Zitto Kabwe: Rais Mwinyi ameteua mtu aliyevuruga uchaguzi wa 2020

Zitto Kabwe: Rais Mwinyi ameteua mtu aliyevuruga uchaguzi wa 2020

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Zitto.jpg

"Suala la Rais Mwinyi kumteua mtu aliyehusika kuvuruga uchaguzi wa 2020 kuwa Mkurugenzi wa ZEC, HALIKUBALIKI. Tumeamua kurudi chini kwa Wanachama wetu. Ni wao waliotaka tuingie kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa, wao pia ndio watakao amua hili," kauli ya Zitto Kabwe akiwa Kata ya Mchoteka, Jimbo la Tunduru Kusini, Ruvuma.

Anasema: “Ziara hii ya Tunduru ilipaswa kufanywa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, lakini imebidi aongoze kikao cha Kamati Maalum ya Kamati Kuu ya ACT Wazalendo Zanzibar, Kujadili Suala ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Rais Mwinyi ameteua mtu aliyesimamia uchaguzi wa 2020, sisi tumeamua kurudi kwa Viongozi na Wanachama wetu ngazi ya Matawi, tutawaambia hali ilivyo, na watuambia la kufanya.”
 
Zitto anataka kutuambia kwamba maamuzi yao kujiunga SUK yalitokana na ridhaa ya wananchi wapi? wale waliopigwa mabomu ya machozi na kuchomewa nyumba zao kule Pemba au wengine?

Kama ni hao Zitto anatudanganya, sikuwahi kuona popote wale waathirika wa uchaguzi wa 2020 kama waliwahi kulipwa fidia ya madhila waliyofanyiwa, na kama Zitto na ACT walienda SUK ili kuwasemea wale waathirika, mpaka leo walikuwa wanafanya nini kule serikalini kama waathirika wale hawakupewa stahiki zao?

Ukweli ni kwamba, ule ndio ulikuwa wakati wa Zitto na ACT wenzake kurudi kwa wananchi na kuwaambia CCM wamegoma kuwalipa fidia, hivyo wajitoe SUK au vipi, lakini sio leo kurudi kwa wananchi kisa aliyeteuliwa na Mwinyi hawamtaki, wao wanawaza uchaguzi tu ili uwape vyeo vya kula, hawa wanaonesha jinsi walivyo selfish.
 
View attachment 2418431
"Suala la Rais Mwinyi kumteua mtu aliyehusika kuvuruga uchaguzi wa 2020 kuwa Mkurugenzi wa ZEC, HALIKUBALIKI. Tumeamua kurudi chini kwa Wanachama wetu. Ni wao waliotaka tuingie kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa, wao pia ndio watakao amua hili," kauli ya Zitto Kabwe akiwa Kata ya Mchoteka, Jimbo la Tunduru Kusini, Ruvuma.

Anasema: “Ziara hii ya Tunduru ilipaswa kufanywa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, lakini imebidi aongoze kikao cha Kamati Maalum ya Kamati Kuu ya ACT Wazalendo Zanzibar, Kujadili Suala ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Rais Mwinyi ameteua mtu aliyesimamia mauaji ya 2020, sisi tumeamua kurudi kwa Viongozi na Wanachama wetu ngazi ya Matawi, tutawaambia hali ilivyo, na watuambia la kufanya.”
ACHA UNAFIKA KAMA HAMLIDHIKI NA HUO UTEUZI JIONDOENI KTK SERIKALI YA UMOJA WENU NA CCM
 
Fuatilieni historia ya Zitto vizuri kwani hamtajiumiza kuumiza kichwa juu yake.
Kwa ujumla Zitto hayuko mbali historia kujirudia kwa uzuri au kwa ubaya ila yy kama yy ameshajua kisiasa yuko wapi. Ndo maana anaishi hayo anayoyaishi kwani ndo njia aliyoiona itamfikisha mapema kumbe mwisho kiza
 
Kombati za CHADEMA zinapendeza Sana hapo sijui huyo ni zito kabwe au kiongozi wa wilaya ACT-tunduru
 
WANACHAMA walitaka hivyo, Sawa na ninyi viongozi mlitakaje? Isije kuwa kama boss wa mastone aliyesema "wananchi walikubali tozo, baada ya muda Big Boss akataka liangaliwe na hilo pia.
 
View attachment 2418431
"Suala la Rais Mwinyi kumteua mtu aliyehusika kuvuruga uchaguzi wa 2020 kuwa Mkurugenzi wa ZEC, HALIKUBALIKI. Tumeamua kurudi chini kwa Wanachama wetu. Ni wao waliotaka tuingie kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa, wao pia ndio watakao amua hili," kauli ya Zitto Kabwe akiwa Kata ya Mchoteka, Jimbo la Tunduru Kusini, Ruvuma.

Anasema: “Ziara hii ya Tunduru ilipaswa kufanywa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, lakini imebidi aongoze kikao cha Kamati Maalum ya Kamati Kuu ya ACT Wazalendo Zanzibar, Kujadili Suala ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa. Rais Mwinyi ameteua mtu aliyesimamia mauaji ya 2020, sisi tumeamua kurudi kwa Viongozi na Wanachama wetu ngazi ya Matawi, tutawaambia hali ilivyo, na watuambia la kufanya.”
Zitto aache hadaa zake za kishamba,lini walikaa na wanachama wao kuwauliza kama waingie SUK au la? Hata Maalim Seif alikubali kwa shingo upande kwani zitto alikuwa ameshakubaliana na watawala na yeye ndiye mwenye chama chake. Ila siku si nyingi Wapemba watamfanya kitu mbaya.
 
Back
Top Bottom