Zitto: CHADEMA walifanya makosa haya ndiyo maana Lowassa akawakimbia, sisi hatutayafanya kwa Membe

Zitto: CHADEMA walifanya makosa haya ndiyo maana Lowassa akawakimbia, sisi hatutayafanya kwa Membe

Kwa lugha nyingine, amejiunga upinzani kwa sababu ya tamaa ya uongozi, na akishapata uongozi basi adhma yake ataibadili juu kwa juu na asipoata uongozi basi atarudi nyumbani kama wenzie waliotangulia
Kuwepo upinzani kwa miezi mitatu tu hata katiba ya ACT WAZALENDO hajaijua halafu kumpa nafasi kubwa hivyo ni makosa makubwa sana.
 
Uko sawa kabisa Mtende. 👊🏽

Kwa lugha nyingine, amejiunga upinzani kwa sababu ya tamaa ya uongozi, na akishapata uongozi basi adhma yake ataibadili juu kwa juu na asipoata uongozi basi atarudi nyumbani kama wenzie waliotangulia
 
EL kashinda KURA ila kashindwa kuutetea uRais wake!! Mzee ni mwoga balaa!!

Unafikiri unapewa Urais wa Tanzania hivi hivi.....Moja ni kura zifike na uhakiishe Umeshinda ...Pili ni lazima ufahamu mbinu la kuudai Urais wako....

Akaweka watu wake pale mlimani city wanadakwa hata robo ya kura hawafikisha kuhesabu.

Hakujipanga yule Mzee....

2020 tunataka Mgombea uRais wa Upinzani mwenye mbinu zote hizo!! Na jibu ni jepesi sana Tundu Antipas Lissu.
 
Sawa lakini tunachosema Membe kuhamia upinzani July, 2020 na miezi mitatu baadaye apewe nafasi ya kupeperusha bendera ya upinzani kugombea Urais siyo sawa hata kidogo.
Lowasa alipata kura mil 6 Magu Mil 8 km sikosei na alihamia CDM miezi 3 tu kabla ya uchaguzi
6 Mil si mchezo ujue

Its obvious Membe hana upepo/nyota ya Lowassa ila Upinzani wakiwa na mgombea mmoja tu wa Urais huwezi jua
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Naona mgombea akiwa mmoja unaweza kuwa nzuri zaidi lakini shida bado ipo,
1:Act 2015 walikataa kujiunga navyama vya upinzan vingine wao wakasimamisha mgombea wao.
kwanin leo watake vyama viungane tena kwa gia kwamba Membe wa act do awe mgombea? ????????
Labda Membe awe mgombea mwenza Lisu awe mgombea urais, vinginevyo......
 
Kada La CCM limeanzisha Mada,

Special kwaajili ya "Kuyagonganisha Vichwa" Misukule ya Vyama halafu lenyewe limekaa kando lina SIP WINE.

Very stupid.

Tusubiri " Magu's Ubatizo wa Moto Part 2"

Kumbe Bado Hamjajitambua.
Yaani huyu ngosha ni 'genious'. Hakuna kada ambaye huwa anafanikiwa kuwachezesha 'ndombolo ya solo' hawa nyumbu wa Mwamba. Yaani kilasiku wanacheza muziki wake vizuri sana....Teh teh teh..
 
Nimemsikiliza Zitto na sababu yake/ zake kwanini suala la Membe kuhamia kwenye chama chake halitokuwa kama ilivyokuwa kwa CHADEMA na Lowassa na Sumaye na wengineo.

Sababu zake kuu ni kwamba hao waliohamia CHADEMA kipindi kile hawakujiona au hawakuonekana kuwa ni sehemu ya ‘movement’.

Pia, eti hawakujiona au kuonekana kuwa walikuwa ni sehemu ya ‘familia’ ya CHADEMA.

Muda utazungumza tu. Ila Zitto inabidi awe mwangalifu na uchaguzi wa maneno yake.

Kwenye hili nadhani Bw. Zitto anaathiriwa na kuwa ‘prisoner of the moment’.

Natumaini yeye na ACT yake watakuwa na mipango baada ya uchaguzi ujao baada ya kushindwa.

Maana ushindi huwaunganisha watu na ushindwaji hugawanyisha.

Kutokana na maelezo ya mh zitto wakuweka wazi maana ya kuwa familia ktk chama na akatolea mfano wa maalim seif kuwa amekuwa sehemu ya familia lakini tuelewe maalim hakutokea ccm yy alikuwa ni mpinzani nasiasa za ipinzani alizijua kwa hiyo yy ni tofauti na mtu alietoka chama tawala lakini nakumbuka lowasa na sumaye walijumuishwa ktk familia ya cdm walikuwa ni wajumbe wa kamati kuu ya cdm na ilibidi wasubiri uchaguzi wa chama kama wangelihitaji nafasi za juu cdm hawana vyeo vya fadhila cheo ni juhudi zako hata hivyo membe hajapewa nafasi yoyote ya juu bado ni mgombea tu wa uraisi kama alivyokuwa lowasa cdm
 
Naanza kuamini mbowe anaendesha siasa tanzania.... alianza kuvuna wanachama nguli toka vyama vingine, wengine wakaiga ikawa ndo trend na ss wanajifanya mamaster.... ss ameona hailipi ameachana nayo... wengine bado wanapita mule mule......

Gia itakayobadilishwa saiz ni hakika itawashangaza wengine km kawaida na wataiga...
 
Mbona hili ni rahisi sana.

Lowasa kuhamia CHADEMA, ajenda yake ilikuwa ni moja tu - Kutafuta urais, hapakuwa na sababu nyingine yoyote iliyomfanya ahamie CHADEMA; kwa hiyo baada ya kuukosa urais, hapakuwa na sababu ya kumfanya aendelee kubaki CHADEMA.
Alipopewa misukosuko toka huko alikokukimbia akaona heri ajisalimishe.
Hapo jambo gumu lipo wapi hadi watu kuumiza vichwa vyao juu yake?

CHADEMA, na wao walikuwa na ajenda yao, matamanio ya kushika madaraka.

Walidhani mwonekano aliokuwa nao Lowassa baada ya kukatwa ungeweza kukidhi matamanio yao hayo.
Ndani ya chama chao kwa wakati huo hawakuwa na tegemeo lolote la mtu ambaye angepambana kuwaletea ushindi.

Chama chochote cha siasa lengo ni kupata ushindi.
Ushindi ulipokosekana, wakaendelea kuwa na matumaini kuwa mgeni wao atawaletea mbinu na uzoefu aliokuwa ameujenga kwa muda mrefu akiwa CCM. Lowassa hakuonyesha dalili zozote za kuwa na uongozi wa aina hiyo. Kwa hiyo akabaki kuwa mzigo tu.

Uchaguzi wa 2015, ulikuwa uwe ushindi wa Lowassa. Yule Lowassa, Waziri Mkuu wa Kikwete angekuwepo kwenye kampeni za uchaguzi wa 2015, Magufuli asingepiga kona.

Kwa bahati mbaya, Lowassa wa enzi za Kikwete hakuwepo kuchukua ushindi ule.
Lowassa alishindwa kwa mwonekano wake aliouonyesha kwenye kampeni
 
Zitto anaongea tu, miaka yote ya utumishi wa Membe huko Serikalini aliwahi kumsikia Membe anaongea/kutetea chochote kwa maslahi ya wapinzani? Labda kuhusu tume huru,sheria mbovu za uchaguzi etc

Atakuja hapa atoe majibu ya siasa haina adui wa kudumu bla bla bla.

Membe ni Lowassa part 2 yule.
Kwa hili Zitto sipo naye
 
Mbona hili ni rahisi sana.

Lowasa kuhamia CHADEMA, ajenda yake ilikuwa ni moja tu - Kutafuta urais, hapakuwa na sababu nyingine yoyote iliyomfanya ahamie CHADEMA; kwa hiyo baada ya kuukosa urais, hapakuwa na sababu ya kumfanya aendelee kubaki CHADEMA.
Alipopewa misukosuko toka huko alikokukimbia akaona heri ajisalimishe.
Hapo jambo gumu lipo wapi hadi watu kuumiza vichwa vyao juu yake?

CHADEMA, na wao walikuwa na ajenda yao, matamanio ya kushika madaraka.

Walidhani mwonekano aliokuwa nao Lowassa baada ya kukatwa ungeweza kukidhi matamanio yao hayo.
Ndani ya chama chao kwa wakati huo hawakuwa na tegemeo lolote la mtu ambaye angepambana kuwaletea ushindi.

Chama chochote cha siasa lengo ni kupata ushindi.
Ushindi ulipokosekana, wakaendelea kuwa na matumaini kuwa mgeni wao atawaletea mbinu na uzoefu aliokuwa ameujenga kwa muda mrefu akiwa CCM. Lowassa hakuonyesha dalili zozote za kuwa na uongozi wa aina hiyo. Kwa hiyo akabaki kuwa mzigo tu.

Uchaguzi wa 2015, ulikuwa uwe ushindi wa Lowassa. Yule Lowassa, Waziri Mkuu wa Kikwete angekuwepo kwenye kampeni za uchaguzi wa 2015, Magufuli asingepiga kona.

Kwa bahati mbaya, Lowassa wa enzi za Kikwete hakuwepo kuchukua ushindi ule.
Lowassa alishindwa kwa mwonekano wake aliouonyesha kwenye kampeni
Tume ingekuwa huru Lowasa leo angekuwa Rais
 
Chadema wasikubali kabisaaaah, wao wawe bizze na lissu.
 
Kwahapa inavyoonekana ni kuwa ACT watanufanika zaidi kwa Membe kuliko yeye atakavyofaidi kwa chama Zitto anaangalia miaka ijayo tena uchaguzi wa 2025 au 2030 ACT hakitokuwa kama kilivyokuwa hivi sasa
 
Back
Top Bottom