Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Advance Physics ilivyokuwa inatugeuka ndani ya chumba cha mtihani

Hili somo lilifanya nimtajirishe mgote maana kila pamphlet lake nilikua nalo ila bado kwa necta nikaunguza, nina uhakika prac ndio ilinibeba
Naona buroka alikuingiza chaka
Hahahahahahaaaaa.

Notes za Mgote zimenitoa kimaso maso na maswali yake mengi yaliyosolviwa kutoka vitabu mbalimbali.
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana, Enzi za Azaboy Taifa Kubwa. Aisee pale Mchikichini sidhani kama kuna banda sikuwahi kusomea lakini matokeo yake Physics ilichonitenda siyo Njema. Nilikuwa najua mpaka washikaji walinichangia buku buku ikafika Twenty ili nikapige forging ya Practical kwa Mtiga, kumbuka wandewa wakikupa hela yao lazima uwe makini sana kwa sababu hiyo buku kiadvance ni kubwa sana. Ila kilichonitokea ni historia ambayo haiwezi kufutika akilini mwangu
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana, Enzi za Azaboy Taifa Kubwa. Aisee pale Mchikichini sidhani kama kuna banda sikuwahi kusomea lakini matokeo yake Physics ilichonitenda siyo Njema. Nilikuwa najua mpaka washikaji walinichangia buku buku ikafika Twenty ili nikapige forging ya Practical kwa Mtiga, kumbuka wandewa wakikupa hela yao lazima uwe makini sana kwa sababu hiyo buku kiadvance ni kubwa sana. Ila kilichonitokea ni historia ambayo haiwezi kufutika akilini mwangu
Ulilambwa KARAI nini mkuu?
 
All in all wakuu, kuna Kitu kinaitwa Medicine, Duuuhhh ni hatari au akili chuo huwa zinapungua... Shikamoo Anatomy, Pharmacology na Pathology haya masomo sikuwahi kupata B, zilikuwa ni C tu zingine za After supplementary
Hayo masomo yana watabe wake.

Halaiki ni kutafuta C na kusonga mbele
 
Mstaarabu sana yule na ndio Head of Department.Ana sauti fulani hivi nzuriiiiiiiiiiiiii......

Yaah mpole sana baba yao alikua katekista tabora..alifaulu ifunda ila mambo ya utoto akazalishwa hvyo akakatisha masomo kulea mtoto so akaanza private school ...mdogo wake tulisoma nae primary some body Deogratius ...kile kichwa achana nacho
 
kama kuna vitopic nulikuwa najipigia basi ni projectile hata swali likunjwe vipi..., Tena ya kwenye vitabu ndio nilimeza hadi majibu, yaani nikiona tu swali nakumbuka na jibu bila hata kusolve, ....shughuli ilikuwa kwenye Electromagnetism aaaaah hapo nilivyoosha mikono
 
kama kuna vitopic nulikuwa najipigia basi ni projectile hata swali likunjwe vipi..., Tena ya kwenye vitabu ndio nilimeza hadi majibu, yaani nikiona tu swali nakumbuka na jibu bila hata kusolve, ....shughuli ilikuwa kwenye Electromagnetism aaaaah hapo nilivyoosha mikono
Projectile likikukuta swali la kuderive utaeleza, bora ya kutafuta height na range.
 
Pure Math aisee.

Math sio kitu kwa mnyama physics,sema math inachukuliwa janga kwa kuwa inasomwa na watu wengi na failures wanakuwa wengi ukilingasha na wachache walio opt PHYSICS.
 
Pure Math aisee.

Math sio kitu kwa mnyama physics,sema math inachukuliwa janga kwa kuwa inasomwa na watu wengi na failures wanakuwa wengi ukilingasha na wachache walio opt PHYSICS.
 
Deadbody umenichekesha sana na uandishi wako hasa ukizingatia nilikuwa nakumbuka matukio ya advance. Kwa kweli ile level ya elimu kwa masomo ya sayansi ni ngumu kupita hata masomo ya digrii ya kwanza (sijui kuhusu ya pili).
Old moshi hiyo,tulikuwa tunafundishwa na mwalimu (aka Pdiddy) ana sauti ndogo halafu ana aibu sana hivyo anaishia kusema na ubao tu. Mifano yake ubaoni mnaelewa vizuri tu sema sasa akiacha maswali unaona kama haukuwamo darasani vile.
Prep ya physics nikifanikiwa swali moja tu kutoka kwenye UP,siku imeisha maana nakuwa nimetumia si chini ya masaa 3-4 kupata ufumbuzi ukijumlisha na baridi la moshi ndio hamu ya kulalal inakuja haraka.
Nakumbuka tulikuwa na mshikaji wangu tukakubaliana kuuza godoro moja (tuwe tunatumia moja kwa zamu) ili kupunguza muda wa kulala ili fiziksi isitushinde lakini mwisho wa hakuna cha maana tulichopata.
Nadhani sitamshauri mwana familia wangu yeyote kusoma advance, ni kupoteza muda tu.
 
Deadbody umenichekesha sana na uandishi wako hasa ukizingatia nilikuwa nakumbuka matukio ya advance. Kwa kweli ile level ya elimu kwa masomo ya sayansi ni ngumu kupita hata masomo ya digrii ya kwanza (sijui kuhusu ya pili).
Old moshi hiyo,tulikuwa tunafundishwa na mwalimu (aka Pdiddy) ana sauti ndogo halafu ana aibu sana hivyo anaishia kusema na ubao tu. Mifano yake ubaoni mnaelewa vizuri tu sema sasa akiacha maswali unaona kama haukuwamo darasani vile.
Prep ya physics nikifanikiwa swali moja tu kutoka kwenye UP,siku imeisha maana nakuwa nimetumia si chini ya masaa 3-4 kupata ufumbuzi ukijumlisha na baridi la moshi ndio hamu ya kulalal inakuja haraka.
Nakumbuka tulikuwa na mshikaji wangu tukakubaliana kuuza godoro moja (tuwe tunatumia moja kwa zamu) ili kupunguza muda wa kulala ili fiziksi isitushinde lakini mwisho wa hakuna cha maana tulichopata.
Nadhani sitamshauri mwana familia wangu yeyote kusoma advance, ni kupoteza muda tu.

Advanced physics ni zaidi ya Bsc. kwa mwaka wa kwanza kozi zote za Engineering .Yale Ma-Newton's rings unaweza kwenda bank kuombea mkopo kama dhamana
 
physics_650x400_51489484821.jpg


5aeb30138efc5bd38c3a8aacd40cc677--projectile-motion-the-motion.jpg


Wakuu japo sijapost kwenye jukwaa hili kwa miezi kadhaa sasa hivyo naomba mnipokee tena mtaalamu Deadbody ,

Wakuu najua JF kuna watu wa kila aina ya masomo humu hivyo leo naomba niwakusanye watu wote waliosoma Advanced Physics tuje tukumbushie namna tulivyokuwa tunashangaa ndani ya chumba cha mtihani .

Ngoja nianze mimi aisee kuleta ushuhuda wangu wa kwanza kabisa:

Story inaanzia pale tu kijana Deadbody niliporipoti Advance school mara ya kwanza aisee ambapo nikapokewa kwa furaha sana na watu niliosoma nao Olevel na Primary.

Walinipokea kwa mbembwe sana maana balaa langu walikuwa wanalijua vizuri kuwa Physics na Maths niliumbiwa mimi(hahaha sipo serious hapa).

Nikapokelewa na kuonyeshwa Block nitakaloishi na maisha ya boarding ndio yakaanza rasmi .

TOPIC YA KWANZA KUFUNDISHWA KWA SOMO LA PHYSICS

Kama ilivyomazoea ya shule za advance kuwa walimu hukimbilia kuanza projectile motion,measurements and error hivyo ikawa hivyo hivyo kwa mwwalimu wetu ambaye alikimbilia kuanza na PROJECTILE MOTION.

ProjectileMotion.jpg


Dah aisee nilishangaa sana kuona topic hiyo ikifundishwa ndani ya siku moja na kuisha yote huku ikiwa na formula nyepesi mno kwa mwanafunzi kilaza kama Jesca kuelewa.

Formulas zilikuwa za Range ,height ambapo kila nikigusa swali kwenye kitabu cha CHAND linaenda natia tiki ,nikaanza kujiuliza kwanini watu wanasema hii topic ngumu mbona nimesolve maswali yote aiseeee..

Dah nikahitimisha tu kwa kujiona mimi ndio mwamba ,mwamba wa mathematics na sikwami kabisa swali la PROJECTILE MOTION .Wakati najitamba hivyo kumbe washikaji wananichora tu kuwa huyu dogo kaja kwa mbwembwe tumtazame kwanza ataishia wapi.

Projectile+motion.jpg


Mwendo ukawa ndio ule ule muhuni nikigusa tu maswali ya examples ya mwalimu napasua tena kwa muda mfupi tu.Na kwa jinsi nilivyokuwa na mbwembwe ilikuwa mtu akiniletea swali la projectile naliweka kwenye calculator lote then nikipiga alama ya sawa sawa kitu imooooo.Wenzangu wakawa wananiambia dogo fanya moja moja kupunguza brackets maana zitakuchanganya,ila kwakuwa nataka kuonyesha mimi ni kichwa sichanganywi nikawabishia na kuweka lote.

Aiseee nilikuwa mpenda sifa hatari enzi hizo kushinda hata BASHITE,nikasema likizo hii watanikoma mchikichini huko ndio nitakuwa nasolvia watu kwenye mabanda ya mihogo wakati wa kusubiri pindi .

Dah maisha yanaenda kasi sana na hatimaye nikapewa habari njema na mwanangu mmoja hivi kuwa kwa mgote jumamosi ni mtihani wa PROJECTILE MOTION hivyo nenda kawaonyeshe aisee kuwa wewe ni mwamba Dar nzima.Nikajawa na sifa kama kawaida yangu na kuwaza mda wote kuwa jumamosi inachelewa aisee nikafanye maajabu mchikichini huko.

SIKU YA MTIHANI WA PROJECTILE MOTION IKAFIKA

projectile_motion_prob_2.png


Kwa kujiamini kabisa nikakaa seat ya mbele kabisa maana nilikuwa sitaki mtu anichungulie tusije tukagongana marks tukawa wote wa kwanza wakati mimi nimetumia nguvu kubwa sana na nimekamia show.

Sitasahau hii siku hasa pale nilipoufungua mtihani wa PROJECTILE MOTION na kukutana na Concepts mpya ambazo sijawahi hata kuhisi kama nazo ni projectile aisee.

Kusoma swali hata halina terminologies ngumu kuelewa ila isipokuwa sina cha kuandika baada ya kulielewa lile swali.Hahahah formulas zangu za RANGE na Maximum height zote hazitumiki na ndio nazitegemea sasa hapo.

Ule mtihani na mimi tulikuwa level tofauti kabisa ambapo ni sawa na mwanafunzi wa darasa la kwanza aliyejifunza hesabu za kujumlisha namba zenye tarakimu moja then umtolee hesabu za magazijuto.

Ule mtihani haukuwa standard yangu japo majirani zangu wanaagiza karatasi za kujibia tu baada ya kujaza za mwanzo.Muhuni natamani nisikusanye niondoke hivyo hivyo ila sasa Mgote anayesimamia mtihani ndio kakaa mbele yangu kiasi kwamba hata nikigeuza jicho tu ananiona ,hhahah noma.

Nikakutana na concepts za kitu kina kuwa projected kutoka kwenye gari linaloenda kwa speed fulani na kitu chenyewe kina speed yake aiseee.Wakati huo air unaambia inaspeed yake then natakiwa kutafuta umbali kitakapotua kutokea umbali ambao gari lilikuwepo wakati wa kurushwa.

material-YTA5u3DP.png


Kila nikiangalia naona nashindwa hata kuchora mstari wa range maana kitu kilirushwa kikiwa kwenye height fulani above the ground.

Kiukweli hilo ndio baadae nikaja kugundua lilikuwa swali rahisi kuliko mengine.Hayo mengine ilikuwa balaaa tupu maana hadi ndege wa angani waliokuwa wanatembea walipishana na hiko kitu walichokiproject tena kwa speed tofauti.

Mfano swali lingine lilikuwa linaanzia mbali kinouma kuwa ,ball imeenza kuserereka kwenye umbo lina shape ya U na kuibuka juu na kuendelea na projectile motion na mara gafla ukagongana na body nyingine huko juu hivyo nitafute velocity waliyogongana nayo halafu unapasuka then kipande kimoja kinaondoka kwa speed yake na kingine kwa speed yake (data zingine ziliwekwa)

Hapo ndio Deadbody nikanza kushtuka kuwa hata ndege na hewa zinaweza kutumika kwenye projectile motion kumbe.

curv_proj_ep2.png


Aisee nilijiona mweupe sana kichwani na hakukuwa na uwezekano wa mimi kupata 1/100 ule mtihani.

Nikasema isiwe shida,maana kukusanya pepa nyeupe ni aibu acha nijitoe ufahamu nitafute range na maximum height ambazo hazijaulizwa nitapate pa kuondokea nyumbani.

Utaratibu ulikuwa simple sana ,yani ukifanya mtihani week hii,majibu yanatoka week ijayo na sikurudi tena huko mpka dk hii napoandika mada hii sijui ule nilipata A au B na sitaki kujua.

NIKAANZA MAISHA MAPYA



Kama principle ilivyokuwa ,ukiona umeshindwa kushinda nao basi ungana nao.Nikaanza kusoma Physics upya mchikichini na nikagundua nilikuwa sijui chochote aisee maana hata circular motion ingeniumbua.
Dah ngoja niishie hapa aisee maana mzuka ukipanda nitaanza kutoa matusi humu kuhusu Newton Rings (Wave 2 ) na madude ya mule..

NAJUA WATU KAMA MIMI WAPO WENGI HUMU,NAOMBA LEO TUJARIBU KUKUMBUSHIA HUYU MNYAMA 'PHYSICS'

KARIBUNI

cart.gif
Ungeweka na mwaka ulosoma a level ingekua poa sana,
 
Mimi nilisoma PCM. Rafiki wa dingi alikuwa mwalimu wa physics akaniambia ukitaka utoboe advance physics kuwa serious na practical ..niliufuata ushauri wake na nikatoboa
 
Back
Top Bottom