Johannesburg, Afrika Kusini. Rais John Magufuli ametunukiwa tuzo ya amani ya Mandela (Mandela Peace Prize) kwa kuendeleza shughuli ya kulinda amani na kupigania usawa wa kijamii.
Kamati ya tuzo za Mandela kwa mwaka 2017 ilipokea maombi ya wawania tuzo 4,956. Wengine waliotunukiwa ni Rais Uhuru Kenyatta aliyeshinda tuzo ya Mandela ya Demokrasia kutokana na kuendeleza demokrasia nchini Kenya.
Pia, Mahakama ya Juu nchini Kenya na Jeshi la Zimbabwe zimetunukiwa tuzo ya ujasiri (Mandela Boldness) kwa kufanya uamuzi kwa kijasiri kwa masilahi ya mataifa yao.
Rais wa Taasisi ya Mandela, Dk Paul Kananura amesema Rais Kenyatta ametunukiwa kwa kudhihirisha demokrasia kwa kukubali uamuzi wa Mahakama ya Juu hivyo kuheshimu kanuni za utengano wa mamlaka. Mahakama ya Juu ya Kenya ilibatilisha matokeo ya urais katika uchaguzi wa Agosti 8,2017 yaliyompa ushindi Kenyatta na kuamuru uchaguzi kurudiwa ambao alishiriki na kuibuka mshindi.
"Hii inaonyesha kuwa Rais Kenyatta amechangia katika uimarishaji wa demokrasia Kenya,” amesema Dk Kananura. Rais wa Chad, Idriss Itno amepata tuzo ya Mandela ya Ulinzi (Mandela Security) kutokana na sera ya kupambana na ugaidi katika maeneo ya Sahel na Ziwa Chad. Mwingine ni Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza aliyetuzwa tuzo ya ujasiri (Mandela Courage).
Tuzo amepewa mpaka Nkurunziza?Hivi Tundu Lissu hajapewa tuzo huko? Naombeni jibu nyie makarai wa Ufipa
Kwa sababu mtu anayekukosha roho yako hayumo.Tuzo nyingi zinazotolewa hapa duniani kuanzia zile za Nobel, Mo hata hizi ukiangalia kwa jicho la tatu ni za kinafiki kupindukia .
Si kwa Nkrunzinza tu walipoharibu, au pengine unaogopa kupataja?Hapo kwa Nkrunzinza ndiyo wameharibu kabisa
Hii hatari sana mkuuMzungu aliposema ' Africa is a Dark Continent' hakukosea
South Africa wamemdhalilisha Nelson Mandela
Shame on You South Africa
All in all we as Tanzanians tunaujua ukweli
Mtu mwenye tetesi za kunanihiiii leo mnampongeza???
Ukiona uzi unaomtaja Magufuli siku hizi lazima udode maana watu wamemchoka ile mbaya!Inaonekana ni HABARI KUBWAAAAAAAAAAA....lakini hadi nashiriki kutoa maoni ndiyo kwanza ina page tatu, hapo ina masaa mawili tangu iwe posted. Wakati habari ya Tundu Lissu kuanza mazoezi jana, ndani ya nusu saa iliweza kujaza zaidi ya kurasa tatu. Mjipime aisee.
Si alipewa na baba ubaya ya kummiminia risasi?Hivi Tundu Lissu hajapewa tuzo huko? Naombeni jibu nyie makarai wa Ufipa
Nice
Johannesburg, Afrika Kusini. Rais John Magufuli ametunukiwa tuzo ya amani ya Mandela (Mandela Peace Prize) kwa kuendeleza shughuli ya kulinda amani na kupigania usawa wa kijamii.
Kamati ya tuzo za Mandela kwa mwaka 2017 ilipokea maombi ya wawania tuzo 4,956. Wengine waliotunukiwa ni Rais Uhuru Kenyatta aliyeshinda tuzo ya Mandela ya Demokrasia kutokana na kuendeleza demokrasia nchini Kenya.
Pia, Mahakama ya Juu nchini Kenya na Jeshi la Zimbabwe zimetunukiwa tuzo ya ujasiri (Mandela Boldness) kwa kufanya uamuzi kwa kijasiri kwa masilahi ya mataifa yao.
Rais wa Taasisi ya Mandela, Dk Paul Kananura amesema Rais Kenyatta ametunukiwa kwa kudhihirisha demokrasia kwa kukubali uamuzi wa Mahakama ya Juu hivyo kuheshimu kanuni za utengano wa mamlaka. Mahakama ya Juu ya Kenya ilibatilisha matokeo ya urais katika uchaguzi wa Agosti 8,2017 yaliyompa ushindi Kenyatta na kuamuru uchaguzi kurudiwa ambao alishiriki na kuibuka mshindi.
"Hii inaonyesha kuwa Rais Kenyatta amechangia katika uimarishaji wa demokrasia Kenya,” amesema Dk Kananura. Rais wa Chad, Idriss Itno amepata tuzo ya Mandela ya Ulinzi (Mandela Security) kutokana na sera ya kupambana na ugaidi katika maeneo ya Sahel na Ziwa Chad. Mwingine ni Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza aliyetuzwa tuzo ya ujasiri (Mandela Courage).