Q-net muda huu saa nne na robo usiku huu wanasalimiana Good morning kwa vidole viwili, kuna jirani yangu nimeshuhudia kwa macho yangu alienda mpaka benk kukopa 5M akawapelekea, alinishawishi nikamwangaliaaaaa.... hahaaaa, nikamwambia ahsante sana, siku hizi aniongeleshi, eti anashindia huko ofisini kwao mpaka saa nne usiku.
mara wameaidiwa Iphone mara Toyota, kuna Mama mmoja n mstaafu alishapeleka 5M kwa hao jamaa sasa hivi anazunguka eti kutafuta partners wengine, basi nilimkuta anamshawishi mzee mmoja hivi ninaemfaham kabisa. Pale pale nikamchana live yule Mama akaniambia we kijana hujui kitu, nikamwambia sawa Mama kama sijui kitu mbona tokea uweke hiyo 5M umekuwa ni mtu wa kuzunguka tu hutulii kwako mwishowe upate maradhi bure, hujatajirika na hiyo Toyota na Iphone mbona hawajakupa eti si ndo nipo natafta Partner ili akaunti yake ijae,
Nikaendelea kumwambia kwamba hakuna pesa zinazokuja kwa haraka hivyo isitoshe wewe umeishastaafu hukutakiwa kuanza kuzunguka na kuhangaika hivi mara huku mara kule eti unatafta Partner wa Q-net, halafu hao Q-net wanakmwabia wanafahamika mpaka Serikalini wanakuonyesha picha walizopiga na viongozi wa Serikalini, mimi nilimuambia huyu aliyetaka kunishawishi kwamba picha zina-editiwa ndugu kuwa makini, nimeona mengi mpaka watumishi ninao wafaham wamecha kazi nao wanaangaika kutafuta Partners.. inahuzunisha sana Serikali inabidi iangilie kwa jicho pana zaidi kuhusu hawa Q-net et all.
Sent from Nokia 7 Plus