Ahsante Rais Samia, hatimaye HESLB wafuta VRF kwenye system yao

Ahsante Rais Samia, hatimaye HESLB wafuta VRF kwenye system yao

Mzalendo Uchwara

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2020
Posts
4,437
Reaction score
13,836
Kama tunavyojua, kwa mujiba wa katiba yetu Mheshimiwa Rais halazimiki kufuata ushauri wa mtu yeyote yule.

Hivyo basi tunapokuwa na rais msikivu tena anayefanyia kazi maoni na malalamiko ya watu wake ni baraka kubwa kwa taifa

Kwa sasa ukiangalia statement ya deni lako kwenye mfumo wa bodi ya mikopo (olas.heslb.go.tz ) utaona kuwa wameondoa tozo zote za VRF, yaani hata zile walizotoza zamani (kabla ya agizo la rais) wameziondoa

Wanufaika wa mikopo tunamshukuru sana Mheshimiwa rais kwa kusikia na kuyafanyia kazi maombi yetu. Tulilalamika sana wakati wa mwendazake lakini tukajibiwa kuwa 'hapangiwi'.

Sasa ni muda wa kila mnufaika mwenye uwezo wa kulipa na alipe, tena wamerahisisha unaweza kulipa hata kwa M-pesa na malipo yako yanaonekana hapohapo kwenye mfumo.

Pia niwakumbushe wadau, twendeni vizuri na mama, naiona katiba mpya hususani wakati wa ungwe yake ya pili Mungu akimjaalia na wananchi wakampa ridhaa.

---- update----
Wadau wengi wameuliza namna ya kuangalia, naamini bodi watatoa maelekezo zaidi lakini kwa hapo ngoja nieleze kwa ufupi.

Ingia kwenye website

Screenshot_20210626-154438~2.png



Kwenye dashboard (juu kushoto) chagua loan repayment
Screenshot_20210626-154608~2.png


Kisha baada ya apo, chagua beneficiary/lonee/ employee login

Screenshot_20210626-154639~2.png


Baada ya hapo ingiza namba yako ya form four kwa format inayo onekana

Screenshot_20210626-154819.png


System itaiangalia namba hiyo kwenye database ya bodi na kukuketea jina lako mnufaika.

Baada ya hapo utathibitisha kuwa ni jina lako kweli kwa ku click hilo jina.

Baada ya hapo utajaza taarifa muhimu kama namba ya simu, email na taarifa za mwajiri pamoja na kutengeneza password.

Ukikamilisha utakua umeshatengeneza account kwenye mfumo wao

Baada ya hapo uta log in as registered user na utaona taarifa zako zote za deni lako. Pia utaona control namba unayoweza kuitumia kulipa mwenyewe.

Natumaini inaeleweka.
NB sijaweka picha za hatua za mwisho kwakua zinaonesha taarifa binafsi za mnufaika.
 
Swala la kulinda thamani ya pesa lilitakiwa kuachwa na cha msingi ingepunguzwa asilimia........ yani ukope leo laki halafu baada ya miaka kumi ulipe laki hiyo hiyo? aiseee
Sio kweli, kila mtu angekuwa anapandisha tozo ya 6% or less kila mwaka kwa kisingizio cha 'kulinda thamani ya fedha' maisha yangekuwa magumu sana.

Wakati nasoma chuo ada ilikua 1,500,000 kwa mwaka. Leo hii miaka karibu kumi mbele ada ni ileile 1,500,000 na ndiyo mnufaika mpya analipiwa hiyo na bodi.

Sasa kwanini bodi itake mimi nirudishe 1,700,000 wakati kiasi anachopewa mwanafunzi mpya ni kilekile nilichopewa mimi miaka kumi iliyopita?

Plus, HESLB haikuanzishwa kufanya biashara.
 
Swala la kulinda thamani ya pesa lilitakiwa kuachwa na cha msingi ingepunguzwa asilimia........ yani ukope leo laki halafu baada ya miaka kumi ulipe laki hiyo hiyo? aiseee
Kwani Serikali inafanya biashara? Na vip kama thamani ya hela itakua imepanda, watakupunguzia deni? Una roho yakishetani ww sio bure. mungu fake wenu kafa huko sasa kila kitu kinabadilika.
 
Swala la kulinda thamani ya pesa lilitakiwa kuachwa na cha msingi ingepunguzwa asilimia, yani ukope leo laki halafu baada ya miaka kumi ulipe laki hiyo hiyo? aiseee
kwa hiyo Bodi wanafanya biashara tena yenye faida sio?Basi walipe kodi Mana hiyo ni biashara!kama wanataka thamani wakatie bima mikopo kama wafanyavjo benki walau 0.5 ya mkopo wanapo mpa mwanafunzi.

Sent from my Nokia 2.4 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom