Afande Veronica yupo barabarani kukusanya hela au kufilisi Raia?

Afande Veronica yupo barabarani kukusanya hela au kufilisi Raia?

Kwenye zebra unatakiwa usimame bila kusimamishwa hata kama hamna mtu anaetaka kuvuka ukijiridhisha hamna mtu karibu ndo unaendelea na safari Kama hulijui hilo iko siku utapigwa faini kwa kupita kwenye zebra bila kusimama hata Kama hamna mtu ndo utashangaaa zaidi
Duh kazi ipo.
 
najua utaanza kusema tushajua una gari
basi nikuambie mie dereva tu nawaandesha WAHINDI mshahara 250000/=

haya turudi kwenye MADA kama sio dereva huwezi kujua adha ya TRAFFIC
anachosema ndio kipo na hiyo MICHEZO sio hapo tu ipo sehemu nyingi
Usione watu wajinga walipofurahia yule TRAFICC morocco aitel kuporomoshewa MITUSI ya nguoni na dreva daladala
hao jamaa ni wapuuzi AKILI zao zimejaa pesa zaidi kuliko kuongoza magari
Ninajiuliza sana swali hili- - Kwanini polisi wanapenda sana hela ? Kuna wengine wanapokea hata rushwa ya elfu moja toka kwa wapiga debe. Inanisikitisha.
 
Salaam Wakuu,

Polisi wana mbinu nyingi za kutengeneza mazingira ya Rushwa na kukupiga faini. Huwezi pona kwemye 18 zake.

Sitaki kusema Chuo cha Polisi Moshi (CCP) hawafundishi ila nadhani wanatakiwa kubadili Mitaala yao. Kuna vitu wanavifanya Polisi wetu hadi unajiuliza huko CCP walienda kusoma Ujinga? Polisi wanatakiwa watoe huduma sababu nu Watumishi wa Umma.

Rais Samia kaongeza Mshahara ili mfanye kazi kwa Tabasamu, sasa hasira za nini?

Mfano: Kuna askari pale Stesheni (maeneo ya Central/TRA (kwenye Zebra)) ana watu wake wa kukatiza zile zebra ili apige watu fine. Anaitwa WP 4548 CPL Veronica, ayafanyayo anakosea na kudhalilisha Jeshi letu.

Unaweza kuwapisha watu, atakaa hadi waishe, ukianza kuondoka ghafla utaona anaibuka mtu na kutaka kukatizazebra. Anafanya timing, Ukianza kuondoka anapita anakimbiwa na Vero anakupiga Mkono. Anakuwa na wenzake wawili. Unaulizwa Kwanini huheshimu watumiaji wengine wa barabara? Anakupiga fine.

Mimi ninahofu, wale jamaa wanatengenezwa? Kwanini wao tu ndo wakatize kwa kuchelewa siku zote?

Pili: Polisi wanatakiwa Wasimamishe Magari ili watu wavuke na wakishaisha wawaruhusu muondoke. Lakini wao wanasimama pembeni pale, Nyie madereva Mtajisimamisha wenyewe watu wavuke na wakishavuka mnajiruhusu wenyewe. Hapo ndipo kwenye mtego wa kuliwa hela.

Polisi tunaomba msaada wetu, mtusaidie muwapo kazini. Sababu Polisi kazi sio kupiga fine tu bali hata kutoa elimu ya barabarani kwa watumiaji wa barabara.

Polisi na Raia ni Ndugu, tushirikiane. Tusiishi kama paka na panya.

Kuwe na taa kuongoza Zebra crossing zote muhimu.

Hii itaondoa rushwa. Pia kuwe na camera ku-record kila kitu.

1654002907225.png
1654002961100.png
 
Iyo pesa una pewa risiti au mna yamaliza kimya kimya tuanzie apo kwanza
Inadaiwa wanaambiwa wakusanye kiasi fulani kwa siku la sivyo wanahamishwa wanapelekwa Nangurukuru. Je, faini ina uhalali? Nimesimama mwenyewe kupisha watu, wakiisha naondoka mwingine anaamua kupita anakimbia then unapigwa faini. Wewe kama Polisi kwanini hukusimamia watu kuvuka? Yeye anasimama pembeni ya barabara anaangalia tu. Lakini sababu pale Trafiki walipo kuna zebra, alitakiwa baada ya kuona watu wa kuvuka wamejaa, alitakiwa asimamishe magari watu wavuke then aruhusu magari. Sio Dreva wanajisimamisha wenyewe watu wanavuta, then akiondoka unamwambia apark pembeni kwamba Uliondoka watu hawajaisha. Dar wavuka barabara wanaisha?
 
Tumia Dash Cam DVR Camera.

Mimi popote wanaponisimamisha wanaiona Camera wanakwenda moja kwa moja kwenye point naomba leseni ya udereva, namwonyesha. Naomba kadi ya gari, nampatia alafu ananiambia nenda.
 
Acha majungu jomba hao watu hawana kazi ya kufanya mpaka wawekwe na polisi kuvuka zebra.
Hujiongezi kwamba nao wanapata cha Kwao hapo? Kazi gani zilizopo za kuwaingizia pesa kirahisi zaidi ya hiyo?
 
Kwenye zebra unatakiwa usimame bila kusimamishwa hata kama hamna mtu anaetaka kuvuka ukijiridhisha hamna mtu karibu ndo unaendelea na safari Kama hulijui hilo iko siku utapigwa faini kwa kupita kwenye zebra bila kusimama hata Kama hamna mtu ndo utashangaaa zaidi
Soma tena alichoandika.
 
Kwenye zebra unatakiwa usimame bila kusimamishwa hata kama hamna mtu anaetaka kuvuka ukijiridhisha hamna mtu karibu ndo unaendelea na safari Kama hulijui hilo iko siku utapigwa faini kwa kupita kwenye zebra bila kusimama hata Kama hamna mtu ndo utashangaaa zaidi
ujamuelewa. Anacho lalamikia ni kwann kila siku ni naru wale wale wanaochelewa kuvuka/wanaotaka kuvuka gari likitaka kuondoka?
 
majungu tu unaleta hapa.

kubeba jina zima la mtu anayekuhudumia eti una malalamiko naye ni uzwazwa.

watu watajuaje kama huna visa naye!!!
Hapa ameokoa wengi sana,siku yakikukuta utaelewa,hakuna watu wa hovyo kama askari wa barabarani........wapiga dili wengine pale Ubungo External
 
Kuna traffic wanakaa mbezi malamba mawili, kila siku asubuh wanachaji bajaji zote zinazopita njia ya malambamawili kwenda mbezi buku, nadaladala zote zinazoenda mbezi - temeke, mbezi- gmboto mbezi - kinyerezi zote zinachajiwa 2000,

Yaan nikisema zote namanisha zote zitakazofanya kazi kwasiku hiyo. Wanakaa kila siku zaweek saa 12 mpaka saa 5 asubuh
 
Back
Top Bottom