Ajinyonga kwa kutotajwa na Padri kwenye misa ya Shukrani

Ajinyonga kwa kutotajwa na Padri kwenye misa ya Shukrani

Msala kwa TTCL.

Ila kmmkk me kujinyonga sio leo au kesho.

Maisha magumu ila aisee kiporo cha wali ma maharage kitamu.
 
Mwanaume mmoja kutoka wilayani Ludewa amekatisha uhai wake kwa kujinyonga sababu ikiwa ni kutotajwa na padri katika misa ya Shukrani.

Bwana huyo na mke wake walikuwa wakitoa Shukrani katika Kanisa la Moravian kwa mtoto wao kupona lakini kwa sababu zisizofahamika Padri aliyeongoza misa hio alimtaja mama wa mtoto pekee na kumuacha yeye baba bila kutajwa hali iliyoleta sintofahamu.

............................
Habari Kamili;

MKAZI wa mtaa wa Kanisani B uliopo wilaya ya Ludewa mkoani Njombe anaefahamika kwa jina la Raban Razalo (48) amefariki kwa kujinyonga na waya kwa madai ya kutoridhishwa na kitendo cha Padri wa kanisa la Moravian kushindwa kumtaja jina wakati wa misa ya sadaka ya shukrani iliyofanywa na mkewe baada ya mtoto wao wa miaka 10 kupona majeraha ya kuvunjika mguu.

Kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Njombe, Hamis Issa amesema taarifa zilizobainiwa na jeshi hilo ni kwamba mtoto wa familia hiyo mwenye umri wa miaka 10 alivunjika mguu na kupelekea familia kuzunguka katika hospitali tofauti kupata matibu na kisha kupona jambo ambalo limemsukuma mama kwenda kanisani kutoa sadaka ya shukrani ambayo imekuwa chanzo cha kuondoa maisha ya baba wa familia.

“Walivyoenda kutoa sadaka ya shukrani,Padri wa kanisa hilo amemtaja mama wa mtoto peke yake, baba imemletea sintofahamu na matokeo yake baba ameamua kujinyonga kwa kutumia waya wa TTCL.

Kamanda Issa ametoa wito kwa viongozi wa dini kuangalia umuhimu wa familia kwa kuwa inaundwa na baba na mama.

“Viongoizi wa dini angalieni umuhimu wa familia,familia ni baba na mama,ukimtaja mmoja matokeo yake ndipo unapopata sintofahamu na maamuzi yasiyo kuwa na tija”amesema kamanda Issa.

Aidha ametoa rai kwa wanafamilia kutochukua maamuzi kwa jambo ambalo wamekwazika huku akisikitika kwa familia hiyo kumuuguza mtoto mpaka kupona na baadaye mzazi anafariki.


Chanzo: RFA
Roho ya mkwawa..
 
Ilikua ngumu kwa padri kutaja jina la baba akati padri anajua yule ni mwanae yeye pengine
 
RFA mmepotosha,. Moravian hawana padri alafu kuhusu kujinyonga Kwa Huyo jamaa (Kwa asilimia kubwa alikuwa anaandamwa na pepo la kifo.apumzike Kwa amani

Sent using Jamii Forums mobile app
Hio taarifa imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe,na yeye ndio kasema padri,kwahio aulizwe Kamanda
 
Na mimi najua hivyo.Sasa mtoa Post ametoa wapi Padri wa Wamoraviani?.
Hio ni taarifa ya Kamanda wa Polisi,ina maana si kafanya uchunguzi akagundua padri ndio hakutaja jina[emoji38]
 
Msala kwa TTCL.

Ila kmmkk me kujinyonga sio leo au kesho.

Maisha magumu ila aisee kiporo cha wali ma maharage kitamu.
Usirudie kuapa ndugu.

Shetani huwa anapenda sana kujaribu
 
Padri ndiye mchungaji,nendeni kwenye page ya Askofu Emmaus Mwamakula FB katoa somo kuhusu neno Padri na Mchungaji.
 
Inaelekea nyumbani kuna mengi yalikua yanaendelea yaliyosababisha baba kukosa kujiamini. Communication is a key to any active relationship.
 
Kuna ushahidi gani kuwa sababu ya kujinyonga ni kutotajwa na Padri?
 
Back
Top Bottom