1894 Loniel Walter Rothschild akivinjari London na punda milia

1894 Loniel Walter Rothschild akivinjari London na punda milia

Yeah! But they don’t own 95% of the World’s net wealthy which in 2018 was estimated to be $317 trillions while the total net worth of this family in the same year was estimated to be $400 billions.
Hawa wana wataalamu wao wa madini, wanafanya tafiti na kufadhili ucimbaji wa madini, mafuta na gesi dunia nzima.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Hivi hata swala hana urafiki na binadamu!? Tunashindwaje kumfuga aisee!?
Kiasi wanyama wote walikuwa porini nasi wanadamu ndio tukaanza wafuga. Hivyo mwanadamu kwa miaka mingi amekuwa akifanya juhudi za kujaribu kuwafuga wanyama kadhaa, wapo waliofanikiwa na wapo alioshindwa kabisa. Hawa wanyama tunaowafuga leo [Farasi, Mbuzi, Ng'ombe, Kondoo na Nguruwe] walikuwa ni wanyama pori waliokuwa wakipatikana eneo la ulaya na asia, huku kwetu waliletwa in the course of human interaction.

Katika wanyama wote ambao wanadamu tumefanikiwa kuwafuga, ni wamekuwa na sifa zifuatazo [ikikosekana hata moja, ilimfanya mnyama huyo iwe ngumu kumfuga]

1. Chakula. Wanyama walao nyama ni ngumu sana kuwafuga. Mf Simba ana kula wastani wa kilo 6 kwa siku. Sasa imagine awe na watoto wake. Unatumia karibu ef 60,000 kwa siku kumlisha. Herbivorous ndio hasa wanaofugwa.

2. Kasi ya ukuaji. Wanyama wanaokuwa haraka ndio wamefugwa. Mf Tembo anahitaji miaka 15 ndio awe amekuwa, sasa hii ni hasara.

3. Namna ya uzalianaji. Wanyama wenye uwezo wa kujamiiana wakiwa wamefungwa ndio ambao wamefugika. Mf Duma hawezi kujamiiana akiwa amefungiwa sehemu mbele ya wanadamu. Pia mchakato wake wa kumpata jike, kukubaliwa na kurutibishwa yai huchukua siku kadhaa. Kinyume na wanyama kama ng'ombe au mbuzi.

4. Madhala kwa wanadamu. Mnyama anayeweza mdhuru mwanadamu, huyu imeshindikana kumfuga. Mfano Zebra ana tabia ya kung'ata na hatabiriki.

5. Hulka ya kupanick. Wapo wanyama ambao hawana hulka ya kupanick sana kwenye hatari na huhitaji binadamu mara nyingi ndio awanusuru. Mf Mbuzi, ndio maana Chatu huwala mbuzi kirahisi bandani.

Wengine wana hulka ya Kupanick na kuruka na kukimbia kwa haraka wanapokuwa hatarini. Mf Swala. Swala akisense hatari anaruka karibu futi 10 juu. Maana yake kwenye banda ni rahisi kujiumiza. Lakini pia akiwa anakimbia speed ambayo mwanadamu ni kazi sana kummudu. Mruko wa suala ni hadi futi 33. Hivyo suala ni ngumu sana kumdhibiti. Huna hakika kama nikianza mfuga leo, siku kadhaa mbele nitakuwa naye, sasa huwezi fanya investment isiyo na hakika.
 
Huyo mzungu kawafanya nini hao Pundamilia??, mbona yupo nao wakifanya kazi ya Farasi na punda???.

Mkuu ni mazoea tu, kufuga pundamilia ni sawa na kufuga Kanga au Tausi kwani hawa wote ni ndege waliozoea kuishi porini, kimsingi wanyama wote asili yao ni porini mfano kuna nchi Mbuzi, ng'ombe, kuku na ngamia wanaishi porini na wame behave kama viumbe pori, ni hivi; huwezi kumfuga Pundamilia awe sawa na Farasi au Punda jinsi Punda hayupo sawa na Farasi au kuku asivyokuwa sawa na kanga au kondoo asivyokuwa sawa na mbuzi lakini wote hao wanafugika licha ya tabia na sifa zao kutofautiana na ni hivyo hivyo pundamilia au nyati (the cape Buffalo) anaweza kufugika akiwa na sifa zake peculiar.
Alichofanya Rothschild ni sehemu ya attempt ya wanadamu sehemu zote duniani kujaribu kumfuga huyu mnyama, lakini tumeshindwa.

Na wala sio mazoea, kuna sababu zimewafanya watu waone ni waste of time na kuweka maisha hatarini kumfuga zebra.

Waliojaribu kumtumia zebra kama Farasi imekuwa ngumu kwa sababu, moja Zebra anang'ata vibaya na hakuachi, kuna tafiti wafugaji Huko america wamejeruhiwa zaidi na Zebra waliojaribu kuwafuga kuliko Chui, pili Zebra hadi sasa hajafanikiwa kuzoea kamba kupita mbele yake anapotaka kufungwa amekuwa akimiisbehave na kujeruhi. Cha tatu, Zebra amekuwa na tabia zisizotabirika. Leo anaweza kuwa friendly kesho akawa hostile. Ndio maana imekuwa ngumu sana.

Wanachokufanya mara nyingi huwa ni kumTAME. Kama ambavyo wanafanya kwa tembo.
 
Zebra hafugiki mkuu. Ni ngumu kumfuga kwa sababu hana urafiki na mwanadamu na hatabiriki, tofauti na 'ndugu yake' farasi. Na hii ndio sababu kwa nini Afrika licha ya kuwa na mnyama huyu maelfu ya miaka iliyopita, hawakuweza kumtumia kwa faida kama Farasi wakivyomtumia watu wa Middle East na ulaya.
'wakivyomtumia'

Kama si mmakonde lazima utakuwa ,mmwera wewe
 
kabisa ni majarity share holders wa benki kuu za mataifa yote duniani isipokuwa Cuba na Korea ya Kaskazini
Pia ni share holders kwenye machimbo mengi ya madini.
 
Wanachokufanya mara nyingi huwa ni kumTAME. Kama ambavyo wanafanya kwa tembo.


Kwani Tembo anatabirika??---- ninachosema ndicho hicho unachoniunga mkono kwamba Zebra anaweza kuwa Tamed/demosticated na hawezi kuwa kama Farasi au punda na hata Farasi sio sawa na Punda katika behaviour zao, kuna wakati Farasi anaweza kumpiga teke Bwana wake au akakimbia hovyo (run amok) na inakuwa mshikemshike na punda ni hivyohivyo naye anaweza kugoma kufanya kazi na kuanza kurusha mateke, sasa usitake kumfanya Zebra awe exactly sawa na Farasi au Punda kitu ambacho hakiwezekani hiyo ni sawa na kum- tame cape Buffalo na awe exactly kama Ng'ombe kitu ambacho haiwezekani.

Kifupi ni kwamba Zebra anaweza kuwa tamed ila anazo tabia zake (genetical inherent behaviors) hizo hazibadiliki.

Kwanini Zebra hapendwi ??, jibu ni kwamba mbadala wake ni Farasi na Punda ndio maana watu hawajishughulishi naye isitoshe hiyo sehemu kubwa duniani hasa Africa wanapotoka Zebra ni nyara ya serikali.
 
Kwani Tembo anatabirika??---- ninachosema ndicho hicho unachoniunga mkono kwamba Zebra anaweza kuwa Tamed/demosticated na hawezi kuwa kama Farasi au punda na hata Farasi sio sawa na Punda katika behaviour zao, kuna wakati Farasi anaweza kumpiga teke Bwana wake au akakimbia hovyo (run amok) na inakuwa mshikemshike na punda ni hivyohivyo naye anaweza kugoma kufanya kazi na kuanza kurusha mateke, sasa usitake kumfanya Zebra awe exactly sawa na Farasi au Punda kitu ambacho hakiwezekani hiyo ni sawa na kum- tame cape Buffalo na awe exactly kama Ng'ombe kitu ambacho haiwezekani.

Kifupi ni kwamba Zebra anaweza kuwa tamed ila anazo tabia zake (genetical inherent behaviors) hizo hazibadiliki.

Kwanini Zebra hapendwi ??, jibu ni kwamba mbadala wake ni Farasi na Punda ndio maana watu hawajishughulishi naye isitoshe hiyo sehemu kubwa duniani hasa Africa wanapotoka Zebra ni nyara ya serikali.
Nadhani unajua kuna tofauti ya taming and domesticating!
 
Nadhani unajua kuna tofauti ya taming and domesticating!


Ku tame ni kumfanya azoee watu na ku domesticate ni kumfanya aweze kuishi katika mazingira ya binadamu kama mbuzi anavyoishi na binadamu., tunachozungumzia ni kum- tame na kumfanya domestic.
 
Ku tame ni kumfanya azoee watu na ku domesticate ni kumfanya aweze kuishi katika mazingira ya binadamu kama mbuzi anavyoishi na binadamu., tunachozungumzia ni kum- tame na kumfanya domestic.
Na ilivyo, Zebra hajafanikiwa kuwa domesticated [kwa maana ya permanent] ila anakuwa tamed [ambayo ni temporary]
 
Mabenk yote mkubwa originated from them, railway kubwa ni initiative zao makampuni kama coca cola n Pepsi wali anzisha na wanae joy loyarities mpka kesho kutwa so far wana miliki 1/3 ya uchumi wa Dunia.
Lakini 1/3 ni asilimia thelathini na tatu (33%)
 
Na ilivyo, Zebra hajafanikiwa kuwa domesticated [kwa maana ya permanent] ila anakuwa tamed [ambayo ni temporary]


Sio kweli, watu wanafuga (domesticate) Tembo, Chui, Cape Buffalo, Simba, Fisi nk, sembuse Zebra ambaye ni jamii ya Farasi, Mule na Punda??.

Huyo ni nyara ya serikali hiyo ndiyo sababu kubwa watu hawajishugulishi naye isitoshe Punda na Farasi na ng'ombe ni wengi na wanatosheleza mahitaji ya drafting, (draft animals).
 
Back
Top Bottom