Airtel inazidi kutanua soko la Unlimited internet, Vodacom na Tigo wakiendelea kushupaza shingo watastuka soko lishamezwa

Hivi Star Link ya Elon Musk imeishia wapi?
Kenya wanaifaida kuna bundle 50gb kwa kes 1600, kuna 6500 hadi mbs 100 speed unlimited. Lakini kwa mtanzania bado atalalamika maaba 6500 ni almost 130000 za kitanzania na hapo wao wanaona ni cheaper kuliko safaricom na ndio maana safaricom wanahaha.
Ila madai ni kwamba starlink katikati ya jiji la nairobi haifanyi kazi poa kwa sababu ya majengo marefu na safaricom signal boosters zina affect mawimbi yake so kupata hizo speed ni ngumu wangine wanadai iko slow sana.
Ila nje ya nairobi wanasema speed yake ni kubwa balaa.
 
Fibre ni nzuri ukiwa unajiweza, Kuunga bando la jero kila siku na baadhi ya siku inaweza kufikia buku, kwa mwezi waweza tumia 20,000 ukijumlisha na fibre ni 75,000.

Kihasibu kwa wabana matumizi ni heri ulipie 4g / 5g router

  • ukihamia sehemu isiyo na fibre haikuathiri
  • unaweza kutembea nayo kwenda ofisini, nje ya mkoa, n.k.
  • umeme ukikatika kuna power bank inakaa masaa 8
  • haiathiriki kwa nguzo za fibre kudondoka au nyaya kukatwa
 
Mimi nahisi hata ningekuwa na router bado nisingetembea nayo kabisa maana kuibeba kwangu ingekuwa kikwazo.
Halafu mimi fiber imenifaa zaidi kwa sababu shughuli zangu nazifanyia home so nikitoka hapo nimeenda kusocialize au kuna kitu nafuatilia nje ya kazi tu.
fiber pia kumbuka haithiriwi na hali ya hewa. nishaona watu wanasema sijui mvua internet speed za airtel zimeshuka, mimi kwa fiber siexperience jambo hilo.
And by the way watu naodeal nao walihitaji niwe na fiber sio wireless internet maana wanasema fiber ni reliable. Ila soon ntahama hii sehemu naenda sehemu hakuna fiber so ntarudi kwenye airtel tu sina namna.
 
Kama shughuli nyingi unafanyia home fibre iko poa na haina mpinzani, labda uongezee power bank.

Tatizo ipo maeneo ya ushuani na town, Nchi kama India wameendelea sana ipo mpaka uswazi na kwa bei nafuu zaidi
 
Kama shughuli nyingi unafanyia home fibre iko poa na haina mpinzani, labda uongezee power bank.

Tatizo ipo maeneo ya ushuani na town, Nchi kama India wameendelea sana ipo mpaka uswazi na kwa bei nafuu zaidi
Nadhani wataendela kuisambaza taratibu mkuu maana nashangaa hawajaipeleka wazo ila wakaileta hadi huku bunju
 
Airtel walifika mapema nchini lakini wakasinzia sana,wanashtuka kumekucha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…