Zitto: Ushauri wangu kuhusu Mlipuko wa Korona

Zitto: Ushauri wangu kuhusu Mlipuko wa Korona

Leo nilienda Mlimani City kwa shughuli zangu binafsi, niliyoyaona yamenisikitisha sana. Watu wamejawa na ulimbukeni wa ajabu, wanavaa zile mask kama fashion huku wakiwa hawazingatii tahadhari nyingine.

Mentality ya watu wengi ni kwamba corona itakuja na kupita ndani ya siku/wiki chache. Niliwahi kusema humu kwamba endapo corona ikilipuka hapa kwetu na ikaathiri watu na kuua kama kule China ama Italy, hali itakua mbaya sana!!

Najaribu kuangalia watu wanaofanya maigizo sasa hivi ya kujidai kuvaa mask, najiuliza hivi corona iki persist angalau kwa miezi sita tu, je watakua na hela za kununua mask mpya kila siku? Kwanza hata hela ya kula watakua nayo? Na hizo mask zitakuepo? Ikiwa sasa hivi tu ugonjwa haujasambaa tayari mask zimeadimika? Hizo mask watu wanazochezea watakuja kuzikumbuka.

China wamepambana na corona tangu november mpaka sasa na bado hawajaimaliza, sisi tunacheza cheza hapa na ujinga ujinga mwingi we ngoja tu.
 
Haya ndiyo maneno, hizi ndizo hoja tunahitaji wana CCM, siyo mipasho wa wakatikia kuni akina Lema na Mbowe.

Nadhani Mmawia na genge la wahuni wenzako akina Nyonyoma mnaelewa sasa maana ya hoja, mwezenu kaleta maoni yaliyojaa hoja na serikali lazima itie jicho hapa.
Hoja msigwa sio zitto. Kachelewa kujua
 
Zitto,
Mara nyingi nimekuwa nikiiona michango ya Zitto ni ya kiupinzani tu kulaumu serikali kwa madhumuni ya kulaumu tu kwa kuwa yuko upinzani. Bandiko lake la leo ni tofauti. Anachambua suala na kutoa mapendekezo tufanyeje.

Hata kama mtu hukubaliani na mapendekezo yake, yeye ametoa mawazo yake bila kuegemeza kwenye uchama. Kwa hiyo yapinge kwa kutoa hoja kwa nini isiwe vile anavyopendekeza. Hivi ndivyo upinzani halali unapaswa kufanya.

Vyama vyote vya siasa vikiwa vinafanya hivi ukumbi wa kisiasa nchini utabadilika kabisa na hakutakuwa na malumbano yasiyo na tija tunayoyashuhudia hivi sasa.
 
Serikali itazame namna ya kuwafidia (stimulus package) wafanyabiashara Katika sekta hiyo ili kulinda ajira za Wananchi. Ikiwezekana fidia iwe ni kulinda ajira kwa kufidia gharama za wafanyakazi ( payroll costs).
Zitto hizo stimulus package zitasababisha shilingi yetu kushuka sana thamani kwani zitailazimu serikali kuflood mtaani pesa kupitia Quantitative Easing
 
Bill Gates has warned that coronavirus in Africa could overwhelm health services and trigger a pandemic which could cause 10 million deaths.
Utabiri wa BG wa vifo mlioni kumi Africa ni wastani wa vifo laki mbili kila nchi afrika. Wapiga kura sio haba.
 
Trump ametangaza dola 1000 kila familia Marekani leo na zile zenye watu wengi wataongezewa dola 500.
Hao ndio wanajua thamani ya mwananchi.

inaonekana wewe hata hujui umuhimu wako wala majukumu yako katika nchi yako.
Pathetic
unafananisha Marekani na Tanzania, ? Tanzania uwezo huo haupo sisi bado ni masikini.
 
Makampuni ya utalii na Hotels nyingi sana Arusha zimewapa wafanyakazi wao likizo isiyo na malipo kutokana na mlipuko wa Corona...swali langu ni kwamba Je ni sawa kuwafukuza wafanyakazi kwa njia hii?..naomba serikali iingilie kati kwani tutakufa kwa njaa.
 
Makampuni ya utalii na Hotels nyingi sana Arusha zimewapa wafanyakazi wao likizo isiyo na malipo kutokana na mlipuko wa Corona...swali langu ni kwamba Je ni sawa kuwafukuza wafanyakazi kwa njia hii?..naomba serikali iingilie kati kwani tutakufa kwa njaa.
Kufa kwa nja na kufa kwa corona kipi ni bora?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Makampuni ya utalii na Hotels nyingi sana Arusha zimewapa wafanyakazi wao likizo isiyo na malipo kutokana na mlipuko wa Corona...swali langu ni kwamba Je ni sawa kuwafukuza wafanyakazi kwa njia hii?..naomba serikali iingilie kati kwani tutakufa kwa njaa.
Rudi kwenye mkataba wako, tazama kama mkataba umeahinisha wafanyakazi kupewa likizo isiyo ya malipo ikiwa patatokea ugonjwa wa mlipuko.

Kama hakuna kiengele/makubaliano hayo, basi muajiri anapaswa akulipe kwasababu yeye ndie ameamua kukupa likizo. Na ikiwa muajiri atakaidi, basi unapaswa umuwajibishe kwa kumchukulia hatua za kisheria.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rudi kwenye mkataba wako, tazama kama mkataba umeahinisha wafanyakazi kupewa likizo isiyo ya malipo ikiwa patatokea ugonjwa wa mlipuko.
Kama hakuna kiengele/makubaliano hayo, basi muajiri anapaswa akulipe kwasababu yeye ndie ameamua kukupa likizo. Na ikiwa muajiri atakaidi, basi unapaswa umuwajibishe kwa kumchukulia hatua za kisheria.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapo inabidi na utu utumike pia aisee[emoji848]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom