Afghanistan: Taliban imesema ni marufuku mfanyakazi wa Serikali kutokuwa na Ndevu. Kama huna Ndevu usikanyage kazini

Afghanistan: Taliban imesema ni marufuku mfanyakazi wa Serikali kutokuwa na Ndevu. Kama huna Ndevu usikanyage kazini

Nchini Afghanistan, viongozi wa Taliban wamepiga marufuku wafanyakazi wa serikali ambao hawana ndevu kufika ofisini.

Taliban wanasema mfanyakazi yoyote wa serikali lazima awe na ndevu za kueleweka, hakuna kunyoa ndevu na wafanyakazi wote ambao hawana ndevu wamepewa muda kabla hawajafukuzwa kazi moja kwa moja.

Ni uchaguzi wako, ufuge ndevu ama ufukuzwe kazi😂


Ni jambo zuri sana, kufuga ndevu kwa ajili ya kufuata sunna ya Mtume wetu Muhammad S.A.W basi unapata thawabu, uislamu ni dini nyepesi sana na utekelezaji wake kuna mambo madogo madogo lakini faida kedekede
 
Hawa jamaa sijui hata wanaamini nini, mara wanawake wasisome mara sijui wasindikizwe wakisafiri yani dunia ina watu hii loh.
 
Hawa jamaa ndio maana watu walikimbia nchi siku wanachukua uongozi.. kesho utasikia hamna kupika sambusa zina pembe kama shetani.
Halafu mambo wanayoyafanya ni utashi wao binafsi tu,hata kwenye dini hayapo
 
kuna taratibu za kuondoa ushindani wa vitu nje ya kazi mf mavazi ya mauzo na ndio maana unaambiwa suruali ya kitambaa sio jeans ili kuepusha kuja na mavaz ambayo yatachukua attention ya watu na kupunguza efficiency ya kaz ila ndevu tunanyoa kwa sababu za usafi zaid wengi hawajui kuzitunza ndev , kuna mtu mpk zinanuka
Basi na WANAWAKE wanyoe Maana nao wengi vichwani wananuka
 
Sijui kwanini waislam wasikimbilie kuishi huko badala ya kujazana Ulaya Na marekani Kwa makafiri
 
Nchi zenye changamoto za hivyo hadi raha kuishi maana akili inafanya kazi ya ziada [emoji23][emoji23]

Nilikuwa Saudia unaona demu ila unajikaza kumwangalia
Nikaenda Iraq kila unakopita ni Usalama wa Taifa huwezi hata kukohoa
Baada ya vita ya Iran/Iraq ndio balaa zaidi waliporudi wajeda na kukuta wake zao wametaifishwa na mafarao aka Egyptians ila waliuwawa kama kuku

Sasa naenda kustaafu Tora Bora
 
Back
Top Bottom