A - Town Gangsters walioitikisa Arusha kwa matukio ya uhalifu

A - Town Gangsters walioitikisa Arusha kwa matukio ya uhalifu

Hahaha, umenikumbusha mbali, Mtoto wa Marehemu diwani Jubilate Kileo mwenye Miami Beach hotel alikuwa rafiki wa karibu na Mafia mmoja kutoka familia ya Laizer mwenye Palson Hotel kipindi hicho akiwa anamiliki timu ya Mpira ya Palson.

Kama umepita Kaloleni nyumbani kwa J. Kileo utaona marekebisho ya nyumba ya Marehemu Mzee Jubilate...kwakweli inapendeza sana kwasasa.
Jubilate Kileo alikuwa na binti yake mmoja changu alikuwa anajiuza pale Mrina
 
alikuwa anawashughulikia au alikuwa mentor wao, mfano sabaya
Angalau aliwashughulikia wakapotea,kuna moja wasiojulikana walikosea tu timing Tarime, kuna moja Mwanza akalipora bilioni 4 kwenye akaunti yake,jingine lilikimbia sauzi,aliyajua majizi yote kwa sababu alikuwa kwenye system na alijua michezo yao hata alivyodili nao alikuwa na taarifa nao wote. Kuna limoja lilimzulumu mjane nyumba Magu akamsaidia kuirudisha nyumba ikihisiwa alishiriki njama za kumuua mume Ili apate nyumba hii nyumba mme aliikopea, michezo yao siku ya marejesho ya riba yanapotea au kuzima simu Ili yapore nyumba.
Mkwere ndie aliyafuga majizi yakawapiga wageni na wabongo pia, huku yakimwaga pesa kwenye muziki. Mengine yalikufa vifo vibaya. Mengine yanajifanya kujifichia kwenye dini.
Angalau jpm aliyatikisa majizi
 
Sema watu wanazidiana level, unataka kushindanisha majambazi kwa matukio, Jombi kwao Mbeya na wewe kama kwenu Mbeya inabidi tukuelewe
Kisa cha jombi kina uzi humu ndani msachi
 
Miaka ya 80 kuna jambazi aliitwa Nyau, katika mazindiko yake alilishwa moyo wa paka. Akikurukia shingoni alikaba na kurarua kama paka. Huyu jamabazi aliteleza mikononi kwa PGO kama nyoka anavyoteleza mikononi mwa mwanadamu.

Alikua na hirizi hiyo akiivaa risasi zilikua zinapita bila kumdhuru. Alikinukisha Dar na kwenda kujificha Tanga vijijini huko kwa wakwe zake.

Aliuzwa na mke wake, mke wake alikula dili na wajomba kuwa akiwasaidia kumkamata yeye hatakua na hatia. Aliwaambia akiwa amevaa hirizi yake hamuwezi kumkamata.yupo wapi siku hizi

Basi bwana alikaa ndani muda wote, kuna siku mke wake alimwambia si aende nje akapate fresh air, jamaa alitaka kuvaa hirizi mkewe alimwambia unavaa ya nini si unaemda hapo tu. Kumbe nje wajomba wamezunguka nyumba usawa wa vichaka.

Nyau alikamatwa kizembe sana bila hirizi yake.
U
 
Hao vibaka tu ,ndo mana Jombi alikua anasubiri waibe aende akawaibie au la wampe mgao.
Jombi ndio jambazi toka mbeya tanzania yote toka 80s mpaka akafa aliyetikisa.
hao walisakwa na rais mmakonde,
JOMBI alipigiwa akaombwa aache mambo yake atulie
akabugi akaenda huko huko Arusha akapiga tukio na tatizo aliua wazungu kadhaa akaiba madini wakamkamatia manyara huko maporini katika kutoroka.pale ndo akafungwa.
Jombi, Tunyande, Masoli, Mtega a.k.a Kisangani, na vijana wao hatari sana Charles Tende, BOOB G, Mophat walitisha sana. ukimiliki VX unalazimika kuwalipa kodi ya ulinzi ili wasilichukue. Siitamani ile Meya ya hao jamaa.
 
Miaka ya 80 kuna jambazi aliitwa Nyau, katika mazindiko yake alilishwa moyo wa paka. Akikurukia shingoni alikaba na kurarua kama paka. Huyu jamabazi aliteleza mikononi kwa PGO kama nyoka anavyoteleza mikononi mwa mwanadamu.

Alikua na hirizi hiyo akiivaa risasi zilikua zinapita bila kumdhuru. Alikinukisha Dar na kwenda kujificha Tanga vijijini huko kwa wakwe zake.

Aliuzwa na mke wake, mke wake alikula dili na wajomba kuwa akiwasaidia kumkamata yeye hatakua na hatia. Aliwaambia akiwa amevaa hirizi yake hamuwezi kumkamata.

Basi bwana alikaa ndani muda wote, kuna siku mke wake alimwambia si aende nje akapate fresh air, jamaa alitaka kuvaa hirizi mkewe alimwambia unavaa ya nini si unaemda hapo tu. Kumbe nje wajomba wamezunguka nyumba usawa wa vichaka.

Nyau alikamatwa kizembe sana bila hirizi yake.
Nyau, King of Kings alikuwa akipita line polisi anawapa watoto wa line pipi na biskuti. kulikuwa pia na chizi mmoja alisumbua sana Hamisi Nindi siku anauawa mitaa ya city center alileta mtafaruku mkubwa sana baada ya kubadilishana risasi kadha na polisi.
 
Mussa Chesa mzaliwa wa kazuramimba alipiga tukio la ubungo mtaa wakitoka kuiba bank. Tukio la risasi ubungo mataa mwalikumbuka miaka ya nyuma kalielezea kwenye simulizi zake,huyu alikuwa shida tabora Kigoma burundi kahama aliua Mzungu hirizi kama zote risasi haiingii. Leo ameokoka na ameapa vita na shetani ni muinjilisti siku hizi anamuhubiri Kristo. Ukimmsearch unampata kaeleza matukio yake yote ya ujambazi aliyofanya na idadi ya watu aliowaua kwa risasi na uchawi, Ili awe gwiji kwenye wizi ilibinidi ajifunze uchawi kwenye wizi na uchawi kafanya makubwa Sana hata akawa mkuu wa kitengo cha misukule TANZANIA. Amewasumbua Sana police Kigoma nk alipokata shauri kuachana na yote na kuamua kumtumikia Mungu hata police awakuamini na kesi zake zote walimfutia. Akawa msaada wa police kuwakamata majambazi wengine. Ndie aliyekuwa gwiji wa wizi kwenye treni ya abiria akimiliki vikosi vinamuibia na kuleta hesabu.
.

Pia ameshiriki kuwauzia misukule wachungaji feki alipokuwa mkuu wa kitengo cha misukule nchini.
Alitaka kupigana studio na diamond baada ya diamond kupora biti yake studio.Visa vyake vyoote amevichezea movie na simulizi youtube.Kwenye redio cloud fm,RFA na channel tv mbalimbali.

Wa pili anaitwa Emma nae alikuwa shida yaani primitives hasa ameua watu wengi sana kwa bunduki ziwa victoria wakiiba samaki na engine,amewakata mikono wavuvi wengi sana kwa staili ya zile nguo za carwash salama yako ujitupe majini,kaua watu wengi sana kwa uchawi na uganga pia
Huyu ni mwanzilishi wa kundi hatari dar la komandoo Yosso na ndie alishiriki tukio la kiwanda cha sukari TPC Moshi wakaua mhasibu nk pia kaeleza uhalifu alioufanya Dar , Arusha na Moshi yeye ndio walikuwa ni waanzilishi wa kundi la komandoo Yosso wamefanya uhalifu Mkubwa Sana dar ikiwemo kuua, kulemaza watu wengi sana, walitaka kumdindishia Mrema akiwa Waziri wa mambo ya ndani walikula Sana bullets kundi likasambaratika akakimbilia Moshi akafanya Sana uhalifu alienda kuokokea jela leo ni mtumishi wa Mungu.
Hawa ndio wachungaji wa ukweli maana wanamjua shetani ndani nje kwa maana wamemtumikia pasipo faida wameamua kumtumia Muumba wao. Ila Mussa Chesa alikuwa shida amewatesa sana police na raia kila mtu aamini wokovu umemuingia.


alikuwa ni teja hatari mitaa ya fire, jangwani,wamepora Sana tena mchana.Wamefanya Sana vurugu kwenye mabaa,nk.

Simulizi zao zinasisimua na kuonyesha uKuu wa Mungu mtu anavyoweza badilika.
Wanajutia Sana matendo yao hasa watu waliowaua .
 
Back
Top Bottom