Adui wa Tanzania ni Uvivu hasa kwa wanaume wanaoishia kujikita kwenye Rushwa na Kubeti

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Maadui wakuu watatu wa Mtanzania yaani Ujinga, Maradhi na Umaskini mama yao ni Uvivu na baba yao ni Tamaa

Watanzania wanaume ni wavivu sana wa kufikiri, wanapenda mteremko na mambo mepesi mepesi na hapo ndipo wanaporidhia Mkataba wa Umaskini na Shetani

Nimemsikia Mtaka akiyataja makabila matano yaliyoshikilia Uchumi wa Tanzania Wakinga, Wapemba, Waha, Wachaga na Wanyantuzu lakini hasemi wamefanikiwaje kushika Uchumi kama ni wakulima sana, wafugaji sana ama ni wachuuzi wa bidhaa za viwandani.

Itoshe tu kusema Watanzania ni lazima tubadili namna yetu ya kufikiri na tuache kabisa kufikiri ki Nyerere Nyerere.

Kwa bahati mbaya Elimu yetu inazalisha waongeaji naa siyo watendaji na ndio sababu wasioingia darasani huyaona mafanikio kwa wepesi.

Mungu wa mbinguni awabariki sana!
 
Wapo mkoa gani? sijawahi kusikia hili kabila asee
 
Ingawa umeongelea uvivu ila hoja kuu iliyopo kwenye uzi wako ni ujinga.

Hili limezungumzwa sana humu JF hata dada yetu FaizaFoxy amelisemea humu jana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…