Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Zitto: Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema...

Status
Not open for further replies.
Nikikumbuka jinsi Tundu Lissu;
●Alivyopigwa risasi Bungeni
●Alivyonyimwa matibabu na Govt
●Alivyonyimwa mshahara
●Alivyoporwa ubunge
Kwa kweli sasa nimeamini malipo ya ubaya ni hapa hapa duniani.
Ukimtendea ubaya mwenzio nawe utalipwa kwa ubaya.
Na mshahara wa dhambi ni mauti.
 
Zitto

Happening now...



Ikulu.JPG
 
Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema:

Mosi: Afya ya Rais wa nchi ni maslahi ya taifa na inapaswa kutofanyiwa soga. Afya ya Rais inahusika na maslahi ya nchi yetu ndani na nje. Tusiuendee uvumi huu kwa papara. Tuwe watulivu, tuipe nafasi Serikali na mamlaka zake zitupatie taarifa kamili na kwa wakati unaofaa.

Inawezekana kuwa katika hali hii ya sintofahamu baadhi yetu tumefanya mambo yanayotafsirika kuombea mabaya kutokea. Binafsi naomba radhi kwa tafsiri hizo hata kama haikuwa nia wala madhumuni.

Pili: Tuendeleze tunu yetu ya utu, umoja na mshikamano ambazo tumeachiwa na Mwalimu Nyerere ambaye tumetoka kuadhimisha miaka 20 ya kifo chake wiki iliyopita. Tusiruhusu chuki kuteka mijadala yetu. Chuki haiwezi kuwa jawabu la chuki. Utu ndio jawabu sahihi la chuki.

Tatu: Ni busara kwa Serikali kuwaondoa hofu wananchi juu ya uvumi huu maana kutofanya hivyo kunazua taharuki inayoweza kuepukika. Ikiwa kweli Rais wetu amepata dharura ya kiafya kama uvumi unavyosema basi haitakuwa mara ya kwanza kwa hilo kutokea nchini.

Watanzania ni waelewa na wenye mapenzi na wenye utu. Tumeona walivyowaombea marais wao Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete walipopata matatizo ya kiafya wakiwa madarakani. Naamini wataungana na kusimama pamoja kama taifa kumuombea Rais wetu na nchi yetu.

Zitto Kabwe, Mb
Kiongozi wa ACT Wazalendo
Kibingo, Mamlaka ya Mji Mdogo Mwandiga, Kigoma
20/10/2019
Wewe Zitto Kabwe ni mpumbavu na mzandiki mkubwa! Jana ulikuwa unaufurahia huu uvumi. Baada ya kuugundua ukweli unajifanya mtetezi. Tulikuonya na tunakuonya, acha siasa za kipumbavu!
 
Msemaji wa Serikali anapaswa aseme jambo kuhusu hili.

Mbona JK aliumwa ngiri (Waliita tezi dume), akatangaza!

Kama kuna ukweli basi tumuombee.

Tunafahamu kuwa kuna mengi ya haki na yasiyo ya haki aliyoyafanya yaliwaumiza wananchi.Wala tusiombeane mabaya..tuombe yote mawili uzima wa afya na kubadilika kwa kiongozi wetu.

Hakika Mwenyezi ndie mwenyezi kujua
Tena JK alitupia hadi picha akiwa kwenye makorido ya hospitali na tababsamu juu.

Binadamu kuugua ni jambo la kawaida,sasa sijui wengine wanajiona miungu watu hawapaswi kuugua!
 
Hii ndo post ya zitto walipoanza kutoa na kueneza uvumi wao. Yaani kubwa zima halina akili.

Kuna watu wanaudhi sana. Afu unataka serikali itoe uvumi. Wakati wewe ndo ulileta huo uvumi. Wewe ndo unatakiwa kutoa hofu ulizoleta mpuuzi mkubwa.
IMG-20191020-WA0005.jpeg
 
Nimefuatilia uvumi na mjadala mtandaoni kuhusu afya ya Mheshimiwa Rais wetu. Nina matatu ya kusema:

Mosi: Afya ya Rais wa nchi ni maslahi ya taifa na inapaswa kutofanyiwa soga. Afya ya Rais inahusika na maslahi ya nchi yetu ndani na nje. Tusiuendee uvumi huu kwa papara. Tuwe watulivu, tuipe nafasi Serikali na mamlaka zake zitupatie taarifa kamili na kwa wakati unaofaa.

Inawezekana kuwa katika hali hii ya sintofahamu baadhi yetu tumefanya mambo yanayotafsirika kuombea mabaya kutokea. Binafsi naomba radhi kwa tafsiri hizo hata kama haikuwa nia wala madhumuni.

Pili: Tuendeleze tunu yetu ya utu, umoja na mshikamano ambazo tumeachiwa na Mwalimu Nyerere ambaye tumetoka kuadhimisha miaka 20 ya kifo chake wiki iliyopita. Tusiruhusu chuki kuteka mijadala yetu. Chuki haiwezi kuwa jawabu la chuki. Utu ndio jawabu sahihi la chuki.

Tatu: Ni busara kwa Serikali kuwaondoa hofu wananchi juu ya uvumi huu maana kutofanya hivyo kunazua taharuki inayoweza kuepukika. Ikiwa kweli Rais wetu amepata dharura ya kiafya kama uvumi unavyosema basi haitakuwa mara ya kwanza kwa hilo kutokea nchini.

Watanzania ni waelewa na wenye mapenzi na wenye utu. Tumeona walivyowaombea marais wao Benjamin Mkapa na Jakaya Kikwete walipopata matatizo ya kiafya wakiwa madarakani. Naamini wataungana na kusimama pamoja kama taifa kumuombea Rais wetu na nchi yetu.

Zitto Kabwe, Mb
Kiongozi wa ACT Wazalendo
Kibingo, Mamlaka ya Mji Mdogo Mwandiga, Kigoma
20/10/2019
Sasa ndio umeshajishtukia, Magufuli hafi ataishi,nguvu za giza zimeshindwa kwa jina la Yesu
 
Hakuna mwenye mamlaka juu ya afya na uhai wake. Mwenyezi Mungu pekee ndiye anayetupa vyote hivyo. Hivyo hatupaswi kujivunia juu ya afya zetu au uhai wetu, wala hatupaswi kufurahia wenzetu afya zao zinapopata matatizo hata kama tutakuwa na tofauti kimitazamo/kifikra!

Nimesikitika kwa baadhi ya watu wanaoshabikia kuhusu tetesi juu ya afya ya rais wetu!
Achilia mbali upendo tunaohubiriwa kwenye dini zetu, kuna ile hali ya ubinadamu ambayo ni natural hiyo nayo wanaikosa?

Wengine wanadhani kupata matatizo ya kiafya ni adhabu kwa sababu wanazozijua wao. Je wewe au kwenye familia yako au ukoo wenu hakuna mwenye tatizo la kiafya? Kama wapo unadhani ni kwa sababu wamefanya machukizo kama unavyofikiria kwa mwenzio kwa hiyo wanaadhibiwa? Kuna wengine kiafya hatuko wazima na wengine tumepoteza wapendwa wetu. Je na sisi tunaadhibiwa au wapendwa wetu waliotutangulia ni kwa sababu walikuwa wakosaji sana?

Nimesikitika sana kwa response ya baadhi yetu baada kuwepo kwa taarifa za uvumi juu ya tetesi za afya ya rais wetu!

Kibusara kabisa hata kama mtu mna tofauti naye kwenye suala kama hili ni vema ukawa kimya kama utashindwa kutoa pole au kufanya dua yako kwa kumoumbea nafuu! Hakuna anayeijua kesho yake hasa kiafya na uzima, Mungu pekee ajua! Wala afya zetu zisitufanye tukajivuna sana dhidi ya wale wanaopitia changamoto za kiafya!

Mungu ni wetu sote! Tuishini kwa upendo na wala ubaya haushindwi kwa ubaya bali kwa wema!

Mungu amtie nguvu rais wetu na ampe wepesi kwa matatizo yanayomkabili juu ya afya yake na uongozi wa nchi yetu!

Mungu ibariki Tanzania
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom