Habari wakuu,
Nimeona taarifa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki imetambulisha noti yake itakayotumika katika nchi wanachama, iliyopewa jina la SHEAFRA (SHF). Wengi wameinukuu akaunti kutoka mtandao wa X (zamani Twitter) inayojulikana Government of East Africa
Moja ya chombo kikubwa kilichoinukuu akaunti hiyo ni pamoja na ITV , binafsi bado nina mashaka na hii taarifa kutokana na kwamba akaunti maalum ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ninayoifahamu siyo hii.
Ukweli ni upi?