Abel na Kaini (kizazi cha Adamu na Hawa); Je, wake zao ni kizazi cha nani?

Abel na Kaini (kizazi cha Adamu na Hawa); Je, wake zao ni kizazi cha nani?

Una maswali marahisi ajabu.Tatizo kila kitu mnatumia mantiki.

Wale walikuwa wanazaliwa wawili,dada na kaka wa kwanza kisha dada na kaka wa pili.Yule ambaye alizaliwa na dada yake wa kwanza pamoja anaozeshwa na dada wa uzao wa pili.Kwahiyo kila kitu kina jibu na kiko wazi.

Lakini Allah anafanya mambo na kuumba atakayo na kuwekea utaratibu na sheria vile alivyoviumba.Mathalani sheria ya torati si sheria ya injili wala si sheria ya zaburi wala si sheria ya Qur'an isipokuwa iwe imewafikiana na Qur'an.

Unapouliza swali hilo pia uulize swali la mbona kuna viumbe wengine wameubwa bila mama wala baba na mwengine ameumbwa bila baba na sisi tumekuwa zao la baba na mama ?

Sababu Allah aliyetukuka ni mjuzi wa kupangilia mambo na mjuzi wa kuumba na kuweka taratibu ameamua kufanya vile anavyotaka.

Leo hii kuna kifo na kuna uhai na kila nafsi amesema itaonja umauti,sasa wale Mulhidi(Wakana Mungu) wakatae kufa au waseme kufa hakupo.Maana yeye aliyetuumba ameshasema na hiyo ndio sheria na angetaka angeumba uhai peke yake lakini ameamua kuumba uwili,yaani kifo na uhai,ili atupe mtihani kwamba ni wakina nani wataamini na kina nani hawataamini.

Kwahiyo muwe mnatumia akili akili zenu kuhoki kuliko tukuka sio zile zenu eti kama A ni 2 na B ni mbili basi A ni B.Upuuzi mtupu.

Ajabu iliyoje sisi tunaoamini uwepo wake na sheria zake nafsi zetu zimetulizana na majibu tunayo.

Tatizo vijana nyinyi wa leo mnafikiria kama wakubwa zenu waliofikiria wale wakina Socrates,Thalesi,Homeri,Anaksimenes,Anaksimanada,Demokretus,Zeno wa Abdela,Plato,Pythagoras na wasio kuwa wao.Wao wamekosewa na nyinyi mnakosea kama wao.

Kuna tatizo pia huwa naliona kwenu huwa mnauliza maswali ya kitoto mnajibiwa na nyinyi mkiulizwa maswali huwa hamjibu bali hamuwezi kujibu,hili ni tatizo kubwa.

Msingi wenu ni nadharia na majaribio(Experimental data),huu ujinga sisi tulitahadharishwa nao zamani.Kwanini vipimo vyenu haviendi bila nadharia na kuchukulia (Assumptions) ? Soma mkasa wenu juu ya Orbits.

Halafu huwa nakushangaa wewe bado upo katika zile zama ambazo wanasayansi walikuwa walikuwa wakana Mungu,wenzako leo hii wamekubali uwepo wake na wakasema ndio msingi wa mambo yote.

Kwahiyo Mola muumba anafanya vile anavyotaka tena kwa bora uliopea nafanowe hakuna.
Kwahiyo huu ujinga ndio mnaomezeshwa?

Una ushahidi gan kwamba Allah ndiye aliyetuumba?

Una ushahidi gani wa kuwepo kwa Allah?

Umesema kila mtu na Dada yake wa kuzaa nae, majina yao ni yepi?

Kama Mungu anafanya atakavyo yeye bila kushirikisha wanadamu, ina maana yeye ni dictator?
 
ukifikiria deep hata kusema sisi ni wanadamu napo tunakosea.. sababu neno binadamu linatokana na neno Bin Adam >>> mwana wa Adamu >>> mwanadamu.

mkuu, our whole life is a lie.
SURE!....tunajiita watoto wa mtu asiye kweli.
 
1. All humans are descendants of Adam and Eve.

In Genesis 4:1,2, we read, "And Adam knew Eve his wife: and she conceived, and bare Cain, and said, I have gotten a man from the LORD. And she again bare his brother Abel." And in Genesis 5:3, we read, "And Adam lived a hundred and thirty years, and begat a son in his own likeness, after his image: and called his name Seth."

In other words, we are told certain details about three sons born to Adam and Eve. It is recorded in Genesis 3:20, "And Adam called his wife's name Eve; because she was the mother of all living." Thus all human beings are descendants of the first woman, Eve. There were no other women—just one woman, Eve.

In I Corinthians 15:45, Paul tells us that "the first man Adam was made a living soul." In other words, Adam was the first man—there were no other men at the beginning. And in Acts 17:26, Paul states that the God who made the world "hath made of one blood all nations of men for to dwell on all the face of the earth."

All human beings are related, because they are alldescendants of the first man, Adam, and the firstwoman, Eve.

As marriage in the Bible specifies one man for one woman for life, this means Christians have to be able to explain how Adam and Eve's sons could marry and have children to propagate the human race. Thus we need to be able to answer the question concerning Cain's wife.

One can actually answer this question with just a little Bible knowledge. Genesis 5:4 tells us that Adam and Eve "begat sons and daughters." Josephus, the Jewish historian, states that "The number of Adam's children, as says the old tradition, was thirty-three sons and twenty-three daughters." The point, of course, is that Adam and Eve did have many children.

Therefore, brothers must have married sisters at the beginning. Remember that the law against close intermarriage was not given until the time of Moses—e.g. "none of you shall approach to any that is near of kin to him" (Leviticus 18:6). There was nothing wrong with brother and sister marriages, originally. If you think about it, that is the only way to populate the world, starting with only one pair. Notice that Abraham married his half sister with no condemnation from God, even though this was later forbidden.

Also, as Adam and Eve were created perfect, their genes would have been perfect. As the curse God placed upon creation started to operate only after they sinned, their descendants would not have had many mistakes in their genes. These mistakes (harmful mutations) add up only after a long period of time.

So brothers and sisters (Adam and Eve's children) could have married and not had the problems of deformities in their offspring as might well happen today, if such close relatives married and had children. This is because today humans have lots of mistakes—because of the curse—in their genes. This may cause problems when matching pairs are inherited from both parents, as is much more likely with close intermarriage.

Some people, though, say that there must have been people other than Adam and Eve, because Cain went to the land of Nod and found his wife. First of all, the Scriptures quoted above make it obvious that there was only one man and one woman from whom came all other human beings.

Secondly, the Scripture says that Cain went to the Land of Nod and "knew" (had sexual relations with) his wife. John Calvin, in his commentary on Genesis, and most other conservative expositors, make the point that Cain was married before he went to the land of Nod.

Since men and women lived to be hundreds of years old in the primeval world, populations grew rapidly, and Cain had plenty of time to marry a sister (or possibly a niece), move to Nod, and build a city for his own descendants and others
 
ni historia au hadithi zinazowahusu waisraeli..

MATAYO. 19:28
Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

hapo unaona hio hukumu itatolewa kwa kabila kumi na mbili za israeli, cha kushangaza unamkuta mndengeleko kama mimi na ye anajihesabia ni mmoja wa makabila hayo wakati yeye ni mndengeleko na mama ni mfipa.. wapi na wapi na kabila 12 za israeli.

hatari sana.
Hahahahaaaa mkuu Imani za Dini ni kifungo ukishaingia kutoka inahitajika ukombozi wa kifikra sio kiroho
 
Kwahiyo huu ujinga ndio mnaomezeshwa?

Una ushahidi gan kwamba Allah ndiye aliyetuumba?

Una ushahidi gani wa kuwepo kwa Allah?

Umesema kila mtu na Dada yake wa kuzaa nae, majina yao ni yepi?

Kama Mungu anafanya atakavyo yeye bila kushirikisha wanadamu, ina maana yeye ni dictator?
Ha ha ha.Kwahiyo ukitajiwa majina ndio utaamini mzee ?

Sasa Mola hana haja ya kutaka ushauri wala msaada.Yeye amekamilika na jakosei.

Uliza maswali ya msingi mzee.

Ushahidi wa uwepo wake upo kupitia maandiko,akili iliyo salama,maumbile na milango ya fahamu.

Ndio hivyo mzee hamna namna acha tumeze tu huu ujinga na ni hiyari tu wala hatuja tenzwa nguvu.

Ila ingekuwa vizuri ungekuwa unazivunja hoja zangu.Halafu kila siku unarudia maswali yale yale.

Ngoja nikupe kisa kimoja.

Zama za imamu Abuu Hanifa Allah amrehemu alikutana na Mulihidi mmoja akawa anajadiliana nae.Nikisema Mulhid I ni myakinifu yaani wale wenye kuamini kwenye vitu vinavyoonekana(Materials World) au watu wa Maada.Tofauti na nyinyi wa leo hata hoja za kubabatiza hamna wale walikuwa vizuri sababu walikuwa wanasoma na wamajua kucheza na lugha barabara.

Sasa imamu katika kumjibu hoja yake kwa hoja ya kiakili akamwambia hivi.

"Kuna siku nilikuwa naenda bandarini nikaoja jahazi kubwa mno wala sikuona hata mtu mmoja,jahazi likawa linajipakilia mizigo lilivyojaza ile mizigo likaondoka zake,likafika huko lilipofika likatia nanga kisha likaanza kupakua mizigo mpaka ikaisha".

Kwa haraka yule myakinifu akapinga hali ile,yakuwa jahazi haliwezi kupakia mizigo lenyewe wala kujiendesha lenyewe bali wala kupakua mizigo lenyewe.

Imamu akamwambia basi ndio vivyo hivyo ilivyo katika ulimwengu,yupo mwenye kuundesha tena katika mpangilio maridhawa usio mfano.

Lakini swali kama hili au hoja ya myakinifu huyu wewe huwezi kuitoa sababu huwezo wa kufikiria kama huyu myakinifu huna.Hiyo ndio tofauti kubwa iliyopo kati yenu na wale wakubwa wenu wale kidogo walikuwa wanajiuliza kwa umakini kidogo.

Ila nyinyi ni vurugu na kujaribu kupinga.
 
Kwahiyo huu ujinga ndio mnaomezeshwa?

Una ushahidi gan kwamba Allah ndiye aliyetuumba?

Una ushahidi gani wa kuwepo kwa Allah?

Umesema kila mtu na Dada yake wa kuzaa nae, majina yao ni yepi?

Kama Mungu anafanya atakavyo yeye bila kushirikisha wanadamu, ina maana yeye ni dictator?
Kaka sisi wenzenu tunaelewa vitu na hatukariri.Nimekuuliza kwahiyo nikuambia majina ya hao Dada zao ndio utakubali uwepo wa Allah au ?

Halafu nilisema dada wa huyu anapewa kaka wa yule Dada mwingine.Huo ulikuwa utaratibu hasa kwa kizazi kile na kizazi chetu au zama zetu Mola ameweka sheria nyingine.Ya kwamba wewe leo hii ni haramu kumuoa dada yako tumbo moja au msichana ambaye umenyonya nae ziwa moja.
 
duniani kuna races 4 ambavo zinaweza kuwa divided into more 3o gorups ambazo ni caucasian, mongoloid or asian, negroid or black and australoid. na hizi races zote haziweza toka kwa wat wawili tu.
Zinatoka kwa watu wangapi ?
 
ukifikiria deep hata kusema sisi ni wanadamu napo tunakosea.. sababu neno binadamu linatokana na neno Bin Adam >>> mwana wa Adamu >>> mwanadamu.

mkuu, our whole life is a lie.
Sasa kosa hapo likowapi na ulichokikosoa kiko wapi mzee ?
 
Kaka sisi wenzenu tunaelewa vitu na hatukariri.Nimekuuliza kwahiyo nikuambia majina ya hao Dada zao ndio utakubali uwepo wa Allah au ?

Halafu nilisema dada wa huyu anapewa kaka wa yule Dada mwingine.Huo ulikuwa utaratibu hasa kwa kizazi kile na kizazi chetu au zama zetu Mola ameweka sheria nyingine.Ya kwamba wewe leo hii ni haramu kumuoa dada yako tumbo moja au msichana ambaye umenyonya nae ziwa moja.
Hivi kwenye hayo maswali yangu umejibu lipi? umeacha mangapi?

Kwahiyo huoni yofauti ya meli na binadamu?

Ulijuaje kwamba kila mtu alikuwa na Dada ili hali huwafahamu hao Dada zao?

Hayo maandiko unayaamini vipi kwamba yalitoka kwa Allah? je kama yaliandikwa na watu wakale?
 
ukifikiria deep hata kusema sisi ni wanadamu napo tunakosea.. sababu neno binadamu linatokana na neno Bin Adam >>> mwana wa Adamu >>> mwanadamu.

mkuu, our whole life is a lie.
Kuna kitu kinaitwa nasaba na hii ni elimu pia na ina watu wake.Kuna ada na desturi huu ni ukumbusho tu yaani ukiwa unauliza maswali kama haya vitu hivyo lazima viwepo akilini mwako.

Wewe leo hii leo hii umezaliwa na una masaba yako.Kwa mtu makini lazima atajiuliza mimi sijatokea pasipo julikana lazima nina asili yangu.Wewe ni zao la wazazi wako na wazazi wako ni zao la babu yako mpaka hukoo.Kwahiyo tunaposema sisi ni wana wa adamu yaani chimbuko au wa kwanza wetu ni Adamu alayhi salaamu.

Lakini pia katika desturi hata babu naye ni baba japo hajanizaa yeye ila yeye ni chimbuko langu.

Halafu msiwe mnalazimisha vitu viende mnavyotaka nyinyi ukweli ni kinyume.Vimeshapangiwa utaratibu na mzee na katika utaratibu ni wewe ukila lazima ukakitoe kile ulichokila au ulichokinywa na utaratibu huu huwezi kuuepuka na lazika ulale mzee huo ndio utaratibu Mzee na Allah mwenyewe ameshatwambia ya kuwa amefanya mchana kuwa maisha yaani watu kujitafutia rizki na usiku kuwa mapumziko yaani baada ya kutafuta basi usiku unapumzika hata wewe utaratibu huu na mfano wako mnaufata na ndio maana Allah anatuambia tuangaliea maumbile ya mbingu na ardhi tunaona ishara za kuwepo kwake sasa msiwe mnafikiria kwa mkopo yaani nusu nusu,fikirieni mazima.
 
Nilisikia walizaa mapacha wa kike na kiume kwa hiyo wakaoana kwa kubadilishana yaani mfano amuoe pacha wa abeli na ukiziangatia zamani hawakuhesabu wanawake. Mi mwenyewe sijui ila nimejibu kutokana na kusoma huhkuhuku JF.
Abel aliuwawa hata kabla hajaoa na kuzaa
 
Hivi kwenye hayo maswali yangu umejibu lipi? umeacha mangapi?

Kwahiyo huoni yofauti ya meli na binadamu?

Ulijuaje kwamba kila mtu alikuwa na Dada ili hali huwafahamu hao Dada zao?

Hayo maandiko unayaamini vipi kwamba yalitoka kwa Allah? je kama yaliandikwa na watu wakale?
Yametoka kwake sababu binadamu hana uwezo huo,na walipewa mtihani wale wa mwanzo katika kupinga maneno ya kuwa kama kweli hayatoki kwa Allah aliyejuu basi walete japo mfano wa aya moja huku wakishishirikiana na wakubwa wao tena makundi kwa makundi.

Pia yanatoka kwake sababu yana bainisha haki na batili na ni kweli tupu.

Kwenye meli na binadamu hakuna tofauti nilichokiongelea pale ni sababu ya kufanya kazi kwa meli na sababu ya kuishi kwa binadamu viwili hivi vinakutana katika ile sababu kwahiyo utofauti haupo.

Pili uwe unasoma hoja zangu vizuri mzee na kuyarejea maswali yako vizuri.

Katika maswali yako sija acha hats moja ndio maana kuna swali nilikujibu kwa swali na kuna swali nikakupa akiba ya swali ya kwamba Je ukitajiwa majina ya hao dada zao ndio utaamini kwamba Allah yupo au ?

Mimi majina ya hao dada zao siyajui.Vile vile mimi kutokuyajua majina yao hakubadilishi ukweli.
 
Kuna mengi ambayo hatuambiwi, katika baadhi ya texts Hawa hakuwa mke wa kwanza wa Adamu, mwanamke waliyeumbwa pamoja na Adam aliitwa Lilith, huyu alitofautiana na Adamu na akakaidi hadi maagizo ya Mungu na kwa kuwa alikuwa na nguvu akaamua kuondoka na kumwacha Adamu, hivyo Mungu akaamua kumuumba Hawa kutokana na ubavu wa Adam ili awe submissive kwa Adam tofauti na Lilith ammbaye aliona wako sawa, Still inaonekana Adam na Hawa na watoto wao watatu wanaotajwa ambao ni Kain, Abel na Seth hawakuwa binadamu pekee katika ulimwengu wakati ule, Kain baada ya kumuua nduguye alifukuzwa na inaonekana aliomba kwa Mungu kuwa anahofia huko aendako kuna majitu ambayo yangemuua. Kuna mengi zaidi ya haya yanayosemwa na vitabu vya imani zetu hizi
 
Hivi kwenye hayo maswali yangu umejibu lipi? umeacha mangapi?

Kwahiyo huoni yofauti ya meli na binadamu?

Ulijuaje kwamba kila mtu alikuwa na Dada ili hali huwafahamu hao Dada zao?

Hayo maandiko unayaamini vipi kwamba yalitoka kwa Allah? je kama yaliandikwa na watu wakale?
Mimi namaani yametoka kwake kwa ushahidi mwingi.Sasa wewe nithibitishie kwamba hayakutoka kwake.Ukiweza kuthibitisha kichwa changu halali yako.

Naona tunawalea sana.Thibitisha kwamba hayakutoka kwake sio dhana tu mara watu wa kale wameandika mara oo hiki.
 
Mwanzo 6
1 Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,
2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

Vv
Wanadamu ni akinanani? Na wana wa Mungu ni akinanani? Nipo gizani nieleweshe.
 
Binadamu wa kwanza kuumbwa Na Mungu ni Adam Na Hawa.Watoto waliowazaa ni Abel Na Kaini.Abeli Na Kaini walioa je Wake zao ni kizazi cha nani?
Mungu alipomuumba Adam na Hawa,Haina maana kwamba kulikuwa hakuna binadamu wengine,.Ila Adam amesimama kama mfano ili upate kuelewa.
 
Swali jepesi sana.iko hivi
Adam na hawa hawakuwa watu halisi kama tulivyo mimi na wewe bali yalikuwa ni majina ambayo yalitumika kuwakilisha makundi ya watu.so Adam alikuwa anawakilisha wanaume na hawa alikuwa anawakilisha wanawake.lengo la kitabu cha mwanzo ni kuonyesha historia ya binadamu so isingewezekana kuzungumziwa namna kila mtu alivyopatikana so yakachaguliwa majina mawili ili yawe vielelezo au kuwakilisha makundi hayo ya watu.ukisoma vizuri kitabu chenyewe kinajieleza mfano habari ya nyoka kuongea unaona kabisa kwamba No kitu ambacho hakileti maana.so mwandishi wa kitabu kile alitumia majina ya adamu na hawa kwa maana hizo.mfano mzuri ni hadithi za sungura na fisi ambazo hutumia majina hayo kuwakilisha watu halisi.
Hayo mafunzo umeyapata wapi mkuu,so shetani alivyomlaghai Eva inamaanisha aliwalaghai wanawake wote kwa mkupuo,kisha hao wanawake wakaenda kuwalaghai wanaume, so hata ule mti wakati labda ni pori la kati.
 
Mimi namaani yametoka kwake kwa ushahidi mwingi.Sasa wewe nithibitishie kwamba hayakutoka kwake.Ukiweza kuthibitisha kichwa changu halali yako.

Naona tunawalea sana.Thibitisha kwamba hayakutoka kwake sio dhana tu mara watu wa kale wameandika mara oo hiki.
Kichwa chako nikipeleke wapi?

Mmezoea kuchinja watu kama hao Boko haram na ISIS?

Ndio hivyo mlivyoagizwa?

Thibitisha kwanza kama Allah yupo.....je umewahi kumuona, kumsikia, kumhisi?....unaabuduje kitu usichokuwa na uhakika juu ya uwepo wake?
 
Back
Top Bottom