Ajali ya Happy Nation yaua Hakimu na mume wake Bukoba

Ajali ya Happy Nation yaua Hakimu na mume wake Bukoba

Aiseeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee!!! kweli TOMORROW IS UKNOWN.. hawa nawafahamu kabisa, na hata walikuwa nampango wa kunipa kazi!! maskini watoto! wameacha watoto watatu na mmoja bado mchanga.....
 
Polisi mkoani Kagera inamshikilia dereva wa Basi la Happy Nation, Shaaban Khatibu 38 mkazi wa Dare es Salaam akidaiwa kusababisha vifo vya watu wawili.

Tukio hilo inadaiwa lilitokea Barabara ya Biharamulo, Kata Ijuganyondo, Manispaa ya Bukoba, Jumanne Desemba 6, mwaka huu majira ya saa 5.30 asubuhi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, William Mwampaghale amewataja marehemu hao kuwa ni Geofrey John (42), mfanyabiashara na Tumaini Jofrey (41), ambaye ni hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kata ya Maruku.

Amesema Geofrey na Tumaini walikuwa wamebebana kwenye pikipiki, yenye namba za usajili T308CLH, ambapo walisukumwa na mwendesha pikipiki aliyekuwa amebeba magunia ya mkaa na kisha kuangukia uvunguni mwa gari la kampuni ya Happy Nation, yenye namba za usajili T70DFV, aina ya Youtong, inayofanya safari zake kati ya Dar es Salaam na Bukoba.

Amesema polisi inaendelea kumtafuta dereva wa pikipiki iliyokuwa imebeba mkaa na kwamba uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.

Katika mitandao mbalimbali ya Whatsapp ya mjini Bukoba, kulisambazwa ujumbe wa Tanzia ulioonesha umetoka Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba kwamba na ukieleza kifo cha hakimu huyo pamoja na mumewe kwa ajali ya gari, ingawa polisi haikusema kama ni mke na mume.

‘Tanzia: Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba, inasikitika kutangaza kifo cha Tumaini John Kiyeyeu-C/No.11510783 Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo Kolekero, Bukoba na mme wake kilichotokea mchana huu kwa ajali ya gari na kupelekea wote kupoteza maisha. Tutaendelea kutoa taarifa kuhusiana na taratibu za mazishi,” unasomeka sehemu ya ujumbe huo.

HABARI LEO
Ooh hii ni sad news.

Mungu aijalie familia utulivu na subira
 
Bodaboda ni mojawapo ya usafiri wa hovyo sana.
 
Mtu mwingine akikamata chombo cha moto kuendesha utadhani kakatwa kichwa!
Sasa kama huyo boda alikuwa anataka apite katikati yetu wakati napishana na gari jingine,alivyokosa nafasi akaamua ashike breki wa nyuma kwa nguvu
 
Barabaran kuna ujinga sana

Dereva hana kosa lakin kakamatwa na atatoa hela nying tu mpaka kumaliza hyo kesi na akitoka anakosa ajira anaanza tena kutafuta

Mimi kuna liboda boda lilishika brek kwa nguvu likateleza likaja upande wangu nikalikwepa ila likajigonga kwenye body,nikasimama kusikilizia,wanazengo walipokuja naambiwa nimpeleke hospital mara polisi nikaambiwa nitengeneze pikpik na kuhudumia mpaka atakapopona likidonda nalo limegoma kupona heri ningekimbia tu siku hyo
Na hela ya matumizi wampa?
 
Na hela ya matumizi wampa?
Mwanzo nilikuwa nampa ila nilivyoona siku zinakuwa nyingi nikasitisha,na anataka akipona kabisa nimlipe,nataka akipona nimkumbushe kuwa "unakumbuka ajari ulisababisha mwenyewe" sahv nishaona ni bora kwenda polisi tu au hata mahakamani
 
Barabaran kuna ujinga sana

Dereva hana kosa lakin kakamatwa na atatoa hela nying tu mpaka kumaliza hyo kesi na akitoka anakosa ajira anaanza tena kutafuta

Mimi kuna liboda boda lilishika brek kwa nguvu likateleza likaja upande wangu nikalikwepa ila likajigonga kwenye body,nikasimama kusikilizia,wanazengo walipokuja naambiwa nimpeleke hospital mara polisi nikaambiwa nitengeneze pikpik na kuhudumia mpaka atakapopona likidonda nalo limegoma kupona heri ningekimbia tu siku hyo
Pole sana mkuu,hio situation ilishanitokea ukiangalia boda alikua na makosa,ila niligoma kutemgeneza pikipiki
 
Barabaran kuna ujinga sana

Dereva hana kosa lakin kakamatwa na atatoa hela nying tu mpaka kumaliza hyo kesi na akitoka anakosa ajira anaanza tena kutafuta

Mimi kuna liboda boda lilishika brek kwa nguvu likateleza likaja upande wangu nikalikwepa ila likajigonga kwenye body,nikasimama kusikilizia,wanazengo walipokuja naambiwa nimpeleke hospital mara polisi nikaambiwa nitengeneze pikpik na kuhudumia mpaka atakapopona likidonda nalo limegoma kupona heri ningekimbia tu siku hyo

Dah pole
 
View attachment 2439021
Screenshot_20221201-084605_Facebook.jpg
View attachment 2439021
Screenshot_20221201-085121_Chrome.jpg
 
Hiyo tafsiri ya sheria. Usidhani kila mtu ni bwege humu kama wewe.
Acha kujificha kwenye kichaka cha sheria we bwege. Nimekuuliza wewe kama wewe kwa mtazamo wako na si kwa mtazamo wa sheria. Tuna sheria ngapi kandamizi zinapigiwa kelele kila uchwao? Nani hajui tuna sheria nyingi za kibwege zinazohitaji amendments. Usiishi kwa kukariri kwa kilichoandaliwa na kuletwa mbele yako ukakimeza kama kilivyo bila ku digest mambo. Kichwa maji!

Halafu sorry we ni Me au ke? Jina lako linanikumbusha demu wangu wa miaka ya 2000 Aika, tulikua tunapendana sana toto lilikua lina mzigo, macho ya kurembua..mtoto alikua anajua mahaba sana. Daah Aika wangu!
 
Mwanzo nilikuwa nampa ila nilivyoona siku zinakuwa nyingi nikasitisha,na anataka akipona kabisa nimlipe,nataka akipona nimkumbushe kuwa "unakumbuka ajari ulisababisha mwenyewe" sahv nishaona ni bora kwenda polisi tu au hata mahakamani
Aisee hapo kama anakukomoa eti,



Ni muda gani sasa?
 
KISA HAKIMU NDO DEREVA KASHIKWA MBNA WENGNE HATUSKII DEREVA KASHIKWA
 
Back
Top Bottom