Zitto Kabwe: Vitabu nilivyosoma Mwaka 2022

Zitto Kabwe: Vitabu nilivyosoma Mwaka 2022

Safi sana Zitto, Sababu mojawapo ya kuwa na Watanzania wengi vilaza mitaani na katika nafasi muhimu za uongozi ni kwa sababu hawasomi vitabu.
Mbona ye msoma vitabu kawa mlamba viatu vya asiyesoma hata miongozo ya kuongoza nchi.
 
Mwaka huu unaomalizika 2022 nimebahatika kusoma vitabu mbalimbali 33 (2021:29, 2020:16, 2019:34). Ulikuwa mwaka mzuri kwa usomaji vitabu na pia mwaka ambao nilibahatika kupata zawadi nyingi za vitabu kutoka kwa marafiki zangu na ndugu zangu.

Nitaanza mwaka 2023, Mungu akijaalia kuvuka salama, nikiwa na karibu dazeni ya vitabu ambavyo sijasoma. Kama nilivyofanya mwaka jana, kutoka orodha ya mwaka huu nimeshatoa orodha ya vitabu 10 ninavyopendekeza watu kuvisoma mwaka ujao kama hawajavisoma.

Vitabu nilivyosoma mwaka huu kwa makundi mbalimbali ni kama ifuatavyo;

Riwaya
  • Magic of Saida – MG Vassanji
  • I am Semba – Ajeka&Fox
  • The Book of Secrets – MG Vassanji
  • The House of Rust – Khadija Abdallah Bajaber
  • Mtumwa kwenye Nchi Huru – Elizabeth Mramba
  • A Line In The River: Khartoum City of Memory – Jamal Mahjoub
  • We are all Birds of Uganda – Hafsa Zayyan
  • The In-Between World of Vikram Lall – MG Vassanji
  • Next In Line – Jeffrey Archer
  • Tea with Ms. Tanzania – Fayyaz Vellani
  • The Shadow King – Maaza Mengiste
Wasifu/Tawasifu
  • The Chancellor: The Remarkable Odyssey of Angela Merkel – Kati Marton
  • Njinga of Angola: Africa’s Warrior Queen – Linda M. Heywood
  • The Prime Ministers We Never Had: Success and Failure from Butler to Corbyn – Steve Richards
  • 38 Reflections on Mwalimu Nyerere – Ed. Mark Mwandosya and Juma V Mwapachu
  • Hani: A life too short – Janet Smith and Beauregard Tromp
  • Juhudi na Changamoto – Sheikh Ponda Issa Ponda
  • The Bhutto Dynasty: The Struggle for Power in Pakistan – Owen Bennett-Jones
  • Maisha Yangu – Khamis Abdallah Ameir
  • Revolution in Zanzibar: An American’s Cold War Tale – Don Petterson
  • The Tanganyika Way: A personal Story of Tanganyika’s Growth to Independence – Sophia Mustafa
Nchi ya mwaka, India
  • Indian Summer: The Secret History of the End of an Empire – Alex Von Tunzelm
  • Pride, Prejudice and Punditry: The Essential – Shashi Tharoor
  • Mamata Beyond 2021 – Jayanta Ghosal
  • The Rise of The BJP: The Making of the World’s Largest Political Party – Bhupender Yadav and Ila Patnak
  • India in a New Key: Nehru to Modi, 75 years of freedom and democracy – Narain D. Batra
Mchanganyiko
  • Time for Socialism – Thomas Piketty
  • Capturing Hope: The Struggle Continues for a New Malaysia – Mahathir Mohamed
  • Final Reckoning: An Insider’s View of the Fall of Malaysia’s Barisan Nasional Government – Romen Bose
  • The World for Sale: Money, Power and the Traders Who Barter the Earth’s Resources – Javier Blas and Jack Farchy
  • Sudan’s Unfinished Democracy: The Promise and Betrayal of a People Revolution – Willow Berridge, Justin Lynch, Raga Makawi and Alex De Waal
  • From Rebel to Ruler: One Hundred Years of the Chinese Communist Party – Tony Saich
  • Borderland: A Journey Through the History of Ukraine – Anna Reid
Heri ya mwaka mpya 2023

23/12/2022


ILANI: Kila mwaka, nikibahatika na kujaaliwa, huwa ninasafiri pamoja na familia yangu. Kwa muda sasa nchi ninayotembelea huchomoza kupitia vitabu nilivyosoma mwaka huo. Mwaka huu nimeamua kuweka kundi la Nchi ya Mwaka ili kuonyesha vitabu nilivyosoma kuhusu nchi husika. Mwaka 2022 ilikuwa India (Rwanda 2021).


Ama kwa hakika Muheshimiwa hongera sana kwa usomaji wa idadi ya vitabu hivyo na hili limenipa hamasa nami nijitahidi angalau kwa mwaka niweze kusoma vitabu japo vichache, kulingana na muda, vitakavyoweza kukuza ufahamu wangu wa mambo mbalimbali.

Elimuni ufunguo wa maisha, Elimu ni chakula cha ubongo na elimu zinapatikana katika njia mbalimbali ikiwemo njia ya kusoma vitabu, nataka niamini kupitia vitabu nk ndio siku zote umepata nguvu ya kujenga na kutetea hoja zako katika uwanja wa kisiasa na kijamii, kudos.

Muheshimiwa, Waafrika wengi na hususan Watz ni wavivu sana katika kusoma vitabu, ni wavivu katika kusoma hata vitabu vilivyoandikwa katika lugha ya Kiswahili (lugha mama) sembuse Lugha ya kiingereza!!, ni wavivu kusoma hata maandiko ya Dini, katiba ya nchi nk.

Muheshimiwa, tufanye nini ili kahamasisha watu kujenga tabia na tamaduni ya kusoma vitabu vyenye elimu za manufaa??--- Watz wanapenda kusoma magazeti, majarida ya udaku na tamthiliya zaidi kuliko kusoma vitabu vya elimu.

Hilo ndilo jambo muhimu sana jamii inatakiwa ihamasishwe kusoma vitabu kuliko kuelezea idadi ya vitabu ulivyosoma na matokeo yake umeyaona asilimia kubwa ya watu wametoa maoni ya kukushambulia kama kwamba wewe unaonyesha majivuno mbele yao Kwamba "you are a plorific reader", hii ni sawa na uende kijijini kwa watu wasiosoma kabisa na kuanza kuongelea jambo la muhimu kwa ajili yao katika lugha ya kiingereza 🤣 watakushangaa!!!, ndio maana badala ya watu humu kuhamasika na usomaji wako wa vitabu wamekuwa mbogo na hapohapo kukushutumu na kuingiza siasa kuhusiana na ugumu wa maisha tunayopitia nchini wakijua kwamba wewe ni political figure kitu ambacho ni irrelevant mada uliyoileta.
 
una muda wa kuchezea wewe yaani pamoja na vitabu hivyo bado unaendelea kununuliwa na kufanya udalali wa kisiasa bado una unafiki wa kumchukia Magufuli huku ukiungana na genge la wafuja Mali akina Malope ndio unatuambia vitabu vinaandika hayo kutwa unadhurula ulaya kwa wakoloni wetu wezi wa Mali zetu kuihujumu nchi ona Sasa tunauzia majrnereta na imeme unakatwa hovyo yaani uzungu mwingi umekupoteza kisiasa
Hiki kimemkimbiza mleta mada
 
Mwaka huu unaomalizika 2022 nimebahatika kusoma vitabu mbalimbali 33 (2021:29, 2020:16, 2019:34). Ulikuwa mwaka mzuri kwa usomaji vitabu na pia mwaka ambao nilibahatika kupata zawadi nyingi za vitabu kutoka kwa marafiki zangu na ndugu zangu.

Nitaanza mwaka 2023, Mungu akijaalia kuvuka salama, nikiwa na karibu dazeni ya vitabu ambavyo sijasoma. Kama nilivyofanya mwaka jana, kutoka orodha ya mwaka huu nimeshatoa orodha ya vitabu 10 ninavyopendekeza watu kuvisoma mwaka ujao kama hawajavisoma.

Vitabu nilivyosoma mwaka huu kwa makundi mbalimbali ni kama ifuatavyo;

Riwaya
  • Magic of Saida – MG Vassanji
  • I am Semba – Ajeka&Fox
  • The Book of Secrets – MG Vassanji
  • The House of Rust – Khadija Abdallah Bajaber
  • Mtumwa kwenye Nchi Huru – Elizabeth Mramba
  • A Line In The River: Khartoum City of Memory – Jamal Mahjoub
  • We are all Birds of Uganda – Hafsa Zayyan
  • The In-Between World of Vikram Lall – MG Vassanji
  • Next In Line – Jeffrey Archer
  • Tea with Ms. Tanzania – Fayyaz Vellani
  • The Shadow King – Maaza Mengiste
Wasifu/Tawasifu
  • The Chancellor: The Remarkable Odyssey of Angela Merkel – Kati Marton
  • Njinga of Angola: Africa’s Warrior Queen – Linda M. Heywood
  • The Prime Ministers We Never Had: Success and Failure from Butler to Corbyn – Steve Richards
  • 38 Reflections on Mwalimu Nyerere – Ed. Mark Mwandosya and Juma V Mwapachu
  • Hani: A life too short – Janet Smith and Beauregard Tromp
  • Juhudi na Changamoto – Sheikh Ponda Issa Ponda
  • The Bhutto Dynasty: The Struggle for Power in Pakistan – Owen Bennett-Jones
  • Maisha Yangu – Khamis Abdallah Ameir
  • Revolution in Zanzibar: An American’s Cold War Tale – Don Petterson
  • The Tanganyika Way: A personal Story of Tanganyika’s Growth to Independence – Sophia Mustafa
Nchi ya mwaka, India
  • Indian Summer: The Secret History of the End of an Empire – Alex Von Tunzelm
  • Pride, Prejudice and Punditry: The Essential – Shashi Tharoor
  • Mamata Beyond 2021 – Jayanta Ghosal
  • The Rise of The BJP: The Making of the World’s Largest Political Party – Bhupender Yadav and Ila Patnak
  • India in a New Key: Nehru to Modi, 75 years of freedom and democracy – Narain D. Batra
Mchanganyiko
  • Time for Socialism – Thomas Piketty
  • Capturing Hope: The Struggle Continues for a New Malaysia – Mahathir Mohamed
  • Final Reckoning: An Insider’s View of the Fall of Malaysia’s Barisan Nasional Government – Romen Bose
  • The World for Sale: Money, Power and the Traders Who Barter the Earth’s Resources – Javier Blas and Jack Farchy
  • Sudan’s Unfinished Democracy: The Promise and Betrayal of a People Revolution – Willow Berridge, Justin Lynch, Raga Makawi and Alex De Waal
  • From Rebel to Ruler: One Hundred Years of the Chinese Communist Party – Tony Saich
  • Borderland: A Journey Through the History of Ukraine – Anna Reid
Heri ya mwaka mpya 2023

23/12/2022


ILANI: Kila mwaka, nikibahatika na kujaaliwa, huwa ninasafiri pamoja na familia yangu. Kwa muda sasa nchi ninayotembelea huchomoza kupitia vitabu nilivyosoma mwaka huo. Mwaka huu nimeamua kuweka kundi la Nchi ya Mwaka ili kuonyesha vitabu nilivyosoma kuhusu nchi husika. Mwaka 2022 ilikuwa India (Rwanda 2021).
Hongera sana Mwami kwa kusoma na kuweka wazi vitabu ulivyosoma kila mwaka.

Ni utaratibu mzuri na ambao mimi binafsi nimeuiga kutoka kwako na kwa mwaka huu nimesoma vitabu 40
 
Watu mpo depressed Sana
Mnasahau mwenzenu kajitoa na siasa ndo Kazi anayoitegemea kulisha Familiya na kulipa bill zake , nyie mkaa huko mnasubiri zitto awatetee ili Familiya ikose mkate wa kila siku!!
 
Hivi vitabu vimekusaidia vipi kutatua changamoto lukuki zinazowakabili watanzania kwa sasa zikiwemo mfumuko wa bei, hali duni za vipato vya watu, huduma hafifu za jamii zikiwemo maji na umeme na kuongezeka kwa kasi kwa deni la taifa kunakotishia uhimilivu wa uchumi wetu kuweza kulibeba.
 
Zitto ni mzalendo anayeipenda Tanzania zadi kuliko maslahi yake binafsi, tatizo huenda ni njia anazochagua kufikia malengo yake ya kisiasa.
Hata mimi naliamini hilo huwa natamani sana huyu bwana akiishi na kukifanyia kazi kile alichojaaliwa na Mungu watu wanaumia sana ni basi tu.
 
Hana kazi ya kufanya, Kwa nini wana siasa wengi wa Tz ni masikini sana? Jibu ni simple tu wana tegemea siasa siku zote, akitoka hapo hawezi kujiendeleza hata kibiashara, hapo zito mdomo na maneno mengi usikute Hana hata kampuni so Yuko iddle tu.

Wakati ndugu zetu wakenya wana siasa wako na pesa na wana fanya biashara, wame wekeza nchini kwao, hata kama ni pesa ya wizi Bado Ina circulate within, mfano mchukue lipumba vs odinga, odinga hadi ana chopper yake binafsi, Kwa wastani ana mawe na apartment za kutosha.

Angalia hata kina sonko wako mbali na ni watu wa kawaida, most of Kenyans politicians ni business men huo muda wa kusoma taka taka wana zitoa wapi? , Hawa wana siasa wetu ni chanzo Cha umasikini Tanzania.
 
Chadema hakuna mtu wanaemshambulia kama Zitto...kama Wana "hidden reason"...
Lowasa,Sumaye..wote kwao sio wasaliti...Dr Slaa sio msaliti...wao Zitto ndo "msaliti" wao....hata thread inahusu vitabu ...all the can share is hate
 
Badala ya kujadili vitabu watu mmeamua kumshambulia mleta vitabu, It is not fair!
Kwani vitabu vimefanyaje mkuu? maana mleta mada hajavichambua, nadhani lengo kuu la mleta mada ni kujizungumzia yeye kuwa ni msoma vitabu na ndio maana watu wanapita humo humo.
 
Kwani vitabu vimefanyaje mkuu? maana mleta mada hajavichambua, nadhani lengo kuu la mleta mada ni kujizungumzia yeye kuwa ni msoma vitabu na ndio maana watu wanapita humo humo.
Ndio ni msoma vitabu, ili awaelekeze kuhusu vitabu, mjadili vitabu, mlivyosoma na alivyosoma.
Sio kumjadili yeye binafsi au maisha yake ya siasa.
 
Chadema hakuna mtu wanaemshambulia kama Zitto...kama Wana "hidden reason"...
Lowasa,Sumaye..wote kwao sio wasaliti...Dr Slaa sio msaliti...wao Zitto ndo "msaliti" wao....hata thread inahusu vitabu ...all the can share is hate
Nadhani Thread inamuhusu Zitto zaidi kuliko vitabu, ameonyesha kuwa yeye ni msoma vitabu anaeleza vitabu vingapi amesoma na kupewa zawadi ya vitabu basi.
 
Ndio ni msoma vitabu, ili awaelekeze kuhusu vitabu, mjadili vitabu, mlivyosoma na alivyosoma.
Sio kumjadili yeye binafsi au maisha yake ya siasa.
Labda tuseme kwamba mleta mada yeye anasoma vitabu kama hobby tu na ndio maana kaishia kutaja idadi ya vitabu na kuzungumzia kupewa zawadi ya vitabu, ila members humu wao wameenda kwenye upande wa maarifa yanayopatikana kwenye usomaji vitabu na hapo ndio ikawa sababu ya kumjadili Zitto mwenyewe kama msomaji wa vitabu ambaye ni mwanasiasa na ni kiongozi wa chama cha siasa.
 
Back
Top Bottom