Zitto Kabwe ''awashukia'' vikali wanaozodoa ACT-Wazalendo kwa kushiriki Uchaguzi mdogo Kigoma

Lakini Fundi…CHADEMA hao mbona wameshiriki chaguzi nyingi tu chini ya hii hii tume ambayo wameisusia sasa?

Kama hii tume ya sasa si huru, ina maana tume za 2015, 2010, na 2000 zilikuwa huru?
Si unajua kisa cha cholera kumvunja ngamia mgongo. Tukiwa wakweli, chaguzi za 2019 na 2020 zilipitiliza kwa brazenness. Kabla ya hapo palikuwa na modicum ya kiaibu. Their brazenness ndio unawafanya washindwe kutoa matokeo ya kila kituo mpaka leo. Walimgusa kipofu wakati wa kula. In all honesty, unaweza kuamini kabisa kuwa wagombea wote wa Chadema hawajui kujaza fomu? Na kuwa nchi nzima ni wabunge wawili tu wa upinzani ndio wameshinda? Watu walitiwa ndani dakika chache kabla ya deadline ya kurudisha fomu ili mgombea wao apite bila kupingwa! Wasimamizi walijifungia au walihama ofisi ili wasipokee fomu za wapinzani halafu voila, wanajitokeza kumtangaza mgombea wa CCM kuwa mshindi! Na hayo ni sehemu tu.

Watu mpaka leo wanasota magerezani kwa sababu tu walimshabikia mpinzani. Na wengine baada ya kusota muda mrefu wameachiwa bila hata aliyewashitaki kujisumbua kuwasilisha ushahidi!

Anaeshangaza ni yule anayeamini kuwa waliofanya yote hayo watamruhusu ashinde kirahisi. Kwa kifupi hamna Tume iliyokuwa huru lakini hii ya sasa imezidi. Badala ya kuweka kidole kwenye mzani wameukalia kabisa.

Amandla...
 
Dah!

Kwa hiyo Bw. Fundi tatizo ni brazenness ya election irregularities na si muundo wa tume unaoifanya isiwe huru?

Kwa maneno mengine, kama hayo uliyoyataja yasingetokea kwa kiwango na kiasi kile, ingekuwa ni sahihi kwa CHADEMA kuendelea kushiriki chaguzi kwa sababu walau huwa wanaachiwa washinde chaguzi kadhaa za kibunge?
 
Ndio ulikuwa mtizamo wao. Waendelee kushiriki wakati wanapiga kelele. Naona wametambua kuwa ni kupoteza wakati tu kufikiria tu kuwa CCM watakubali Tume huru bila shinikizo. Their only recourse ni kususa maana otherwise wataonekana wapuuzi. Of course, CCM wanaamini kuwa njaa itawafanya wabadili msimamo hata bila Tume huru. I think they are in for a nasty surprise.

Amandla...
 
Kwa hiyo Zitto yeye yuko so sophisticated eeh?

He is so deluded on so many levels!
Contention hapo ni ku- concede. Wanataka hata ukishindwa unatakiwa kutoa sababu, umeibiwa kura, polisi wame wazuia kupiga kura, tumepigwa nabomu. nk.
Kukataa hivyo na kusema uchaguzi ulikuwa huru na haki. Ndicho anachozungumzia Zitto . Wapinzani wanachulia kuwa anaifagia tume ya Uchaguzi.
 
Chadema walisusia uchaguzi jimbo la Lazaro Nyalandu Singida kwa madai ya Tume huru ya Uchaguzi na Katiba mpya

Wakaja kushiriki Uchaguzi ndogo wa Kinondoni Wakasusia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Sababu haukuwa na manufaa yoyote kwa mbowe na genge lake...wakaja kushiriki uchaguzi Mkuu ili kupata ruzuku na nafasi za viti maalumu ambavyo kina mdee walikuja kuviwahi. Nyakati zote hizo hapakuwa na Mabadiliko yoyote

Lipumba nae baada ya uchaguzi Mkuu akaitisha Press Conference akasema hawatashiriki uchaguzi wowote hadi Tume Huru ya Uchaguzi ipatikane lakin ghafla uchaguzi uliofuata ndani ya miezi miwili kule Pemba wameshiriki

CHA AJABU WANAMSAKAMA ZITTO KABWE KWA KUSHIRIKI UCHAGUZI MDOGO MUHAMBWE NA BUHIGWE
 
Many are using excessive force to turn JF a Kindergartens platform.
 
Mkuu tuombe uzima.

Ni kwasababu hakuna uchaguzi serious hivi karibuni.

Tusubiri tuone CHADEMA haitakuja kushiriki uchaguzi wa aina yoyote chini ya Tume hii mpaka pale CCM watakapokuja kuibadili ili iweze kutoa matokeo ya kuwafurahisha CHADEMA.
 
Tunapambana tukishiriki naTunashiriki tukipambana.
 
Huyo muha mtabishana usiku kucha.kuna makabila hii nchi ni kuyapuuza tu.
 
Zitto Zuberi Kabwe, tulio wengi tuna-miss uwepo wako Bungeni.
Mimi natamani kukuona ukiteuliwa kuingia Bungeni kwenye nafasi za Rais wa JMT.
Pamoja na yote hayo, jiongezee ustaarabu. Ni muhimu.
Sentensi zako tatu za mwisho zinakuwekea wingu la mashaka kwenye haiba yako.
Huna sababu ya kutamka uliyotamka kwenye sentensi tatu za mwisho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…