2002 FIFA WORLD CUP: Taifa kubwa la Tanzania na rafiki yake wa karibu Uganda wakiunganisha nguvu zao wanaweza kuandaa mashindano ya AFCON 2027/2029?

Mkuu na uwanja wa Ally Hassan Mwinyi wa Tabora una ngazi zinazozunguka uwanja wote.
 
Idea nzuri sana hii
 
Umesema kweli
 
Hii miji tukiwa na utashi tunajenga viwanja vya kisasa.Viwanja vilivyopo vinakosa vigezo vya kuwashawishi viongozi wenye kuidhinisha mashindano kufanyika kwa kutumia aina ya viwanja vya Mwanza,Arusha na Dodoma.
 
Ikiwezekana iwe Tanzania, Kenya na Uganda.
Absolutely! Inawezekana kwa uzuri tu hata 2024. Ukiangalia World Cup 2026 ni Kanada, Marekani na Mexico though Gianni Infartino alifanya uongo na dhulma tofauti na aliyoyasema wakati akiomba kura, by the way!

Tanzania, Kenya na Uganda ziungane kuandaa AFCON ijayo kila taifa liteuwe miji minne viwanja vinne kuweza kunufaika.
 
Tunapotenga tenga gharama za ukarabati sisi (mimi, wewe na viongozi wetu) kama serikali tunajumuisha gharama za upanuzi wa maeneo. Refer barabara, bomba la gesi la na mafuta na viwanja vya ndege.

Tukitenga billioni 100 tunaweza kukarabati kiwanja kila mkoa na kuwa na hadhi ya kimataifa na kimchezo kwa kugawa billioni 3 huku tukiziomba halmashauri kuchangia asilimia 15 ya mapato yake katika utekelezaji huo.

Faida ni nyingi sana baada ya maboresho haya kufanyika.
 
Hii miji tukiwa na utashi tunajenga viwanja vya kisasa.Viwanja vilivyopo vinakosa vigezo vya kuwashawishi viongozi wenye kuidhinisha mashindano kufanyika kwa kutumia aina ya viwanja vya Mwanza,Arusha na Dodoma.
Ndio maana nikasema kunahitajika uboreshaji mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…