Ajali ya Precision Air: Ripoti yabaini hakuna Control Tower, Boti za Uokozi zilichelewa, Mhudumu na Abiria ndio waliofungua mlango

Ajali ya Precision Air: Ripoti yabaini hakuna Control Tower, Boti za Uokozi zilichelewa, Mhudumu na Abiria ndio waliofungua mlango

Kwa hiyo pilot alipigwa maluweluwe, badala ya kuona maji akaona nchi kavu........abiria wenyewe wanaweza kuona nje, itakuwa rubani bhana ashindwe kujua hapa anatua majini au nchi kavu......
 
Ina maana Rubani hakuwatangazia abiria kuwa emergency landing ili wavae vesti zao.

Inanamaa alishusha landing gear na akatua kwenye shalow waters kitu kilichomsababishia drag na Ndege kuchotwa na kupoteza muelekeo iwapo asingeshusha landing gear Ndege ingeslide hadi Nchi kavu.
 
The END justifies the means.

Watakuja wengine kusema huyo kijana Jina lake halisi Si Majaliwa.

Majaliwa mvuvi ameshamnasua Majaliwa PM Kutoka HILA za kuzamishwa na wabunge wenzie Bungeni.

Akipanga Mungu, mwanadamu hawezi Pangua.

Ameeeeen.
 
Hivi black box kazi yake ni nini? Na hyo ripoti imengalia vitu gan mpak kuja na majibu ya hvyo , duniani kote ripoti za ajali ya ndege primary data ni black box , kwenye hii ya kwetu hata black box haitajwi
Hii ni report ya awali...ile ya black box itakuja baadae na chanzo halisi na mapendekezo...Ukiisoma hii ripoti imesema uchunguzi wa chanzo is ongoing.
 
Duh..hiyo taarifa aliyoitoa kwamba anatua majini alikupatia wewe pekeako? ukiogopa kupanda ndege si utakuwa mwendawazimu sababu ndo usafiri salama kuliko vyote, hakuwa na sababu ya kwenda Mwanza sababu wingu zito na fog vilikuwa vimepungua na uwanja ulikuwa unaonekana nadhani ndo sababu akaishusha ndege, mahali ndege ilipotua ni mita 500 tu kutoka uwanja ulipo, unataka kutuambia mafuta ya kukimbia hizo 500m yalikuwa hayatoshi?
Mi nahisi hiyo ndege ilikutwa na kitu kinaitwa aerodynamic stall dakika chache kabla ya kutua kutokana na kupungua kwa airspeed kutokana na kuzunguka mara mbili kabla hali ya hewa haijaimarika maana ni rahisi rubani kupunguza umakini wa kubalance airspeed hivyo wings kuacha ku generate lift na hivyo ndege kuanguka (nosedive).

Kama nitakuja kubahatika kuiona ripoti kamili ya uchunguzi nitalinganisha na mtazamo huu.
 
kama mlango ulifunguliwa na mhudumu kwa nn yeye hakujiokoa.ni kweli katika mazingira ya kawaida ufungue mlango halafu wewe mwenyewe ukubali ufe kwa kuwaokoa kwanza wengine?tusaidiane hapo.mm siko kinyume na taarifa lkn kuna maswali yanahitaji majibu ya kina.
Ndugu nani kakudanganya wahudumu walikufa?wahudumu wote wawili walipona.Tusiokoteze habari vijiweni
 
Hii ni report ya awali...ile ya black box itakuja baadae na chanzo halisi na mapendekezo...Ukiisoma hii ripoti imesema uchunguzi wa chanzo is ongoing.
Ngoja tusubiri hiyo ya black box mkuu
 
Majaliwa bado atakua Shujaa maana ndiyo Mtu wa kwanza kuiona hiyo ajali na kuwataarifu Wavuvi wenzie na kuwai kukimbilia kwenye ajali na kutoa msaada kwa wakati!!
Hivi ndege ilivyokuwa kubwa tutegemee kuwa wasingeiona?

Serikali na wananchi walikosea kupaisha mtu kabla hawajatoa ripoti.
Ona sasa wameumbuka

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Bongo kila mtu ni mjuaji. Ripoti imetoka bado haiaminiki.

In my view, hata kama unaona mabaya always ila ripoti imekuwa fair. Serikali na vyombo vyake wameambiwa udhaifu wao

Na uchunguzi wa chanzo cha ajali bado unaendelea, tupewe nini tena?
 
Hivi ndege ilivyokuwa kubwa tutegemee kuwa wasingeiona?

Serikali na wananchi walikosea kupaisha mtu kabla hawajatoa ripoti.
Ona sasa wameumbuka

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Namshangaa mdau hapo juu, kwa ukubwa wa ndege bado unamuhitaji majaliwa akuoneshe ndege iliyodondoka tena ikiwa bado inaelea?
 
Imefahamika kuwa licha ya Jeshi la Wanamaji kujulishwa tukio la ajali, Boti rasmi ya uokoaji ya Kitengo cha Wanamaji ilichelewa kufika eneo la ajali na sababu ni kwamba haikuwepo katika Bandari ya Bukoba
-
Pia, pamoja na Askari wa Kitengo cha Wanamaji kuchelewa kufika, hawakuweza kufanikisha zoezi la uokoaji chini ya maji kwa sababu ya ukosefu wa oksijeni na mafuta ya kutosha Boti

Aidha, kabla ya kuwasili kwa Polisi Kitengo cha Wanamaji, mmoja wa wavuvi wa eneo hilo alianza mchakato ya uopoaji wa maiti kutoka kwenye mabaki Ndege.

======

Novemba 9, 2022, Ndege ya Precision Air iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Bukoba ilipata ajali pembezoni mwa ziwa Victoria, karibu kabisa na uwanja wa Ndege wa Bukoba.

Ajali hii iliyoua watu 19 ikiwemo wasafiri 17 na wahudumu 2 iliwasili Bukoba saa 8:25 asubuhi ambapo hali ya hewa ilikuwa mbaya, kukiwa na radi, mawingu mazito na upepo mkali.

Kwa mujibu wa Ripoti iliyotolewa na wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, ndege hii ilizunguka mji wa Bukoba mara mbili, kisha abiria walipewa taarifa kuwa ingegeuza kurudi Mwanza kwa kuwa hali iliyokuwepo hapo haikuwa rafiki.

Lakini wakati ikizunguka kwa mara ya tatu, rubani aliweza kuona sehemu ya kutua ndipo akaamua kuishusha. Kwa mujibu wa manusura, ndege hii ilishuka salama, lakini kabda haijakanyaga ardhi ndipo ilibadili uelekeo kuelekea upande wa ziwa.

Mhudumu mmoja wa ndege hiyo pamoja na abiria mwingine ndiyo walihusika kufungua mlango, kisha abiria huyo alisimama kuzuia mlango ili usijifunge ili abiria wengine waweze kutoka na kuingia kwenye mitumbwi ya wavuvi.

Boti ya uokoaji iliwasili saa 7:49 mchana sababu ilikuwa inafanya oparesheni zingine, hivyo haikuwa karibu na uwanja wa Ndege wa Bukoba.

Marubani wote wawili walishindwa kufungua mlango kutokana na nguvu kubwa ya maji, kama kungekuwa na msaada wa haraka, watu wengi wangeokolewa

Pia, ripoti imebainisha kuwa uwanja wa ndege wa Bukoba hauna mnara kwa kuongozea ndege (Control tower). Mawasiliano yote hufanyika kwa kutumia mnara wa Mwanza.

Uchunguzi wa kubaini chanzo halisi cha ajali hii bado unaendelea.

View attachment 2424342View attachment 2424343
Kwahiyo mnataka kutuambia Majaliwa hakusaidIa ama? Mwacheni nae alicheza pat yake huyo muhudumu yuko wapi?
 
Binafsi nimesoma maswala ya aviation ndege huwez kufungua mlango ukiwa nje.

Afu pia kasia ambalo ni jiti haliwezi kuvunja mlango wa ndege ukafunguka swali ni je kama majaliwa alifungua mlango wa ndege je huyo muhudumu ameiongopea bodi ya uchunguzi kwamba yey ndo alie fungua mlango na kuuzuia usijifunge mpka abilia washuke?

Jaribuni kutunga uongo unao fanana na ukweli
 
Kampuni ya precision bangiii ,wale I tu eti wanamlaumu majaliwa kwani majaliwa anahusikaje na ujinga wao ??

Hawana akili hao wao ndio walipaswa kuweka mambo Yao sawa wameua watu watu Kisa uzembe wanasingizia serikali wapuuzi labda ingekuwa air Tanzania maana ndio ya serikali wameniboa au walitaka kutoa wenzao sadaka wapate wateja wengi
Soma ripoti Acha tantalila.
 
Kwa skendo kama hii, ya kizembe na kuwadanganya wananchi kwa kuweka shujaa wa "mchongo", ingekuwa ni nchi za wenzetu Ulaya, kuanzia Waziri Mkuu, Mkuu wa Mkoa, Spika wa Bunge na viongozi wengine wengi wangelazimika kujiuzulu nafasi zao.

Lakini kwakuwa tupo Bongo sishangai kuona wakiendelea na kazi zao bila hata mshipa wa aibu.

Swali la kujiuliza, walitudanganya sisi Wananchi kwa manufaa ya nani????
 
kwa hio kitalaam Majaliwa tunamwitaje ?

tatizo Tanzania siasa mpaka kwenye maisha ya watu
 
Imefahamika kuwa licha ya Jeshi la Wanamaji kujulishwa tukio la ajali, Boti rasmi ya uokoaji ya Kitengo cha Wanamaji ilichelewa kufika eneo la ajali na sababu ni kwamba haikuwepo katika Bandari ya Bukoba
-
Pia, pamoja na Askari wa Kitengo cha Wanamaji kuchelewa kufika, hawakuweza kufanikisha zoezi la uokoaji chini ya maji kwa sababu ya ukosefu wa oksijeni na mafuta ya kutosha Boti

Aidha, kabla ya kuwasili kwa Polisi Kitengo cha Wanamaji, mmoja wa wavuvi wa eneo hilo alianza mchakato ya uopoaji wa maiti kutoka kwenye mabaki Ndege.

======

Novemba 9, 2022, Ndege ya Precision Air iliyokuwa inasafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Bukoba ilipata ajali pembezoni mwa ziwa Victoria, karibu kabisa na uwanja wa Ndege wa Bukoba.

Ajali hii iliyoua watu 19 ikiwemo wasafiri 17 na wahudumu 2 iliwasili Bukoba saa 8:25 asubuhi ambapo hali ya hewa ilikuwa mbaya, kukiwa na radi, mawingu mazito na upepo mkali.

Kwa mujibu wa Ripoti iliyotolewa na wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, ndege hii ilizunguka mji wa Bukoba mara mbili, kisha abiria walipewa taarifa kuwa ingegeuza kurudi Mwanza kwa kuwa hali iliyokuwepo hapo haikuwa rafiki.

Lakini wakati ikizunguka kwa mara ya tatu, rubani aliweza kuona sehemu ya kutua ndipo akaamua kuishusha. Kwa mujibu wa manusura, ndege hii ilishuka salama, lakini kabda haijakanyaga ardhi ndipo ilibadili uelekeo kuelekea upande wa ziwa.

Mhudumu mmoja wa ndege hiyo pamoja na abiria mwingine ndiyo walihusika kufungua mlango, kisha abiria huyo alisimama kuzuia mlango ili usijifunge ili abiria wengine waweze kutoka na kuingia kwenye mitumbwi ya wavuvi.

Boti ya uokoaji iliwasili saa 7:49 mchana sababu ilikuwa inafanya oparesheni zingine, hivyo haikuwa karibu na uwanja wa Ndege wa Bukoba.

Marubani wote wawili walishindwa kufungua mlango kutokana na nguvu kubwa ya maji, kama kungekuwa na msaada wa haraka, watu wengi wangeokolewa

Pia, ripoti imebainisha kuwa uwanja wa ndege wa Bukoba hauna mnara kwa kuongozea ndege (Control tower). Mawasiliano yote hufanyika kwa kutumia mnara wa Mwanza.

Uchunguzi wa kubaini chanzo halisi cha ajali hii bado unaendelea.

View attachment 2424342View attachment 2424343
Aircraft investigation acha ianze kufanya kazi sasa
 
Back
Top Bottom