Zitto Kabwe apendekeza TANESCO wauze hisa(20%) fedha itakayopatikana ilipe madeni, Waziri Makamba atoa maagizo

Kwanini usitoe mchango wako tu kama wewe huta nunua labda kuna wengine wata nunua. Kwa uelewa wangu ni kwamba Zitto kashauri tu na ushauri umepokelewa sio kwamba ndio una tekelezwa
 
Si mpaka wawe accountable...wakihujumu nchi kwa maslahi yao nani wakulaumiwa..ni sawa sawa na kuwinda fisi ndani ya bucha
acha tuwe positive kwasababu wazo limeletwa with good intention, nafikiri lazima litajadiliwa kwa maslahi mapana ya Tanzania.
 

Ni mchanganyiko juu ya mchanganyiko
Magufuli alirudisha Tanesco Utumishi
Makusanyo yanapelekwa hazina .
Halafu wanaomba bajeti ya chochote kile kutoka hazina..
Hata watumishi wengine wanahamishwa kupelekwa Halmashauri n.k..

Sasa katika huo mchanganyiko ulete hili la DSE...pata picha
 
Reactions: SMU
Lazima ukose akili na maarifa ndiyo ukanunue hisa za TANESCO. Shirika halijawahi kupata faida hata mwaka mmoja tangu lianzishwe, ukanunue hisa, kwaajili ya nini?
 
Sio bei gani,issue je hisa zangu nitapata faida gani? Shirika linaendeshwa kijanja janja unategemea nini?
 

Sasa shirika la Tanesco hata mkaguzi mkuu wanamkwepa hivyo hawapo kwenye ripoti. Leo hii ni sababu gani ya mwekezaji kununua hisa za kampuni ambayo mahesabu yake hayako wazi? Au ni wale wawekezaji ambao hawajui kama mashirika mengine yanayotumia pesa za makato hii sio sawa. Shirika liwe na uwazi kwanza likaguiwe mikataba yote na wawekezaji wajue litaenda vipi kwa hasara maana mikataba mingi ni mibaya sana
 
Walianza Richmond halafu Dowans kuuzia Tanesco umeme kupitia mikataba mibovu!!

Now they are back to take the all honeypot!!
 
Kwa madeni ya Tanesco ni kiasi gani?
Serikali imeshindwa kuyalipa?
Madeni ya Tanesco ni ya muda mrefu. Wakishauza hizo hisa kulipa madeni. Halafu baadae ikarudi kwenye madeni tena. Watauza hisa zilizobakia kulipa madeni??
 


TANESCO wanatengeneza hasara kwenye operation tu kabla ya ata kulipa madeni.

So ata ukilipa madeni yao yote bado shirika litatengeneza hasara tu.

Halafu 20% ya hisa itazalisha kiasi, kwa bei ya soko? Lini shirika lilifanyiwa market valuation kuona 20% ya hisa inaweza kukusanya zaidi ya tsh trillioni 5 na zaidi ili kufanya uwekazaji mwingine huyo Zitto aliopendekeza.

Huo ndio wasiwasi wangu kwa Makamba anakuwa na grand ideas bila ya hata kufikilia practicality wakishakutana kule Twitter na wasomi uchwara wengine kutwa kupongezana ujinga.

 
Hatutaki udalali kwenye TANESCO

Tunataka serikali imiliki hisa zote za TANESCO 100%, namna hii maana yake wananchi wote tunaimiliki TANESCO yetu

Hii tabia ya kuuzauza hisa kwenye kila kitu(ambazo zinaenda kuishia mikononi mwa Matajiri wachache anyway) ni tabia ya kukosa ubunifu.

TANESCO is our pride msituletee mambo ya kuuza mashirika muhimu kama alivyofanya Mkapa kwenye benki ya NBC
 
Walianza Richmond halafu Dowans kuuzia Tanesco umeme kupitia mikataba mibovu!!

Now they are back to take the all honeypot!!
Yaani hata mzee Rugemalira hajspumzika wanataka kuturudisha kule kule!
 
Huyu Zitto ni mtu wa madili tu hamana kitu hapo .Shida ya Tanesco ni mikataba ya kilaghai .Vunjeni hiyo mikataba shirika lipate mapato liweze kijiendesha kwa faida

Duniani kote Huwa Kuna mashirika ya uma ambayo Huwa ni Mali ya Nchi kwa ajili ya Usalama wake kiusalama na kiuchumi,mashirika kama Reli na umeme Huwa ni moyo wa nchi.
 
Wazo la kijinga sana kuuza nyumba ya watoto au kuuza mbegu ili kulipa deni.
Badala alete mbinu Tanesco ipate faida ili deni lilipwe kupitia faida yeye anataka tuuze mbegu kulipia deni
Waambie wavunje mikataba ya kihuni ili shirika lipate mapato ljiendeshe kwa faida
 
Hivi mnaweza kutufafanulia ni kwa vipi Tanesco inapata hasara?

Kila kitu tunalipia, hii hasara inatokana na nini?
Bosi wangu Tanesco inapata hasara kwa Sababu ya mikataba mibovu ya kitapeli ndo tatizo Liko hapo.Vigogo wezi wananufaika kwa njia hiyo na siku hii mikataba ikuvunjwa shirika litaanza kupata faida,hii ishu ni ngumu sana maana walnaufaika ni watu wazito ukionekana unwafatilia unapotezwa.
 

Taratibu mkuu. Hii ni nchi ambayo shirika lake mfu la ndege (ATCL) lilipata faida kubwa na kutoa dividend ya mabilioni mwaka 2020.

Usijeshangaa hizo hisa za TANESCO zikauzwa wakanunua unaowaona “wapumbavu” halafu ukasikia baada ya miaka miwili wamegawiwa mabilioni ya dividend kutoka faida ya “capacity charges”. The guys are wizards with all sorts of accounting gymnastics.
 
Kwa vitabu 2018. Tanesco total assets ni trilioni 8.7?!!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…