Abel na Kaini (kizazi cha Adamu na Hawa); Je, wake zao ni kizazi cha nani?

Abel na Kaini (kizazi cha Adamu na Hawa); Je, wake zao ni kizazi cha nani?

Kichwa chako nikipeleke wapi?

Mmezoea kuchinja watu kama hao Boko haram na ISIS?

Ndio hivyo mlivyoagizwa?

Thibitisha kwanza kama Allah yupo.....je umewahi kumuona, kumsikia, kumhisi?....unaabuduje kitu usichokuwa na uhakika juu ya uwepo wake?
Nimesema kichwa sababu kichwa bila kichwa siwi mimi yaani nimekuonyesha thamani ya kichwa na wewe kutoweza kuthibitisha kutokuwepo kwake.

Pili suala la mimi na boko haramu na ISIS ni vitu kando wala hatupikwi chungu kimoja.Si kosa lako sababu unapelekwa nasukumo wa hisi.Nimekupa udhuru Mshairi anasema :

Akiba hii chukua ** Mjinga kimjibu hupea
Akizidi tukania ** Wewe hasira zuia
Enda mbali kutulia ** Mwache pweke kizogoa
Yu pamojawe Jalia ** Lilo bora vumilia

Turudi kwenye hoja yako ya kuhisi,kuona.Swali kutokuonekana kwa jambo au kitu ndio sababu ya kutokuamini uwepo wake ? Jibu ni hapana.

Leo vingapi huvioni na wala huvihisi lakini unaviamini na vina kushughulisha ?Kesho huioni wala huihisi lakini inakushughulisha na nani amekwambia kwamba sharti la Mola kuabudiwa ni mpaka umuhisi au umuone ? Bila shaka unafikiria kitoto kabisa.

Leo hii njaa huioni lakini unaamini ipo.Viko vingi vyenye sifa ya kutokuonekana na kutohisiwa Bali
Hata kutoguswa lakini unaviamini.

Njaa ipo lakini huwezi kuigusa hewa ipo lakini huwezi kuigusa wala kuiona.Kwahiyo jaribu kufikiria kikubwa ili ulete maswali ya msingi kidogo.
 
Abel alikua na Pacha wa kike, akaoa huyo Pacha wake, na Kaini alikua nae ana Pacha akaoa huyo! Kilichofanyika ni kutowaandika wanawake Majina yao, ndio ulivyokua utamaduni wa Wakati wao. Zamani ulikua unazaliwa na mkeo au mmeo.
 
Kichwa chako nikipeleke wapi?

Mmezoea kuchinja watu kama hao Boko haram na ISIS?

Ndio hivyo mlivyoagizwa?

Thibitisha kwanza kama Allah yupo.....je umewahi kumuona, kumsikia, kumhisi?....unaabuduje kitu usichokuwa na uhakika juu ya uwepo wake?
Kashalika Allah si kitu wala hawi kitu Allah ni muumba na mwenye kupaswa kuabudiwa.
 
Kichwa chako nikipeleke wapi?

Mmezoea kuchinja watu kama hao Boko haram na ISIS?

Ndio hivyo mlivyoagizwa?

Thibitisha kwanza kama Allah yupo.....je umewahi kumuona, kumsikia, kumhisi?....unaabuduje kitu usichokuwa na uhakika juu ya uwepo wake?
Halafu sijakwambia sina uhakika wa uwepo wake.Nina uhakika wa uwepo wake ndio maana namuabudu.

Leta hoja za msingi.Ila usisahau kunithibitishia kutokuwepo kwake na kunipa ushahidi ya kwamba maneno hayo si ya Allah.
 
Na je kaini alivomua nduguye abeli alifuzwa akaenda nchi ya mbali na alienda kuishi na watu. je watu wale ni wa kizazi ipi?
 
Swali jepesi sana.iko hivi
Adam na hawa hawakuwa watu halisi kama tulivyo mimi na wewe bali yalikuwa ni majina ambayo yalitumika kuwakilisha makundi ya watu.so Adam alikuwa anawakilisha wanaume na hawa alikuwa anawakilisha wanawake.lengo la kitabu cha mwanzo ni kuonyesha historia ya binadamu so isingewezekana kuzungumziwa namna kila mtu alivyopatikana so yakachaguliwa majina mawili ili yawe vielelezo au kuwakilisha makundi hayo ya watu.ukisoma vizuri kitabu chenyewe kinajieleza mfano habari ya nyoka kuongea unaona kabisa kwamba No kitu ambacho hakileti maana.so mwandishi wa kitabu kile alitumia majina ya adamu na hawa kwa maana hizo.mfano mzuri ni hadithi za sungura na fisi ambazo hutumia majina hayo kuwakilisha watu halisi.
Umechemka kutetaa hoja yako
 
Abel alimuoa pacha wa Kaini na Kaini alitakiwa amuoe pacha wa Abel ndipo Kaini akakataa kwani pacha wake alikuwa mzuri sana kuliko pacha wa Abel.Baada ya mzozo Adam akapewa maelekezo na Mwenyezi Mungu waandae sadaka na yayule itakayochukuliwa atakuwa imekubaliwa.Sadaka ya Abel ilikubaliwa na Kaini alikasirishwa sana na kuahidi lazima atamwangamiza Abel.Kaini alipewa mbinu na Shetani ya kumuua Abel na akamuua.Abeli akawa ndiyo mtu wa kwanza kuuwawa na Kaini akawa mtu wa kwanza kua.
Weka basi hata vesrse kidogo from Biblia au Quraan ku support hili jibu
 
Back
Top Bottom