Afrika ianze kugomea kupokea fedha toka Marekani ili ijitegemee

Afrika ianze kugomea kupokea fedha toka Marekani ili ijitegemee

1.Africa itapata wapi pesa za kulipa madeni inayodaiwa na Marekani?

2.Kwa nini Africa iache kupokea misaada kutoka Marekani?

3. China tayari inauza hadi toothpicks na Urembo Africa, Russia tayari inauza ngano,mbolea na AK47 kwa wingi Africa, Brazil inauza wigi za wanawake, Africa Kusini inatuuzia juice, India inatuuzia hadi dawa za maumivu na viongozi wengi wa Africa wanatibiwa huko. Unataka biashara gani zaidi kati Africa na BRICS?!

4. Nchi nyingi Africa zinauza mazao ya kilimo na rasilimali ghafi, unataka wauziane mahindi na madini kati yao?!

5. Unaposema teknolojia ya Marekani isitumike Africa unamaanisha pamoja na Internet, GPS, Ndege, Microsoft, Twitter, Facebook, WhatsApp, VISA?

6. Mitumba inaweza kuzuiwa ukiwa na "wajasiriamali" wengi kama Vunjabei na wengine wa Kariakoo wanaoweza kujaza soko la Africa na nguo za bei rahisi za Kichina

7. Miradi mingi ya Africa sasa hivi wanachukua mikopo kutoka China, huku ndiko kujitegemea unavyomaanisha??
Afrika walipe tu madeni wanayodaiwa sasa na Marekani kisha nchi zote ziache kupokea fedha na misaada toka Marekani. Afrika ianze kufanya biashara kati ya nchi na nchi ndani ya Afrika na nchi nyingine zile za BRICS na nyinginezo.

Afrika ili iendelee ihakikishe teknolojia yoyote toka Marekani haitumiwi Afrika na ile Mikataba ya kiulinzi na Marekani ivunjiliwe mbali na mikataba yote ya kibiashara isitishwe mara moja. Afrika izuie mitumba na bidhaa zinazoweza kupatikana kwingineko mbali na Marekani kuingia Afrika.

Afrika isimame imara dhidi ya Marekani ili ijitegemee!!
 
Nchi za Africa zitakuwa zinauziana nini na hiyo sarafu yake?? Tanzania itauziana nini na Malawi au Zambia na sarafu yake?
Africa ifikirie kutumia sarafu yake kwanza ili ijikomboe kutoka kwenye dola. Tukiliweza hilo tutakua mbali.
 
Mbulaa tuache kutembeza bakuli kwa Taifa Teule la Mungu , Nasema baada ya Mungu anafuatiwa USA hayo mataifa mengine ni upuuzi tuu , kama sio Taifa The great National USA ungekuta tumeshatawaliwa na SHARIA
cheki nae huyu anavyoropoka nikajua hata ana point
 
Afrika walipe tu madeni wanayodaiwa sasa na Marekani kisha nchi zote ziache kupokea fedha na misaada toka Marekani. Afrika ianze kufanya biashara kati ya nchi na nchi ndani ya Afrika na nchi nyingine zile za BRICS na nyinginezo.

Afrika ili iendelee ihakikishe teknolojia yoyote toka Marekani haitumiwi Afrika na ile Mikataba ya kiulinzi na Marekani ivunjiliwe mbali na mikataba yote ya kibiashara isitishwe mara moja. Afrika izuie mitumba na bidhaa zinazoweza kupatikana kwingineko mbali na Marekani kuingia Afrika.

Afrika isimame imara dhidi ya Marekani ili ijitegemee!!
Afrika haiwezi kuendelea bila ku invest kwenye defense kwanza. Unaanza kutengeneza nyuklia ilikuwazuia kurudi kututawala sababu make no mistake, resources zikipungua watarudi kuchukua kwa nguvu.
 
Kwa hizi siasa za ccm&chadema? Hilo sahau labda wapatikane viongoz nje ya haya mavyama ambayo kimsingi yanaendeshwa kwa misingi ya hao hao wamarekan.

Ni vigumu kuwakwepa hao mabwana kama akili yako inafungamana na agenda zao za kisiasa.
 
Mawazo ya mtu mpumbavu

Hao BRICS hawajawahi isaidia Tanzania chochote cha bure tukiondoa TAZARA
Hujielewi wewe,unajipinga wewe mwenyewe,umeonyesha jinsi ulivyo na uwezo mdogo wa kufikiri,unasema "Hawajawahi isaidia chochote cha bure tukiondoa TAZARA"

Hiyo Tazara inaingiaje hapo na wewe umeshatumia neno "Hawajaisaidia chochote?"

Sio kila thd lazima uonyeshe ujinga wako,piga kimya ili usijulikane kua wewe ni hamnazo.
 
Hivi nani aliwaambia BRICS wanataka kujitenga na USA na EU kiuchumi na kibiashara?

Naona hili jambo watu wanalichukulia kiushabiki sana. Huo ni muungano tu hawana hata mpango wa kujitenga na mataifa mengine

Kila siku tunaona nchi wanachama wa BRICS kama China na India zinaingia mikataba ya kibiashara na mataifa ya Ulaya na Marekani. Halafu leo hii mtu aseme Afrika ijitenge na Marekani ifanye biashara na BRICS tu
 
Nchi za Africa zitakuwa zinauziana nini na hiyo sarafu yake?? Tanzania itauziana nini na Malawi au Zambia na sarafu yake?
Mkuu, usitake kuniaminisha hujui biashara zinazofanyika Kati ya mataifa ya Africa.. Angalia mfano mdogo wa Zambia, tangu isimimie sarafu yake imekua namba 10 kwenye sarafu zenye nguvu Africa.

Kitu gani kitashindwa Africa kufanya biashara kwa Sarafu Yao.? Uoga wetu na kuamini dola ndio kila kitu unatufanya tegemezi na utaendelea kua hivyo na kama Kuna threat kubwa kwa nchi za Magharibi ni endapo siku Africa itatumia sarafu moja.
 
Ni vyema tupunguze ndoto za mchana, kabla ya kuanza kufikiria sarafu moja ya Africa tufukirie kwanza sarafu moja ya Jumuiya ya Africa Mashariki au SADC. Huku tu katika hizi jumuiya ndogo imeshindikana halafu tunaota sarafu moja ya Africa.
Mkuu, usitake kuniaminisha hujui biashara zinazofanyika Kati ya mataifa ya Africa.. Angalia mfano mdogo wa Zambia, tangu isimimie sarafu yake imekua namba 10 kwenye sarafu zenye nguvu Africa.

Kitu gani kitashindwa Africa kufanya biashara kwa Sarafu Yao.? Uoga wetu na kuamini dola ndio kila kitu unatufanya tegemezi na utaendelea kua hivyo na kama Kuna threat kubwa kwa nchi za Magharibi ni endapo siku Africa itatumia sarafu moja.
 
Sekta ya afya Tz ikikosa misaada toka mashirika ya misaada kama USAID, mwaka mmoja inacollapse.
Watu hawalijui hilo!, Shida kubwa ya watanzania ni kukosa taarifa , ndo maana huwa tunaropoka tu, huyu anasema tususie Usa products, ilhali yeye mwenyewe anatumia , internet, android , Google, Visa au MasterCard na pengine hata Iphone kutoka kwa shoga Tim cook.
 
Kwa ufupi tu ile ziara ya Kamala ilikua na malengo ya kujaribu kufuta ushawishi wa China hapa Afrika.

Tanzania ilichaguliwa kwakua ni moja wapo ya maeneo ya kimkakati kiuchumi na kiulinzi hapa eneo la maziwa makuu.

Mawakala wa mabeberu yapo hapa nchini kuangalia fursa na namna ya kushindana na influence ya mchina.

Kiufupi tu Marekani anapambana sana kurejesha influence yake duniani baada ya tishio la mchina.
 
Moja ya nchi za Brics ni South Africa ambayo ina shida kama tanzania Tu.


Sasa Tanzania itapeleka nini South Africa ambayo Kwa mwaka sasa Wana mgao WA umeme ambao tanzania haijawahi kuwa nao.
 
Na tazara si msaada ule, mchina aliilenga Shaba ya Zambia!
Wachina hawana msaada wowote Africa , ni vile tu wa africa wenyewe tupo slow minded kung'amua mambo. Nigeria kuna taarifa ya wizi wa mabilion ya pesa za mafuta suspect mkuu ni china company.

China want this continent with its fertile land and rich minerals, but they dont it with us in it. Kule kwao wameshajaza na hakuna kitu chini.
 
Back
Top Bottom