Habari wakuu, nimeshangaa sana kuona WASAFI TV ikitumia lugha ya kihuni tena yenye maudhi katika uwasilishaji wa taarifa.
Chombo mahili hakiwezi kutumia neno 'usela mavi' katika kufikisha ujumbe wake kwa hadhira,binafsi siyo mtaalamu wa teknolojia labda nyie wajuvi wa mambo hayo tazameni hii video chini kisha mniambie kama ni editing au laa.
Kama ni Wasafi kweli lazima tujiulize maswali yafuatayo:
Je hii jeuri wanaipata wapi ya kutudhihaki sisi juu ya msiba mkubwa kama huo?
Je wao wanatumika katika kuchochea maovu ya utekaji au wao wanajikuta akina nani labda na chombo chao?
Je wamezingatia nini katika uwasilishaji wao wa hiyo habari na je wameelewa kweli nini maana ya kupinga na kupaza sauti kwa vitendo juu ya mauaji?
Pia soma...