Zitto Kabwe asubiriwa na Bunge kueleza lengo la barua yake Benki ya Dunia kuzuia mkopo wa kuboresha Elimu (SEQUIP)

Tulikataa USD 500 million za Millennium Challenge Account mwaka 2016 na tumedunda miaka yote hiyo bila tabu. Sasa tatizo liko wapi kama tunanyimwa million 500 leo?

Inaelekea Zitto yuko sawa .... Pesa ya kampeni itakuwa imepwelea!!
 

Sema mtalazimisha ushindi. Lakini hilo halitawasaidia, unadhani anahitaji kuwa bungeni ili atoe maoni yake na kusikilizwa? Tutaanzisha petition ya bidhaa za Tanzania kususiwa kimataifa hadi mshike adabu. Na sio kazi kubwa sana.
 
Asingemsikiliza,akithubutu kufanya hivyo(Akimpa nafasi ya kuongelea hiyo Sera Bungeni hata yeye Ndugai angekiona cha moto tokea kwa jiwe na wapambe wake.
Namshauri kama anaona vipi aruhusu muswada wa Tume Huru ya Uchaguzi na Katiba ya Wananchi.
Akiwezesha hilo tutampigia kampeni arejee Binge LA 12 na awe Spika wake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kazi za mbunge zimeanishwa wazi kabisa hiyo ya kuwasiliana na benki ya dunia kwa kutumia Ofisi ya bunge na karatasi yenye nembo ya bunge haimo kwenye kazi za mbunge.
Na hilo nalo pia ni kosa jingine kubwa. Barua aliyoiandika hakuwa ametumwa na Bunge, ilikuwa ni yake binafsi, na hakutakiwa kuisaini akiwa anaonyesha kuwa ni Mbunge wa JMT, bali alitakiwa aisaini akiwa anaonyesha kuwa ni Kiongozi Mkuu wa Chama Cha ACT. Mandate iliyomfanya aandike barua hiyo ni Uongozi wake ndani ya chama anachokiongoza na si kama Mbunge wa JMT. HIlo ni kosa jingine kubwa, tena kubwa asana
 
Zitto kwenye barua yake kwenda WB kaweka icon ya bunge la Tanzania bila idhini ya bunge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…