Zombe aachiwa huru, Mshirika wake ahukumiwa kunyongwa hadi kufa

Zombe aachiwa huru, Mshirika wake ahukumiwa kunyongwa hadi kufa

Pole Sana kwa aliyehukumiwa kunyongwa lakini haya ndiyo matunda ya kufanya kazi kwa kutaka kuwafurahisha baadhi ya watu ambao baadaye mambo yanapokuwa magumu wanakuruka.
Umenena vyema ila hawazingatii matokeo kama haya
 
Sasa nasikia harufu mbaya, Baba Lowassa kuwa makini, hawa watu wameanza kufufua wafu na kuwahukumu wapendavyo!
 
Pole Sana kwa aliyehukumiwa kunyongwa lakini haya ndiyo matunda ya kufanya kazi kwa kutaka kuwafurahisha baadhi ya watu ambao baadaye mambo yanapokuwa magumu wanakuruka.
Ndo maana tunaelezwa kuwa akili za kuambiwa changanya na zako...
Hata yule askari aliyemuua mwangosi ni hivyo hivyo, bosi wake aliyemuamrisha karuka viunzi yeye kanaswa....
 
Mahakama ya Rufaa imemhukumu aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Wilaya ya Kinondoni, Christopher Bageni kunyongwa hadi kufa katika kesi ya vifo vya wafanyabiashara wa madini iliyokuwa ikimkabili yeye pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Dar es Salaam (RCO) Kamishna Msaidizi wa Polisi Abdallah Zombe na maofisa wenzake wawili.

Katika hukumu hiyo, Zombe na maafisa wengine wawili wameachiwa baada ya kushinda rufani hiyo dhidi yao.

Hukumu hiyo imehitimisha mvutano wa muda mrefu wa kisheria kati ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) na maofisa hao kwani baada ya kimya kirefu hukumu hiyo imetolewa.

Watuhumiwa wengine katika kesi hiyo walikuwa ni, aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Kituo cha Polisi Urafiki, Mratibu Msaidizi wa Polisi (ASP) Ahmed Makelle na Rajabu Bakari.

Hukumu hiyo imekuwa ikisubiriwa kwa muda mrefu, wakiwamo ndugu wa marehemu hao, wanasheria na jamii kwa jumla baada ya miezi minne, majuma mawili na siku mbili, tangu rufaa iliposikilizwa.

DPP alikata rufaa akipinga hukumu ya Mahakama Kuu iliyowaachia huru Zombe na wenzake wanane katika kesi ya mauaji ya wafanyabiashara wawili wa madini kutoka Mahenge, Morogoro na dereva wa teksi, mkazi wa Dar es Salaam.

Katika kesi ya msingi, Zombe na wenzake walidaiwa kuwaua kwa kukusudia wafanyabiashara Sabinus Chigumbi, maarufu Jongo na ndugu yake, Ephrahim Chigumbi, Mathias Lunkombe na Juma Ndugu, aliyekuwa dereva wa teksi wa Manzese.

Walidaiwa kutenda makosa hayo Januari 14, mwaka 2006, katika msitu wa Pande, uliopo wilayani Kinondoni baada ya kuwakamata wafanyabiashara hao Sinza, walipokuja Dar es Salaam kuuza madini.

Agosti 17, 2009, Mahakama Kuu iliwaachia huru washtakiwa hao ikisema baada ya kusikiliza ushahidi na hoja za mawakili wa pande zote iliridhika kuwa hawakuwa na hatia ya mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili.

Badala ya kosa la mauaji ambalo adhabu yake ni kunyongwa hadi kufaa, DPP aliiomba Mahakama imtie hatiani Zombe kwa kosa la kuwalinda wahalifu, ambao adhabu yake ni kifungo kisichozidi miaka saba jela.

Wakili wa Serikali Mkuu (PSA), Timon Vitalis alidai DPP alifikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa hakuna ushahidi wa kumtia hatiani Zombe kwa kosa la mauaji.


Chanzo: HiviSasa Blog

Mleta mada tupu basi na hukumu hapa. Maji walikuwa nani
 
Kilichomsaidia Zombe ni kukubali kufuta kesi ya kudai fidia kutokana na hukumu ya awali. State made a deal with him wakampa option moja kati ya mbili kabla hukumu ya rufaa haijatoka. Either rufaa imkute na hatia aende jela or akubali kudrop off madai ya fidia yale ya billions dhidi ya state.... You don't need a degree kuona kuwa alikuwa na hatia kabisa.


Nimewaza tu

This is a serious allegation, kama huna uhakika ifute. Ni insult kubwa kwa judiciary. Meaning kwamba haki haikutendtka na aliyehukumiwa kunyongwa ni maonevu.
 
I cant imagine ni mawazo ya kiasi gani yanapita kwenye kichwa cha SP Bageni muda huu
Du, Bageni kijana mdogo aliyekuwa anainukia.
Inaelekea waliompa amri wamemruka.
Lakini kwa yale mauaji yaliyotikisa nchi haki lazima itendeke, damu ya wananchi imemlilia Mungu.
 
  • Thanks
Reactions: MC7
Na ile kauli ya kuwalaza chini wawe makini nayo, manake wanaweza kuitumia kuonea na mwisho wa Siku wanabaki peke yao mahakamani
 
This is a serious allegation, kama huna uhakika ifute. Ni insult kubwa kwa judiciary. Meaning kwamba haki haikutendtka na aliyehukumiwa kunyongwa ni maonevu.
Ni watu wangapi hawakutendewa haki na judiciary (courts of law) katika taifa hili masikini!!!! Ni wangapi wamefungwa kwa hila na kukosa uwezo wa kiuchumi!!! Nenda mahabusu/jela kafanye utafiti then leta mrejesho.


Nawaza....
 
"Mahakama ni sehemu sahihi ya kupata haki ila kuna muda sheria hukosa jicho la tatu kuuona ukweli"
 
Ni watu wangapi hawakutendewa haki na judiciary (courts of law) katika taifa hili masikini!!!! Ni wangapi wamefungwa kwa hila na kukosa uwezo wa kiuchumi!!! Nenda mahabusu/jela kafanye utafiti then leta mrejesho.


Nawaza....

Nakubaliana na contention yako. Lkn for Zombe case you can not say for sure kuwa haki haikutendeka kuwa alipewa options mbili na mahakama ikaangukia kwenye options hizo.
 
Polisi wakifanyiwa hivi kila mara watatuheshimu Wananchi
 
Back
Top Bottom