Ajifungua Akiwa Safarini Kwenye Basi Kampuni ya Katarama

Ajifungua Akiwa Safarini Kwenye Basi Kampuni ya Katarama

Inaweza kuwa safari yenye huzuni na kukushtua endapo kunatokea taarifa za kuogofya za ajali hama hama tukio lenye kuhuzunisha.

Hapo hapo safari inaweza kuwa na furaha endapo safarini kuna vicheko kwa wasafiri.

Tukio lililotokea majira ya saa 19:34 maeneo ya dumila karibu na mzani ni mshangao.

View attachment 3132869
Censored image ☝🏾

Ni abiria aliyekuwa anatokea Dar Es Salaam aliyefahamika kwa jina moja la Aneth kuelekea Bukoba amejifungua mtoto wa kike akiwa safarini.

Hatimaye Mama na mtoto wamebaki kituo cha Afya hapo Dumila kwa uangalizi wa wataalam wa Afya.

Hongera kwa wamama wote waliotoa msaada na hatimaye mzazi kujifungua salama, asante kwa kampuni ya Katarama kwa ushirikiano mliotoa.

USHAURI; Wenye makampuni ya mabasi naona haja ya kuwapa elimu zaidi wafanyakazi wenu hata hii ya ukunga, maana si mara ya kwanza kwa tukio kama hili.
Una mimba ya karibia kujifungua unaanza safari ya basi dar bukoba😬😬😬😬😬😬😬. Tuna vichaa wengi sana mtaani.
 
Huwa sielewi kwann mtu anasafiri akiwa na mimba ya miezi tisa, mwaka 2015 dada yangu alisafiri na ndege toka mkoani akiwa na mimba ya miezi tisa alivyoulizwa airport akasema Ina miezi sita Sasa na mwili wake unajua ni kweli, basi Ile anatua tu pale airport uchungu balaa, akakimbizwa haraka hospitali Ile kufika hata daktari hajamuona akajifungua, alijifungulia pale rugambwa hospital Iko sijui ukonga pale, mjini asingeweza kufika..!
 
Inaweza kuwa safari yenye huzuni na kukushtua endapo kunatokea taarifa za kuogofya za ajali hama hama tukio lenye kuhuzunisha.

Hapo hapo safari inaweza kuwa na furaha endapo safarini kuna vicheko kwa wasafiri.

Tukio lililotokea majira ya saa 19:34 maeneo ya dumila karibu na mzani ni mshangao.

View attachment 3132869
Censored image ☝🏾

Ni abiria aliyekuwa anatokea Dar Es Salaam aliyefahamika kwa jina moja la Aneth kuelekea Bukoba amejifungua mtoto wa kike akiwa safarini.

Hatimaye Mama na mtoto wamebaki kituo cha Afya hapo Dumila kwa uangalizi wa wataalam wa Afya.

Hongera kwa wamama wote waliotoa msaada na hatimaye mzazi kujifungua salama, asante kwa kampuni ya Katarama kwa ushirikiano mliotoa.

USHAURI; Wenye makampuni ya mabasi naona haja ya kuwapa elimu zaidi wafanyakazi wenu hata hii ya ukunga, maana si mara ya kwanza kwa tukio kama hili.
Hakutakiwa kusafiri huyo asirudie tena kusafiri iwe kwa ndege au gari kama anakaribia kujifungua
 
Huwa sielewi kwann mtu anasafiri akiwa na mimba ya miezi tisa, mwaka 2015 dada yangu alisafiri na ndege toka mkoani akiwa na mimba ya miezi tisa alivyoulizwa airport akasema Ina miezi sita Sasa na mwili wake unajua ni kweli, basi Ile anatua tu pale airport uchungu balaa, akakimbizwa haraka hospitali Ile kufika hata daktari hajamuona akajifungua, alijifungulia pale rugambwa hospital Iko sijui ukonga pale, mjini asingeweza kufika..!
Watu Bado wanaishi kizamani kwa kujisemea "mimba yangu ya kwanza ilikuwa hivi" au "mama alikuwa hivi" hivyo nikiondoka naweza kufika. Alafu hofu tu zilizopitwa na wakati mtu anaenda kujifungulia nyumbani maana unakuta na mwanaume wake ameunga mkono hoja ya mkewe kwenda home. Wakati siku hizi mtu akionyesha dalili tu unakimbiza hospital unasikilizia tu atajifungua lini.

Walihisi wataokoa gharama ndo wameingia gharama sasa maana nauli imekwenda na wanapata gharama za kumsikilizia mzazi kwa siku moja ama mbili aweze kutoka, na tushukuru tu huduma ya kujifungua ni bure
 
Una mimba ya karibia kujifungua unaanza safari ya basi dar bukoba😬😬😬😬😬😬😬. Tuna vichaa wengi sana mtaani.
Shotocan
Kila jambo lina sababu yake, wkt umemuita huyo mzazi kichaa, nilitamani ungepata nafasi kuonana naye na kumuuliza kisa na mkasa kilicho mpelekea Kusafiri ktk hali ile!.
 
Back
Top Bottom