Afariki akiwa kwenye mfungo wa siku 30, aliahidi kufufuka Desemba 8

Afariki akiwa kwenye mfungo wa siku 30, aliahidi kufufuka Desemba 8

TheCrocodile

JF-Expert Member
Joined
May 31, 2021
Posts
1,199
Reaction score
3,307
Abdel Raphael (42) Mkazi wa Mtaa wa Uwanja halmashauri ya mji Geita amekutwa amefariki ndani kwake akiwa kwenye mfungo wa siku 30 akitarajia kufufuka Desemba 8.

Mmoja wa waumini waliokuwa wakishiriki ibada ya pamoja na marehemu ambaye alikuwa mchungaji wao anasema marehemu aliwaaminisha kuwa ifikapo Desemba 8 atafufuka lakini kufikia siku hiyo akawa amefariki na mwili wake kuharibika.

"Tulikuwa tumefunga tangu tarehe 28 mwezi wa 11 ilivyofika tarehe 2, kwenye chumba chake cha maombi kumcheki alikuwa mzima, tarehe 3 kwenda kumwangalia ile hali ilitutisha tukakuta ameanguka kitandani, yupo kifua wazi, yupo kwenye bukta, ikabidi tumkusanye miguu, tumuoshe vizuri. Tukamfunika mdomo, macho vizuri, tukamlaza vizuri, halafu tukaenda kutoa taarifa katika uongozi wa mtaa kwa ajili ya taratibu zinazofuata", amesema Jumanne Zuberi ambaye ni muumini mwenzake.

IMG-20221214-WA0067.jpg


Chanzo: East Africa Radio
 
Hivi mwanaume asipokula lazima afe baada ya siku ngapi?
Na mwanamke asipokula lazima afe baada ya siku ngapi?

Yaani walivyomkuta yupo hio ilibidi wampe chakula pale pale angeamka.

Wenzake ni wajanja walikuwa wakitoka kwenye maombi wanapiga msosi.

Biblia imesema tutafufuka siku ya mwisho sasa inakuwaje yeye afufuke trh 8 mbona leo trh 17?
 
Hivi mwanaume asipokila lazima afe baada ya siku ngapi?
Na mwanamke asipokula lazima afe baada ya siku ngapi?

Yaani walivyomkuta yupo hio ilibidi wampe chakula pale pale angeamka.

Wenzake ni wajanja walikuwa wakitoka kwenye maombi wanapiga msosi.

Biblia imesema tutafufuka siku ya mwisho sasa inakuwaje yeye afufuke trh 8 mbona leo trh 17?
Mwanamke ni siku saba ndo anaaga dunia kwa sababu mwili wake una matiti(maziwa)yanasaidia akae kwa huo muda/siku akiwa mzima bila kula[emoji2]

Mwanaume siku tano tu chali inakuwa kwa heri mwalim[emoji2]

Habari za asubuhi mpendwa luckyline
 
Mwanamke ni siku saba ndo anaaga dunia kwa sababu mwili wake una matiti(maziwa)yanasaidia akae kwa huo muda/siku akiwa mzima bila kula[emoji2]

Mwanaume siku tano tu chali

inakuwa kwa heri mwalim[emoji2]

Habari za asubuhi mpendwa luckyline

Sasa yule tunayeambiwa alikaa siku 40 bila kula wala Kunywa? Mambo ya Comic books, Iman hizi? Mimi naamini huyo ndio kifo kiliamua kumfika kwa njia hiyo, na niyo tarehe 8 aliyosema hakukosea ni kweli alifufuka lakini katika Roho, alichagua kuishi katika roho zaidi kuliko kupambana na matamko na madeni na matozo yasiyoeleweka kila siku
 
Mmoja wa waumini waliokuwa wakishiriki ibada ya pamoja na marehemu ambaye alikuwa mchungaji wao anasema marehemu aliwaaminisha kuwa ifikapo Desemba 8 atafufuka lakini kufikia siku hiyo akawa amefariki na mwili wake kuharibika.
Ataenda mbinguni moja kwa moja huyu
 
Mmoja wa waumini waliokuwa wakishiriki ibada ya pamoja na marehemu ambaye alikuwa mchungaji wao anasema marehemu aliwaaminisha kuwa ifikapo Desemba 8 atafufuka lakini kufikia siku hiyo akawa amefariki na mwili wake kuharibika.
Ataenda mbinguni moja kwa moja huyu
 
Mwanamke ni siku saba ndo anaaga dunia kwa sababu mwili wake una matiti(maziwa)yanasaidia akae kwa huo muda/siku akiwa mzima bila kula[emoji2]

Mwanaume siku tano tu chali inakuwa kwa heri mwalim[emoji2]

Habari za asubuhi mpendwa luckyline
Aiseee tule mbinguni hakuna hotel.

Mimi ninavyojua mtu akifunga si jion anafungua anakula? Ilikuwaje marehemu hakula hata kidogo?
 
Back
Top Bottom