Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Mmesikia huko 😂
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, ametumia ukurasa wake wa Instagram kuelezea kuhusu mchezaji wao, Yusuph Kagoma, na uvumi unaozunguka hatma yake.
Ahmed Ally ameandika:
"Klabu yenu inampenda sana Yusuph Kagoma, yaani kila mkilala mnamuota. Roho zinawauma kumkosa na mngetamani aje kwenu. Lakini cha kufanya kwa sasa ni kuwa na subira".
"Kwa sasa Kagoma ana umri wa miaka 23, na kwa uwezo wa Mungu (Insha Allah) atabaki Simba kwa miaka zaidi ya 10. Akiwa na miaka 33 au 35, hapo ndipo atakapokuja kwenu".
"Mfumo ni ule ule kama mlivyosubiri mchezaji kutoka Zambia kwa miaka 7 au mchezaji namba 20 kwa miaka 15. Hivyo Kagoma naye ni mali halali ya Simba kwa sasa."
Ahmed Ally amesisitiza kuwa Kagoma kwa sasa ni mchezaji wa Simba na mashabiki wa klabu nyingine wanatakiwa kuwa na subira, kwani nyota huyo bado ana muda mrefu ndani ya Simba SC.
Soma pia;
=> Sakata la Yusuph Kagoma kusaini timu mbili Klabu ya Simba kukatwa alama
=> Mwigulu awaomba viongozi wa Yanga wapotezee suala la Kagoma ili aweze kucheza Simba
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, ametumia ukurasa wake wa Instagram kuelezea kuhusu mchezaji wao, Yusuph Kagoma, na uvumi unaozunguka hatma yake.
"Mfumo ni ule ule kama mlivyosubiri mchezaji kutoka Zambia kwa miaka 7 au mchezaji namba 20 kwa miaka 15. Hivyo Kagoma naye ni mali halali ya Simba kwa sasa."
Ahmed Ally amesisitiza kuwa Kagoma kwa sasa ni mchezaji wa Simba na mashabiki wa klabu nyingine wanatakiwa kuwa na subira, kwani nyota huyo bado ana muda mrefu ndani ya Simba SC.
Soma pia;
=> Sakata la Yusuph Kagoma kusaini timu mbili Klabu ya Simba kukatwa alama
=> Mwigulu awaomba viongozi wa Yanga wapotezee suala la Kagoma ili aweze kucheza Simba