Afrika ndiyo kinara wa kufanya kazi ngumu lakini kisukari ni tishio je kazi ngumu sio mbadala wa mazoezi?

Sema vyakula vya wanga mkuu. Sisi tunatumia sana nafaka zenye carbohydrates sana kama mahindi na mchele na ngano. Hili lina mchango mkubwa sana kwenye gonjwa la sukari.
Mbona wazungu wanakula mikate na tambi sana,sio wanga huo?
 
Sukari ina uhusiano mkubwa sana na upofu pamoja na urijali,
Huwa inaua mishipa midogo ya damu na moja ya mishipa hiyo ni ilie inayosimamisha uume pamoja na macho
Shukrani chiefπŸ‘Š
 
Ukifanya mazoezini au kazi ngumu unaunguza au kutumia sukari nyingi kama energy.
Ukiwa unakula tu na haufanyi mazoezini hii sukari inalundikana mwilini na ndo hiyo huleta ugonjwa
Bush dokta kwa msaada ya gugo
Asante sana bush dokta from gugo univasiti. Maelezo yanaeleweka πŸ˜…
 
Asante sana bush dokta from gugo univasiti. Maelezo yanaeleweka πŸ˜…
Ogopa sana sukari ikishafikia kwenye kuleta ukhanithi!!!
Mzigo unaona kabisa huu hapa!! Halafu chombo haisimami!!! yani kama hakuna kilichotokea πŸ™‚ unaeza kulia!!
 
Umeongelea upande mmoja ukaacha mwingine, ni kweli insulin inatumika ku regulate glucose, lakini inategemea wingi wa glucose, ulaji mbaya wa chakula husababisa glucose kuwa nyingi kuliko uwezo wa insulin, (insulin resistance,) na hapa ndo tatizo la sukari huanzia. Na ndio hiyo. Huitwa type 2 diabetes, insulin inakuwepo lakini inakuwa imezidiwa na wingi wa glucose.
ha
 
Nchi Ina watu milioni 55! Unapima watu 200 wa mjini! Unasema kisukari kinatisha bongo!
 
Sukari inayosababishwa na hitilafu ya kongosho siyo maarufu sana huku kwetu, (type 1) huwa inatokeaga tu kongosho haitoi insulin au ikazidisha insulin, type 1 diabetes sio lifestyle disease! Ni ugonjwa sana sana wa kurithi( genetic)
Inayosumbua sasa Africa ni type 2 diabetes hii sasa ni lifestyle disease.. Kongosho inatoa insulin ila sukari inakuwa nyingi mwilini kuliko dose ya insulin.
 
Hili la kusema Afrika watu ndiyo hufanya kazi ngumu zaidi una uhakika nalo? Siyo kama zile zile story za kusema wanaokula ugali ndiyo wenye nguvu na wazungu ni legelege? Mimi nadhani Afrika ndiyo yenye watu wavivu zaidi. Kama umewahi kufika Ulaya au nchi yoyote iliyoendelea nadhani utakubaliana na mimi wanafanya kazi mara kumi kuliko sisi. Huku kwetu kazi ngumu wanafanya watu wa vijijini ambako hakuna vyakula na huduma za afya za kutosha. Mjini watu wanaishi maisha ya hatari sana. Wengi kila siku jioni wanakwenda bar kunywa na kula na maofisini hata kukoroga chai wanafanyiwa.
 
Nakumbuka Mzee wangu katika ukuaji wangu alikuwa ananizuia kunywa maji huku nakula kuwa italeta kisukari sikuwa na uhakika ila ilikuwa fact sana kwangu katika digestion system
 
Ila sio saidia fundi mkuu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Utakimbua kimbia kwa kitumwa hafi ukome. Leta kipande cha tofali,...... sio hichoo leta kitofalii,....... Oya huyu dogo mmemtoa wapi hajui kitofa πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Mostly vyakula tunakula na kunywa ni hormonal suppressor so unaweza ukafanya mazoezi but hormones sio balanced hapo sasa sukari inaingia
 
Comments za washauri wengi ni kama hawana mtindo mbaya wa maisha. Kitu ambacho si kweli.

Magonjwa mengine yapo kwenye vinasaba, magonjwa hayo huwa yanasubiri visababishi tu.

Wengine tunakunywa pombe monday to sunday, usizungumzie mitoko official ya weekend ambapo mtakunywa hadi asubuhi.
Vyakula ni ugali, nyama choma, wali, tunakunywa sana soda na tukichelewa kula chips na juice au soda inahusika.

Haya mambo wakati mwingine ni Mungu tu lakini pia familia unayotokea, ninavyoona kama mzazi wako alishakuwa na kisukari ni vyema kujiangalia hasa katika ulaji.


Kubadili lifestyle inataka moyo sana na kujitoa lakini hamna namna.

Wanga ndio maisha yetu, familia ina watoto 8, baba kajitafuta uwezo wake ni kununua unga wa mahindi watoto wale ndicho chakula bei nafuu.

Umasikini na kisukari vinapendana sana.

Chanzo cha rate kubwa ya kisukari ni umasikini hakuna lingine.
 
Kazi ngumu sio mazoezi

Tusingekuwa tunaambiwa punguza kufanya kazi ngumu ila fanya mazoezi
 
Nadhani mazoezi ni ziada,mfumo wa chakula ukoje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…