Zitto: IGP amemdhalilisha Waziri Gwajima na Rais Samia

Zitto: IGP amemdhalilisha Waziri Gwajima na Rais Samia

Zitto amesema IGP Sirro anapaswa kujiuzulu maana amekataa kutii amri ya askari wa mwamvuli wa Rais Samia Suluhu kwa kukataa kumkamata Askofu Gwajima.

Na kwa kufanya hivyo Sirro amegoma kutii amri toka kwa Rais SSH.

Chanzo: StarTV medani za siasa.
Zitto aseme tu ukweli asituongopee, Sirro anawanyoosha kweli kweli na wapinzani hawamtaki sasa Zitto anataka kujificha kwenye suala la huyo mama mtestiwa mitambo kama pointi ya kumuondoa Sirro
 
Tatizo gender
Anacheka na nyani? Atavuna mabua. Yaani unaingia ikulu na serikali ya mtu mwingine?
Kwa taarifa tu ni kwamba Gwajima hapongani na wazir wa afya. Anapingana na raisi.
Gwajima na gwajima walikuwa na msimamo sawa juu ya covid.
Alipokuja mama ndo alitangaza chanjo huyu mama ni mgeni kwenye siasa za Tanzania.
Asome historia za kina jumbe na wengine
Acha ninywe konyagi yangu
 
Hizi chanjo zinamatatizo nini?
Zitto vipi yuko salama?
 
Kuna viumbe hapa duniani vikikosa pesa na akili vinakosa kabisa. Umaskini ni shida. Mwacheni Gwajima atumie haki yake kikatiba.

Ningemuona wa maana kama angelipigania swala la katiba mpya ipitishwe, na sio kujibishana na wanawake, ictoshe yule ni shemeji yake.
 
Fiksi zipi ?Kwani kifo hupiga hodi ?Mgonjwa kuendelea vizuri mara kifo kinamchukua. Hapo Uongo uko wapi ?
😂 Vee uliandika nini kuhusu marehemu? Nimecheka sana nimekumbuka comment nyingine mtu akikuambia eti "sina imani na wewe, ulituambia anaendelea vizuri mara akabinuka" 😂😂😂😂 Inachekesha
 
😂 Vee uliandika nini kuhusu marehemu? Nimecheka sana nimekumbuka comment nyingine mtu akikuambia eti "sina imani na wewe, ulituambia anaendelea vizuri mara akabinuka" 😂😂😂😂 Inachekesha
Alikuwa anaendelea vizuri. Sema akazidiwa.
 
Kwa mujibu wa katiba yetu Kazi ya police ni kutii maagizo ya mwanasiasa bila kuhoji inafaa igpu ajipeleke mwenyewe lockup kwa kukaidi kutii maagizo
 
Dorothy aliagiza “majeshi yote”. Aliagiza kama nani? Sirro yupo sahihi.

Hatuwezi kuanzisha au kuendeleza hii culture ya kutishiana kukamatana baada ya watawala kuzidiwa hoja
 
Zitto amesema IGP Sirro anapaswa kujiuzulu maana amekataa kutii amri ya askari wa mwamvuli wa Rais Samia Suluhu kwa kukataa kumkamata Askofu Gwajima.

Na kwa kufanya hivyo Sirro amegoma kutii amri toka kwa Rais SSH.

Chanzo: StarTV medani za siasa.
Siku hizi Zitto amekuwa mjinga, polisi hawaongozwi na amri za waziri, hii tabia ya kiongozi wa serikali kuamuru mtu akamatwe pasipo kufuata sheria inatakiwa ikomeshwe , haya ndio tunayoyapinga na ndio hata hao akina Zitto wanataka katiba mpya ili kupunguza mamlaka walizonazo watawala wetu, tusirudi nyuma ,hapa ilitakiwa Sirro apongezwe, tumeshuhudia wanasiasa kwa kujipendekeza tu wakiamuru wakuu wa polisi wakamate watu hovyohovyo kisa anayetoa amri ni mteule wa raisina ndio maana hata wengi wanataka wakuu wa wilaya na mikoa wasiwe wenyeviti wa kamati za usalama na ulinzi, Zitto aacache na akome kujipendekeza kwa mama. hatua alizochukua sirro ni za kupongezwa na mwanzo mzuri kwa ustawi wa nchi.
 
Ningemuona wa maana kama angelipigania swala la katiba mpya ipitishwe, na sio kujibishana na wanawake, ictoshe yule ni shemeji yake.

Unaingilia uhuru wa mtu kuamua maamuzi yake binafsi. Kama ungemuuliza yeye angesema angekuona wa maana kupigania suala la afya kwanza. Katiba inaruhusu mtu kuwaza tofauti na kuwa na mtizamo wake tofauti. Sasa unapomlazimisha mtu afikiri kama wewe tayari unakuwa dikteta. Ushemeji na afya uhusiani. Wajibishane kwa hoja tu. Hayo mengine sisi hayatuhusu. Tuheshimu katiba. Tutetee katiba.
 
Zitto amesema IGP Sirro anapaswa kujiuzulu maana amekataa kutii amri ya askari wa mwamvuli wa Rais Samia Suluhu kwa kukataa kumkamata Askofu Gwajima.

Na kwa kufanya hivyo Sirro amegoma kutii amri toka kwa Rais SSH.

Chanzo: StarTV medani za siasa.
Tuhuma ni za rushwa, sirro anahusikaje? Mbona Salum Hamduni yuko kimya na hamsemi? Shenzi zenu
 
Unaingilia uhuru wa mtu kuamua maamuzi yake binafsi. Kama ungemuuliza yeye angesema angekuona wa maana kupigania suala la afya kwanza. Katiba inaruhusu mtu kuwaza tofauti na kuwa na mtizamo wake tofauti. Sasa unapomlazimisha mtu afikiri kama wewe tayari unakuwa dikteta. Ushemeji na afya uhusiani. Wajibishane kwa hoja tu. Hayo mengine sisi hayatuhusu. Tuheshimu katiba. Tutetee katiba.

Swala la afya amwachie waziri wa afya ndiyo jukumu lake, na ndiye musemaji wa serikali. Na co yeye kama mbunge wa kawe!!! Huoni kuwa wamemdhalilisha uyu Dr dorothy kwa speech iliyotolewa in church!!!, na hata Rais vile vile wamemzalilisha mno. Mbona wakati wa Magu hakuwa mpingaji na kuilaumu serikali icpokuwa kwa uyu mama!!! Angefanya jambo lamaana muno kulalamikia katiba mpya ipitishwe, tozo za miamala, kodi za majengo kupitia makato ya luku, ushuru wa magari uko juu mno, kodi za TRA, Bima/Insurance n.K, bei ya umeme, bei ya vyakula n.k.,,hapo ningempa tano babaa.

U know that uyu mama wamemuona mpole muno ndiyomaana wanafanya wanavotaka. Na hela inampa mtu kibuli muno kama hujui. Anapinga chanjo, na wengine wanamuunga mkono without reflection uyu mtu isijekuwa ashapata chanjo anatuchezea akili zetu 🤣🤣🤣


Mungu asaidie Katiba mupya mama apitishe, hope everything will be fine mkuu.
 
Zito mzito sana!! Hajui kama ameshachuja!! Anajidhalilisha!! Rais atamdharau na hana haja ya kumjibu!! IGP naye atamďharau, hana haja ya kumjibu!! Hata na mimi namdharau sina haja ya kumjibu!! ZITO kachuja vibaya!! Kwa hili ataona jinsi alivyochuja!!
 
Hakuna suala la mama au upole hapo. Suala ni haki ya kikatiba. Kwa nini pia unapodai katiba mpya asiachiwe waziri wa katiba na sheria? Ni haki kila mtu kuzungumzia afya yake. Mi nadhani katika hili tusiweke ushabiki,udini na uvyama. Aachiwe haki yake Gwajima kuzungumza anachoamini.ili mradi havunji katiba.

Swala la afya amwachie waziri wa afya ndiyo jukumu lake, na ndiye musemaji wa serikali. Na co yeye kama mbunge wa kawe!!! Huoni kuwa wamemdhalilisha uyu Dr dorothy kwa speech iliyotolewa in church!!!, na hata Rais vile vile wamemzalilisha mno. Mbona wakati wa Magu hakuwa mpingaji na kuilaumu serikali icpokuwa kwa uyu mama!!! Angefanya jambo lamaana muno kulalamikia katiba mpya ipitishwe, tozo za miamala, kodi za majengo kupitia makato ya luku, ushuru wa magari uko juu mno, kodi za TRA, Bima/Insurance n.K, bei ya umeme, bei ya vyakula n.k.,,hapo ningempa tano babaa.

U know that uyu mama wamemuona mpole muno ndiyomaana wanafanya wanavotaka. Na hela inampa mtu kibuli muno kama hujui. Anapinga chanjo, na wengine wanamuunga mkono without reflection uyu mtu isijekuwa ashapata chanjo anatuchezea akili zetu 🤣🤣🤣


Mungu asaidie Katiba mupya mama apitishe, hope everything will be fine mkuu.
 
Dini ni imani ya mtu binafsi haiingiliwi na ili mradi haivunji katiba. Gwajima anatumia haki yake kikatiba. Chanjo ni Hiyari. AnAyechanjwa anajitangaza amechanjwa na asiyechanjwa anajitangaza hajachanjwa sasa kwa nini mwingine alazimishe watu kuchwanjwa? Au kutochanjwa? Jibuni maswali ya Gwajjma. Acheni blah blah.... Jibuni ili ionekane amepotoka wapi... Msianike upumbavu wenu mkitaka watu wakausage wapikie uji.


Hii nchi haina dini kikatiba.
Masuala ya serikali hayajibiwi kwenye nyumba za ibada Kwa kuweka msimamo wa kidini.

Maswali ya Gwajima yameshajibiwa kitaalam na wa taalam wengi ndani na nje ya nchi.
Suala la chanjo lipo dunia nzima na hakuna atakayekwepa ni suala la muda tu na kujifariji.

Sayansi siku zote inapoletwa duniani watu wa dini wamekua wakiipinga lakini baadae wao ndio wanakua mstari wa mbele kunufaika nayo.

Oooh wazungu wanataka kutumaliza waafrika wakati kila kitu cha kisayansi kinatoka kwao. Sio kila mzungu ni mbaya.
Wenzetu hawalali ili waondoe matatizo yao yanapojitokeza. Gwajama anapinga chanjo kama nani?
Kama anachanjo yake ailete ili apinge iliyopo sio kupinga dawa kwa maneno ya mitandaoni.
Sayansi inapingwa kisayansi kwa kuingia kwenye maabara sio kama mabishano ya kisheria kahakamani.
Ndio maana hata mahakamani ushahidi wa kitaalam unatolewa na wataalam sio vinginevyo.
Gwajima anataka ajibiwi na wataalam kama nani? Rais alishakaa na wataalam akaunda mpaka tume ikampa majibu ya kitaalam sasa Gwajima anataka aunde tume yake au anataka tu kumsumbua kwa sababu Rais aliyepo hatumii mkono wa Chuma au kwa sababu Rais sio wa kabila lake au dini yake??
Acheni kuyumbisha maamuzi ya serikali.
Gajima ahubiri watu waache ulevi,uzinzi, rushwa, ufisadi,wizi wa kura,dhuluma ,uonevu ,kubambikia watu Kesi za uongo ,ulawiti,ushoga, uasherati, ushirikina ,uchawi ,kupenda pesa kupita kiasi.kuua n.k.
Hayo ndiyo Mwenyezi Mungu anayotaka yaachwe ili dunia iwe sehemu salama ya kuishi.
Watu wasipoacha dhambi bado pataibuka gonjwa lingune tena baya zaidi mana dunia inaangamia kwa sababu ya uovu na sio chanjo.
Yaani unatangazia waovu kuwa watakua salama bila kuacha uovu wao.
Haiwezekani.
Sayansi inakimbia kasi sana yale mambo ya kufanya tafiti miaka kumi yamepitwa sana na wakati.
Sasa hivi tafiti zinafanywa kwa kasi kubwa lakini pia ikimbukwe kuwa korona na magonjwa yanayofanana nayo yapo kwa kipindi kirefu hivyo tafiti zilishaanza muda mrefu kwa ajili ya magonjwa yanayoshabihiana nayo.
 
Kuna jambo halipo sawa....nyuma ya GwajiBoy kuna kundi kubwa la Friends of Mwendazake linalojipanga kwa 2025....hili ndilo limegomea katiba isiguswe...stay turned..picha linakuja.
 
Back
Top Bottom