kama nyumba na gari lake, na ana uwezo wa kuamua na kufanya chochote bila kuingiliwa.

Binafsi nawaonea sana huruma wale wanajitia ACT kindakindaki. Wanamshutumu bure Mbowe, sijawahi ona ka tweet pumba kiasi hiki.

Kuna siku mtashangaa ACT imekuwa registered kama Chattle ya kuombea mkopo benki... Maana ni mali ya mtu binafsi.
Vijana wa CHADEMA Achaneni na Zitto.

Zitto alikuwa CHADEMA mkamtumia Dokta Slaa akamfukuza kama mbwa, leo Slaa yuko CCM.

Skendo zote kwamba anatumika na usalama, mlikuwa mnamtumia Kubenea kupitia magazeti yake ya MwanaHALISI na Mawio, leo huyo Kubenea yuko na Zitto huko huko ACT.

Mamangi wa CHADEMA kwanini hampambani na DAID ARFI, SLAA, KSTAMBI, JULIANA SHONZA, Ninyi vita yenu mmekomaa na Zitto tu.

Tangu hiyo ACT inaanzishwa ml nzisha vita kaki sana, kwamba imeanzishwa na CCM kuiua CHADEMA, mara imeanzishwa na LOWASAA.

Mara ghafla Lowassa akahamia CHADEMA. Akafanya yake halafu wakati Mbowe yuko mahabusu yeye akaenda Ikulu kumsifia Jiwe na kisha kuhamia CCM.

Mamangi wa CHADEMA mjue hakuna MTOTO humu ???????????

Probably bange na pombe zinawapotezea uwezo wa kumbukumbu.

MaCCM hayampendi Lissu kiasi kwamba yako tayari kupambana naye akiwa mahututi, naona hali iko hivyo kwa CHADEMA na Zitto.

Mnachoshaaa.
 
Kupokea ruzuku ni sawa na kujiunga na serikali uliosema hauitambui? Ninavyo jua mimi ruzuku inatokana na kodi ambazo hata wanachama wa CDM wanalipa. Kwa mtaji huo, ulitaka CDM wakatae pia kulipa kodi kwa sababu hawatambui serikali iliyopo?..
Ruzuku inatokana na "kura" mlizopata kwenye uchaguzi mkuu.

Hivyo kama uchaguzi ni batili na ruzuku unayopokea ni haramu vile vile!
 
NI Watu kuwa wabishi wa kuelewa mambo ukweli ni kwamba vyama hivi vya kisiasa mrengo wake mkuu ni KUSONGESHA MAISHA HUKU WAKIJIPATIA RIZKI KWA AJILI YA USTAWI WA FAMILIA ZAO
 
Vijana wa CHADEMA Achaneni na Zitto....
Una uhakika kuwa wanaompinga Zitto ni Chadema? Jee umewauliza wana ACT wote wakakuambia wanaunga mkono kuingia kwenye SUK? Hukumsikia Maalim kwenye hotuba yake siku anaapishwa jinsi walivyopambana na upinzani ndani ya vikao vyao vya ndani?

Chadema hawana muda huo kwani nao wana changamoto zao kama vile covid 19 na nyinginezo. Wacheni kila chama kibebe mzigo wake, walioiba kura, kuteka hata kuua ili kujitangazia ushindi nao wanapambana na changamoto zao za jinsi dhamira zao zinavyowatesa wakijutia uharamia wao huku wakiwa hawawezi kutubia dhami yao hii.
 
Kupokea ruzuku ni sawa na kujiunga na serikali uliosema hauitambui? Ninavyo jua mimi ruzuku inatokana na kodi ambazo hata wanachama wa CDM wanalipa. Kwa mtaji huo, ulitaka CDM wakatae pia kulipa kodi kwa sababu hawatambui serikali iliyopo?...
Akili ya ubwabwa, pole.

Alisema kuwa CHADEMA inapinga akina Mdee kuingia bungeni ilihali ruzuku wanayopewa CHADEMA ni pamoja na inayotokana na uwakilishi wa akina Mdee. Meanwhile, kama ubunge wa akina Mdee ni haramu basi CHADEMA ikatae ruzuku inayotokana na wabunge viti maalum yaani akina Mdee.
 
Kuanzisha chama si kuwa mali yako, bado ni mali ya wanachama, iwapo wanachama wakionyesha msimamo tofauti si maana yake waanzishe chama chao, ni suala la kuwashawishi wakubaliane nao!
 
Msiwalaumu,hii karne haina wazalendo,ina wachumia tumbo tu, Na kile kizazi cha Kwame Nkurumah, Steve biko, Mandela, Nyerere,Sokoine, Hashim Mbita, Ahmed Salim, Desmond Tutu, Lumumba, Tundu Lissu hakitakuja kiwepo tena. Siku hizi wanasiasa wanawaza kwa kutumia matumbo, sio vichwa,

Kafulila, Silinde, Lijua Likali, Mwita, Lowasa, Sumaye, Membe na wale covid 19, kila mmoja anaangalia ni bwana yupi analipa dau kubwa, huyo ndio anampa mambo, hawana ajenda, misimamo yao inabadilika Kama mwanamke Malaya.

Wao ni pochi tu, hapendwi mtu/Wala nchi hapa.
 
Msiwalaumu,hii karne Haina wazalendo,ina wachumia tumbo tu,
Kile kizazi Cha Kwame Nkurumah,Steve biko,Mandela,Nyerere,Sokoine,Hashim Mbita,Ahmed Salim,Desmond Tutu,Lumumba,Tundu Lisu,,hakitakuja kiwepo Tena,
Siku hizi wanasiasa wanawaza kwa kutumia matumbo,sio kichwa,
Kafulila,Silinde,Lijua likali,Mwita,Lowasa,Sumaye,Membe,na wale covid 19,kila mmoja anaangalia ni bwana yupi analipa dau kubwa,huyo ndio anampa mambo,hawana ajenda,misimamo yao inabadirika Kama mwanamke Malaya,
Wao ni pochi tu,hapendwi mtu/Wala nchi,hapa,

Hebu msikilize Zitto wa mwezi uliopita baada ya uchaguzi, kisha linganisha na Zitto wa leo anayesema kuwa kama hukubaliani nao anzisha chama chako.

 
Wanasiasa wote ni vinyonga - wote. Wanabadirika rangi kulingana na situation inavyoathiri matakwa yao kwa wakati huo.

Zitto aachwe tu. Hata CHADEMA walishawahi kupiga u-turn na maisha yakaenda. CCM wanapiga u-turn daily.

Zitto na ACT yake hawakuwa na choice nyingine baada ya wafurukutwa (wa mitandaoni), wanachama na wafuasi wao kushindwa kuwaunga mkono when it mattered most
 
Back
Top Bottom