Zitto: Serikali ya awamu ya Tano yatia fora kutofikia malengo ya Bajeti

Punguzeni ujuaji,tunakopelekwa ni kubaya zaidi
 
Duniani kote hakuna serikali ya mtu mmoja, kwamba yeye ndiye kila kitu.

Hata wafalme huwa wanaweka waziri mkuu mwenye uwezo wa kuisimamia serikali.

Hapa Mzilankende ndiye waziri wa wizara zote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesoma kila comment naona hakuna inayomtuhumu Dokta Mipango wa Mipango.
 
Jana niliwambia watu hiki kitu kuwa huyu jamaa anatumia taaluma yake mata nyingi kuingiza ujanja ujanja na anajua Watanzania wengi uwezo wao wa kutambua mambo mdogo. Anachofanya anaonyesha makadirio, Makusanyo na nakishi kwa JPM halafu kwa JK ambaye ndo anamtumia Kama kipimo haonyeshi Makadirio, wala Makusanyo Kama ulivofanya hapo juu, bali anaonyesha nakishi tu, na hapo ni makusudi ili kuipa nguvu hoja yake ya uongo kwa kwakuwa Mambumbu wengi basi wanaona kaandika ukweli.
Kwamba alijipangia kukusanya tsh.1000,000/= akafanikiwa kukusanya tsh.950,000/=amefanikiwa sana katika Makusanyo kuliko aliyejipangia kukusanya Tsh.10,000,000/= na akafanikiwa kukusanya Tsh.7000,000/=kwa kutumia vyanzo vile vile. Kama Hawa ndo wachumi wetu naanza kuona mantiki ya Jalala.
 
Hapa Zitto hashangilii,anajaribu kuonyesha masikitiko makubwa juu ya Jambo hili,Wapi Zitto kashangilia?
 
Itakwenda hadi pesa itaisha.

Uchumi wa Dunia ndio ushaharibika, hii ina maana kwamba uwezo wetu wa kupata US Dollar utakuwa mdogo, US Dollar inahitajika kuwalipa Wakandarasi wa hii miradi mikubwa.
Lakini hamna mradi hata mmoja uliokwama kwa kukosa pesa, ndiyo kwanza mandege , Sgr yananunuliwa kwa keshi

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Nchi huwa haijengwi na mawazo ya mtu mmoja.Ujuaji wa Nyerere kutokushaurika sababu ya ujuaji kujua kila kitu akafail kwenye uchumi.
 

Mbio za sakafuni sawa na nguvu ya soda.
 
L7 huwezi wapata uzi kama hizi pumzi imekata wamesafisha Sana mikojo wamechoka, huwezi pambana na reality.
 
Huna vyanzo vya kukusanya mapato,utafikiaje malengo ya kukusanya mapato mengi ?Vitu vingine hauhitaji uwe na degree ya uchumi kuvifahamu.
Kusomeshwa watu namba ni kujijichimbia kaburi.
Alidhani akisomesha watu namba atabaki salama,
Kanuni ya namba ukimaliza kuwasomesha watu namba ni lzm uisome namba.Huwezi komoa watu wakuleteao Kodi eti wawe masikini hapo ni sawa na kuzuia mito ikuleteayo maji ziwani lzm ziwa litakauka ndo kilichopo Sasa uwezo wa kupandisha mishahara hawana wamesingizia kwenye uhakiki usioisha
 
Leo ndio mnataka ushauri baada ya kulikoroga ni Mara ngapi imeonywa madhara ya maamuzi Fulani yasifanyike yataleta madhara haya na haya,pamba zikiwekwa masikioni huku wengi wakitupwa jela,pigwa risasi,nk leo mambo yameharibika.Acha jahazi lizame ili mvune ujuaji wenu.
 
Utamshauri vipi mtu mjuaji ajuaye kila kitu Hali ni mweupe nje ya asivovijua.Taifa bila mashauri ni lzm litaangamia,panapo mashauri uja uponyaji.
Uliambiwa usifanye hivi utauwa secta binafsi, usifanye hivi wafanyabiashara watakimbia nk lkn kila mtu unamuona ni mpiga dili sijui wakulima,wavuvi walipiga dili gani.Masikini walishangilia Sana matajiri wakishughulikiwa leo masikini ndio wamelimia meno wanapumulia mashine dhoofu Hali hata kula tu shida matajiri wamewekeza nje nenda beira Mozambique ukaone truck za tz zinaplate no za Congo,Zambia,Malawi,nk zikipiga kazi kama kawaida ajira ngapi za watz zimekufa.Tajiri ni mtu mwenye exposure hawezi soma namba au ishi kishetani zaidi utauwa watu wako tu kwa njaa.Haya mambo ya uongozi yatakiwa mtu ambae ana asili ya utajiri au biashara by nature.
 
Huna vyanzo vya kukusanya mapato,utafikiaje malengo ya kukusanya mapato mengi ?Vitu vingine hauhitaji uwe na degree ya uchumi kuvifahamu.


Badala ya kuisha kulaumu na kubeza Vitajeni hivyo vyanzo ili wahusika wavichukue na kuvifanyia kazi ili kuona kama vitaweza kuzaa matunda (makusanyo ya kodi).

“Kwa pamoja tujenge Taifa letu”


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chapa kazi tulisha ambiwa nchi yetu ni donar county, pesa ipo na tunavunja records za mapato.

Nani mkweli CAG au Mkulu wetu, mm kichwa kinauma na hichi kikorona nachapa kazi tu
 
Nimesoma kila comment naona hakuna inayomtuhumu Dokta Mipango wa Mipango.


Ninachompendea Mpango ni vile alivyo mtu mwenye kujaa subira wakati wote!

He is humble and firmly!

Si mwepesi wa hasira,

Si mtu wa jazba na visasi wala visilani!

Angalia akiwa bungeni anavyopewa makavu mubashara na kina John Heche lakini amejaa subra !

Actually Heche huwa anakuwa na hoja za msingi siku zote!


Mtu kama Mpango huwezi kuacha kumstiri.

Natamani wengi wajifunze kutoka kwa Bwana Mpango.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Serikali hii sio rafiki na wafanyabiashara.

Mfano, Serikali imekuwa wafanyabiashara wao wenyewe kwa kuanza kufuta mashirika binafsi ya Mawakala wa meli (shipping agent) na kufanya wao kazi za uwakala wa meli.

Nasema imeamua kuyafuta indirect, serikali inapotunga sheria kuwa kazi zote za shipping agent, atafanya yeye kasoro Meli za Container, maana yake yale makampuni yaliokuwa yanafanya kazi ambazo sio meli za container hawatakuwa na kazi na automatically watafunga biashara zao.

Ni kodi zao kiasi gani itapotea?
Wafanyakazi wangapi wanarudi mtaani?

Katika dunia ya sasa ambayo bandari jirani wanaweka ushindani zaidi, sisi tunaondoa ushindani kwa kuwanyima wenye meli kuwa na uamuzi wa kumtumia wakala wanayemtaka, huku tozo za kodi zikiwa juu, tutegemee mzigo unaoshushwa Dar kupungua kwa kiasi kikubwa, hasa transit cargo na kuhamia Mombasa na beira.

Kupanga ni kuchagua, huwezi ukawa adui wa wafanyabiashara, vilio ni vingi sana, wakati mwingine Mungu hawezi akaruhusu serikali kufanikiwa, anaposikia vilio vya watu wanaoumizwa kutoka kila kona.

TASAC (wakala wa meli wa serikali)
1) Yeye ni regulator kwa makampuni yote ya shipping agent (sijui anaji regulate vipi yeye mwenyewe maana na yeye pia ni wakala na ni regulator)

2) Yeye ni Wakala wa Meli (shipping agent) kwa sheria inayompa kufanya kazi almost zote kasoro container

3) Yeye ameweka sheria kuwa ni lazima afanye Tallying, mzigo wowote unaoshuka yeye anatoa huduma ya Tallying KWA LAZIMA, na ameweka rate kubwa mno, mwenye mzigo hana uchaguzi kuwa afanye tally au laa kama mwanzo. Mfano, mzigo wa ngano ton elfu 40, saivi wanalipa dola 18,000 ambayo kabla walikuwa hawalipi. Halafu wanaulizwa how do they tally ngano, hawana majibu. Huu ni wizi na kupandisha bei ya bidhaa bila sababu ya msingi.

4) Yeye ameweka sheria lazima afanye clearing and forwarding ya aina ya mizigo almost more than 50% inayoshuka, hizi kampuni za clearing zitafanya kazi gani?

5) Tasac huyohuyo anakusanya 1.3% ya mapato yote ya kampuni binafsi za shipping agent kabla ya matumizi yao.

6) Tasac huyohuyo anakusanya kodi ya mzigo kutokana na mahali ulipakiwa.

Yaani kila kitu sasa bandarini ni Tasac, Tasac, Tasac., mzigo.mmoja, Tasac anatozo lukuki

Tunasubiri anguko la uchumi kwa maamuzi haya mabaya waliofanya ktk sekta ya bandari, na watakapotaka kurudi, itakuwa too late



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…