Ahsante Rais Samia, hatimaye HESLB wafuta VRF kwenye system yao

Ahsante Rais Samia, hatimaye HESLB wafuta VRF kwenye system yao

Swala la kulinda thamani ya pesa lilitakiwa kuachwa na cha msingi ingepunguzwa asilimia........ yani ukope leo laki halafu baada ya miaka kumi ulipe laki hiyo hiyo? aiseee

Kwanini mshahara haupandi asilimia 6 kila mwaka kulinda dhamani ya fedha. Yaani mkataba nimesaini 2015 mpaka leo nalipwa hela hiyo hiyo!!
 
Kama tunavyojua, kwa mujiba wa katiba yetu Mheshimiwa Rais halazimiki kufuata ushauri wa mtu yeyote yule.

Hivyo basi tunapokuwa na rais msikivu tena anayefanyia kazi maoni na malalamiko ya watu wake ni baraka kubwa kwa taifa

Kwasasa ukiangalia statement ya deni lako kwenye mfumo wa bodi ya mikopo ( olas.heslb.go.tz ) utaona kuwa wameondoa tozo zote za VRF, yaani hata zile walizotoza zamani (kabla ya agizo la rais) wameziondoa

Wanufaika wa mikopo tunamshukuru sana Mheshimiwa rais kwa kusikia na kuyafanyia kazi maombi yetu. Tulilalamika sana wakati wa mwendazake lakini tukajibiwa kuwa 'hapangiwi'.

Sasa ni muda wa kila mnufaika mwenye uwezo wa kulipa na alipe, tena wamerahisisha unaweza kulipa hata kwa m-pesa na malipo yako yanaonekana hapohapo kwenye mfumo.

Pia niwakumbushe wadau, twendeni vizuri na mama, naiona katiba mpya hususani wakati wa ungwe yake ya pili Mungu akimjaalia na wananchi wakampa ridhaa.
Hakuna kitu hicho mleta mada unatuchora
 
Sorry mkuu naomba nieleweshe. Miaka labda kumi iliyopita ada yangu chuo ililipwa milioni 5. Unataka kusema kwa sasa hivi hata kesho nikienda na million 5 na clear deni bila usumbuf wowote. Au itaongezeka haitakua ile ile million 5 exactly? mwarobaini
Kwa chuo nilichosoma mimi, YES. Ada haijabadilika kabisa, ni ileile.
 
Swala la kulinda thamani ya pesa lilitakiwa kuachwa na cha msingi ingepunguzwa asilimia........ yani ukope leo laki halafu baada ya miaka kumi ulipe laki hiyo hiyo? aiseee
Shetani wa kike wewe.
Shwain!
Hurreee Mama Samia💪
 
Kama tunavyojua, kwa mujiba wa katiba yetu Mheshimiwa Rais halazimiki kufuata ushauri wa mtu yeyote yule.

Hivyo basi tunapokuwa na rais msikivu tena anayefanyia kazi maoni na malalamiko ya watu wake ni baraka kubwa kwa taifa

Kwa sasa ukiangalia statement ya deni lako kwenye mfumo wa bodi ya mikopo (olas.heslb.go.tz ) utaona kuwa wameondoa tozo zote za VRF, yaani hata zile walizotoza zamani (kabla ya agizo la rais) wameziondoa

Wanufaika wa mikopo tunamshukuru sana Mheshimiwa rais kwa kusikia na kuyafanyia kazi maombi yetu. Tulilalamika sana wakati wa mwendazake lakini tukajibiwa kuwa 'hapangiwi'.

Sasa ni muda wa kila mnufaika mwenye uwezo wa kulipa na alipe, tena wamerahisisha unaweza kulipa hata kwa M-pesa na malipo yako yanaonekana hapohapo kwenye mfumo.

Pia niwakumbushe wadau, twendeni vizuri na mama, naiona katiba mpya hususani wakati wa ungwe yake ya pili Mungu akimjaalia na wananchi wakampa ridhaa.
Swali kama wameondoa hiyo tozo tafsiri yake ni kwamba haikuwa halali, je Yale Makato uliyokatwa kinyume na makubaliano utarudishiwa au yanaingia kwenye kupunguza deni? Au ndo unafunika kombe mwanaharamu apite.
 
Ok mkuu umesema kwenye slip ipo vilevile ila kwenye chungu cha bodi ya mikopo inasomeka kivingine.

Sasa huoni ya kwamba utaendelea kutumikia deni linalo onekana kwenye slip kwasababu ndilo linalo tambulika na hazina?
Hapana, la bodi likiisha nakweda kuchukua barua inayoonesha nimemaliza deni, kisha naipeleka kwa afisa utumishi ambaye atasitisha makato kutoka kwenye mshahara.

Na ikitokea mchakato umechelewa wakanikata zaidi, upo utaratibu wa kurudishiwa pesa yako kutoka bodi.
 
Hapana, la bodi likiisha nakweda kuchukua barua inayoonesha nimemaliza deni, kisha naipeleka kwa afisa utumishi ambaye atasitisha makato kutoka kwenye mshahara.

Na ikitokea mchakato umechelewa wakanikata zaidi, upo utaratibu wa kurudishiwa pesa yako kutoka bodi.
Ushauri ni vyema bod ya mikopo kama kweli imepunguza kwa namna hiyo wawasiliane na ofisi za utumishi watume majina na kiasi cha madeni cha wanaokatwa
 
Lengo la mikopo kwa wanafunzi sio bishara yenye kuhitaji kuwekewa tozo ya kulinda thamani ya deni. Kumbuka serikali inawajibu wa moja kwa moja kutoa huduma ya elimu, haya kuchangia kwa njia ya kupewa mkopo ni baada ya kuingia viongozi wenye mawazo ya ulafi kama wewe. Hizi ni kodi za wananchi na hivyo si wajibu wa serikali kuzifanyia biashara zaidi ya kutoa huduma.
Swala la kulinda thamani ya pesa lilitakiwa kuachwa na cha msingi ingepunguzwa asilimia........ yani ukope leo laki halafu baada ya miaka kumi ulipe laki hiyo hiyo? aiseee
 
Sawa lkn awaambie hao watu wa bodi kuwa mkopo ni haki wa kila raia.Kusema kisa umesomesha mtt wako shule ya kulipia unyimwe mkopo si saw.
kabisa aisee.
mfano mimi watoto wangu walisoma shule za msingi za serikali, maarufu kama kayumba, O level nikawapeleka shule za private, A level wakasoma shule za serikali, walivyochaguliwa vyuo vikuu hawakupewa mkopo na bodi, ikabidi kuingia tu gharama maana hakuna jinsi hasa ukichukulia sisi watumishi wa serikali tuliopigwa "ribiti" kwa miaka mitano unabaki kushangaa tu, haya jamaa si wangempa hata mmoja tu ili kunipunguzia kamzigo kidogo.
 
Back
Top Bottom