Aina za Limbwata Wanawake wanazotumia kutushika, je we umepewa mojawapo hapa. Ni uchafu mtupu

Aina za Limbwata Wanawake wanazotumia kutushika, je we umepewa mojawapo hapa. Ni uchafu mtupu

Vipi ameshatoka kifungoni?
Uko sahihi kabisa..

Mimi bro wangu alifanyiwa hiyo ya nyama, aliteseka sana. Kwanza aliichukia kazi akawa hataki kwenda kazini anataka abaki na mkewe nyumbani. Akiwa nyumbani anazima simu kabisa hapatikani hata siku tatu. Kazini haendi kazi yake kukaa nyumbani.

Mke sasa ndo anakuwa mume, yeye kutwa kiguu na njia na asiulizwe unaenda wapi. Bro anabaki kuhudumia watoto, awapikie, awaogeshe afue nguo, asafishe nyumba...

Siku akienda kazini akirudi msosi hakuna anaambiwa "nimechoka kupika kama vp kapike mwenyewe" hapo hela ameacha asbh. Bas bro anakuwa mpole tu anaenda kununua viepe alalie. Sina hakika kama unyumba alikuwa anapewa aisee.

Na siku zote ukimwambia umelogwa wewe basi atakufukuza kwake kama mbwa. Usiombe ndg yako afanyiwe hii kitu aisee
 
I wish siku mtu anifanyie hayo makitu nione ufanisi wake..Sijawahi kuyaamini..
Muombe Mungu akuepushe nahiyo mitihan nilimuona Mwalimu wetu naubabe wake wote yalimkuta haya akawa km mpumbavu kabisa alikuwa anafua na kupika Ndugu zake wakagundua wakamsaidia.
Lilipotoka jamaa katoa Talaka na ndoa ikaishia hapohapo.
 
Hata sisi wanaume hutilia limbwata wanawake pia......

...... kuna mwanaume anashinda kwa bao toka asubuhi bila mishe yoyote, then ana wake wanne, mmoja nurse , wawili maticha, na wa mwisho mama wa nyumbani. .... Hao wafanyakazi mshahara ukiingia wanapeleka kwa husband akapange matumizi ya mwezi.....

Cha ajabu zaidi wote wanakaa ktk jumba moja lililojengwa kwa mkopo wa bank wa kila mmoja wa hao watatu

Maajabu hayaishi Africa


# huyu bwana ni walewale kina Faiza Fox.
 
Mambo ya mwanaume anakaa tu home kazi ya kusema ndio mke wangu mie siyataki... Raha ya mwanaume anishughulishe, achelewe kurudi home tugombane kidogo tuombane msamaha... Nigundue walau ana ka mchepuko ka kunikasirisha tuvurugane weee sio jitu lina kazi ya kusema I love you my wife kajaa sebuleni mapemaaaa... Hapana mie limbwata simwekei mtu sitaki

Haha ! Umeua aisee
 
Anayekuwekea hilo limbwata ni mkeo au mchepuko?kama ni mke ni vigumu kufanikiwa kwani ndoa imebarikiwa na Mungu mwenyewe labda uaminifu usiwepo.
 
Back
Top Bottom