Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Vile vifaa ni vya kichina vingine ni feki kabisa.
Nafikiri hii ni moja sababu ya watu kufeli physics.
Tena hata vile vinavyotumika o'level vya practical ya electricity ni vya kichina vinaleta data za uongo.
Kufaulu pale unahitaji akili ya ziada (uwe kichwa kwelikweli)
Mimi prac za Phyz nilikuwa nafoji sana kuanzia O-level hadi Advance, chache nilikuwa nafanya real
 
Mimi sijapitia huko nilivikuta FTC.DIT kwenye electric and electricity nagonga umeme vibaya hadi mwalimu wa umeme akawa ananikubali lakini hapo hapo akawa anashanga huyu jamaa mbona electronics ina msumbua hadi Leo. Ni electrician mzuri sanaa ila maisha hayana formula. Aise nafanya busy nyingine kabisa.baada ya miaka nane ya kuhasle kwenye kazi za umeme.
 
Phyz ilikuwa ngumu sana lakini nilikomaa naye na ikanitoa kimasomaso NECTA.

Miongoni mwa somo lililokuwa linanipanikisha kwenye pepa ilikuwa ni Phyz.

Sikuwahi kumaliza pepa hata moja la physics, siku moja nilienda kupiga mtihani(series) kwa mtiga ilikuwa pepa one.

Mechanics ilikuwa imesimama aisee, kila swali nikigusa haliendi na lina concepts mpya. Muda wa masaa 3 nauona kama lisaa limoja.

Baada ya Mechanics kugoma nikahamia swali la Environmental Physics nikajipoza kidogo kabla navuta pumz nasikia muda umeisha, nikapanic sana. Nilirudi shule nimenuna sana.

Sikukata tamaa nikakaza buti zaidi, wiki inayofuata nikarna tena kupiga series nyingine ambayo ilikuwa pepa two.

Kufika kituoni nikakuta matokeo ya wiki iliyopita yamebandikwa, nikajikuta nipo top ten japo niliambulia 40%, kuona hivyo nikajisemea kumbe mambo yanawezekana hapa. Nikaingia kupiga pepa na kwenye pepa hiyo nikawa na above 50% nikaingia top ten pia.

Kuanzia muda huo nikawa sikosi series kila wiki huku nikikomaa kusahihisha makosa yaliyojitokeza kwenye series zilizopita, ikafika muda nikaimprove na pepa moja nikawa wa kwanza. Hadi hapo nikacha kwenda kupiga series tena.

Physics ni somo nililotumia muda mwingi na pesa nyingi kulisoma kuliko masomo mengine.
Hongera kwa moyo wa uvumilivu
 
Haha aisee siamin o-level nilikua physics nagonga 90% kuja advance level nikawa napata namba za viatu daah yaani 12% 11%...ni maksi za kawaida sna kwangu haha nikajiona kama nimelogwa vile

Ila nikichek masela nao hoooi yaani siwezi sahau two years ya advance level ilikua kama miaka mia vile [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwa kweli physics ilinisumbuaga sana ila nashukuru kemia nilikua vizur kupita maelezo, chemistry na biology vikaniokoa necta ila kwa kwel ad physics nilizingua na nilikua siipendi toka moyoni hadi leo hii.
 
Hahaha Daaah physics ni balaa Kuna T.O mmoja hivi alimaliza 2006 alikuja Kutufundisha sisi tukiwa form 6 tukajiona Vilaza Wote.. vitabu vya Chand...Roger. vyote tuliona Tumemaliza na Hakuna Swali Gumu.. Jamaa Halafu alikuwa ana dharau balaa na Chuo alifukuzwa Kisa Dharau kwa Maprofesa kwahiyo akabak anapiga Tuition mtaani tu na Sifa Kibao na Kuwaona Watanzania wote hawana Akili ila Yeye peke yake

Ila Nakumbuka Siku ya Mtihani wa Physics Nilipiga msuli Usiku halafu kesho yake Pepa Asubuhi Na Nikasolve Maswali Kama matatu hivi ya Chand kwenye Pepa Yamekuja Vile vile Nikasema Nashukuru Mungu Ndalichako kaniona

Ila Yote tisa nitarudi Shule Zote ila Siyo Advance
Katika elimu ngumu nilyowah kusoma ni ile physics ya advance nilianza kuvurugwa siku ya kwanza tu naingia darasan
 
Katika elimu ngumu nilyowah kusoma ni ile physics ya advance nilianza kuvurugwa siku ya kwanza tu naingia darasan
Mkuu siku ya kwanza ulikutana na madude gani hayo aiseee?? Au nyie shuleni kwenu mlianza na yale wanaitwa Newton Rings ???
 
Phyz ilikuwa ngumu sana lakini nilikomaa naye na ikanitoa kimasomaso NECTA.

Miongoni mwa somo lililokuwa linanipanikisha kwenye pepa ilikuwa ni Phyz.

Sikuwahi kumaliza pepa hata moja la physics, siku moja nilienda kupiga mtihani(series) kwa mtiga ilikuwa pepa one.

Mechanics ilikuwa imesimama aisee, kila swali nikigusa haliendi na lina concepts mpya. Muda wa masaa 3 nauona kama lisaa limoja.

Baada ya Mechanics kugoma nikahamia swali la Environmental Physics nikajipoza kidogo kabla navuta pumz nasikia muda umeisha, nikapanic sana. Nilirudi shule nimenuna sana.

Sikukata tamaa nikakaza buti zaidi, wiki inayofuata nikarna tena kupiga series nyingine ambayo ilikuwa pepa two.

Kufika kituoni nikakuta matokeo ya wiki iliyopita yamebandikwa, nikajikuta nipo top ten japo niliambulia 40%, kuona hivyo nikajisemea kumbe mambo yanawezekana hapa. Nikaingia kupiga pepa na kwenye pepa hiyo nikawa na above 50% nikaingia top ten pia.

Kuanzia muda huo nikawa sikosi series kila wiki huku nikikomaa kusahihisha makosa yaliyojitokeza kwenye series zilizopita, ikafika muda nikaimprove na pepa moja nikawa wa kwanza. Hadi hapo nikacha kwenda kupiga series tena.

Physics ni somo nililotumia muda mwingi na pesa nyingi kulisoma kuliko masomo mengine.


kwenye necta physics ulipata grade gani? Mwifwa
 
Hongera mkuu mwifwa , kuna jamaa yangu mmoja alichukua PCM, aliniambia watu wanaopata Div 1 point 3 ya PCM:
A- kwenye physics A- kwenye chemistry na A- kwenye math ya "Advanced level" "wana matatizo nyumbani kwao, nlicheka sana.. Mwifwa Deadbody
Matatizo kama yapi?

Kama sio uongo huo
 
Back
Top Bottom