Ajiua kwa kujinyonga siku chache kabla ya harusi yake

Ajiua kwa kujinyonga siku chache kabla ya harusi yake

Ww ni graduate unashindwa hata kuandika kitu kinachoeleweka??
Mimi na wewe nan ambaye ni smart ? Hujaelewa nn au shobo tu!!

Angalia hata jina lako umeanza na herufi ndogo kati Kuna herufi kubwa ,uliskip madarasa na utakuwa mbara tu kiswahili hujui.
 
Sahih kbsa wabongo michosho sna unamshirikisah had ndugu yako wa damu magumu unayopitia yey anaenda kumuadidhia mke wake kbsa

Nilikereka Sana siku moja namuambia kak angu ishu zangu yey kazipeleka had kwa mke wake dah nilijuta kusema yaani

Mwingine magumu yako unamuambia lkn anazbaa Zaid unashanga ripoti zako zina fuja

Bas tu mm sisemi Wala nn na hkuna kujiua nijiue niwaachie yanga Nani[emoji1]
Si Bora wewe Kaka yako

Mimi kuna shemeji yangu tuko age Sawa nilimshirikisha kitu cha kiume anipe ushauri nikashangaa dada yangu ananipigia simu.


Tangu siku hiyo sijawahi kumwambia huyu jamaa Jambo langu

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Wazee hili laifu sio poa hasa ukiwa mzaliwa wa kwanza...kwa kifupi mimi pia napita hardtime sana

Sina kazi (jobless)

Kodi yangu inaisha December (kichwa kinauma machozi yanatoka)

Umri umesogea miaka 26 mates wenzangu wengi wana maisha na darasani nilikuwa bora kuliko wao.nimeomba makazi ya majeshi yote mwaka jana mpka nimekataa tamaa

Kula yangu mzozo,unaumwa ila unapona kwa nguvu za Mungu...

Kushinda week mfukoni huna mia ni kawaida

Kwa kifupi depression is real ukiona unaaamka unakula unavaa mshukuru Mungu

Mungu anisaidie nivuke salama nakiri sometimes najifikiriaga sana kujipoteza(kujitoa uhai) sema namuonea huruma mama na madogo zangu.
Pole sana ndugu.
 
Yupo jamaa mmoja alikuwa rafiki yangu nilisoma nae chuo na nishawai kukaa group moja japo mi nilikuwa chairman ila alikuwa mtu yuko active sana nilimkubali ila ishu zake anaficha mpaka ilipobuma .

Ilikuwa ivi jamaa alikuwa na demu wake wanapendana sana na hapo chuo kusema la ukweli kasoma mpaka third year hakuwai hata kutongoza kwa maelezo yake alimpenda demu sana ila mshkaji kwao life la kawaida sana ,kama tegemezi basi kipind tukiwa chuo alikuwa na hustling Sana kila dili yye hata dalali yupo anamake money anatuma kwa bi mother wake na kumuhudumia demu..basi miaka kadhaa mbele baada ya chuo zilitokea ajira akasema hatoenda alikuwa kashaanza biashara na alipiga mwaka mmoja awe kashamuoa demu wake anajulikana mpaka home kwa huyo demu yaani kama kwao maana wote Wana asili moja ni watu wa mbeya ...

Basi jamaa ule mwaka aliyumba kiasi cha kuingia madeni kibao mpaka biashara ikafa ndani ya mwaka mmoja kingine akasema hapo hapo demu alianza kuleta nyodo ,bahati mbaya demu kashaanzisha mahusiano na jamaa mwingine..

Basi washkaji wake wakamsanua kwamba demu kashachumbiwa yeye akajipa moyo labda masnitch ..kumbe kweli mpaka demu kaolewa na jamaa hapa dar harusi kubwa kabisa .,jamaa kaenda home kwa kina demu wakawambia eti kwa nn alikuwa anamchezea na sio kumuoa jamaa akawaeleza zile ishu bado wakamtolea nje maana demu kashaolewa na kweny simu kablockiwa na demu.

No way jamaa alifanya attempt ya kunywa sumu watu wakamuwahi haswa washkaji na ishu wakasema iwe kimya hata mwenyekitu asijue basi jamaa tangu hapo Kawa kama kapumbaa yaani kama kachizisha kimtindo ,kapooza ila demu kashaolewa Kuna kipind vilitulia akawa anapiga dili coz chuo alikuwa na performance nzuri tu sasa akiwa mishe posta ile kashapoteza kama mwaka na kitu tangu ya tukio ,bahati mbaya akakutana na demu yule akiwa na jamaa na demu akiwa na mimba jamaa ilikuwa siku mbaya kwake Tena ile hali ikaanza kumrudia Tena..

Akaona arudi kwao mbeya ila yupo town sasa yuko fresh anapiga ishu zake tu za maana namkubali ni hustler .
Msomi gani wewe unaandika kiswahili cha kihuni kwenye issue serious ????
 
Dah hatari sana ,Kuna jambo nyuma ya pazia
Haya mambo yapo huku kwetu bado tunaamini kuna jambo nyuma ya pazia ukweli sio lazima tumeona huko ulaya watu wana kila kitu anaamua kutoa maisha yake hana deni wala hana shida ana kila kitu. Tumesikia wachezaji mpira wana fanya kampeni kuwa ongea na mtu ukihisi una mzongo wa mawazo. Hii ni mental health issue unakuwa unawaza kupita kiasi huna wa kuongea naye akakusikiliza na mbaya zaidi ukiwa na shida halafu wale watu uliokuwa unadhani ni wa karibu sana na wewe unaona wanakuacha unabaki peke yako haijalishi una nini lakini ukipata mtu wa kukusikiliza unapata relief. Ni bahati mbaya lakini sisi bado hatujaona kama mental health ni issue, mimi kuna kijana namjuwa hakuwa close friend lakini tunajuana vizuri sana kijana kasoma ana kazi nzuri sana alikuwa muongeji kiasi ila kuna wakati tabia zikaanza kubadilika haongei sana wala kuingiliana na watu kuna siku nikaongea naye kuuliza una nini unaumwa au kuna mtu mmegombana akasema hapana nikamwambia kama una jambo ukitaka ongea na mimi au rafiki yako yoyote akasema hakuna kitu, nikaongea na rafiki zake wa karibu sana na wote waliona ile hali lakini hatukuweza kumsaidia kuna siku alipotea akaja kukutwa amefariki baada ya siku mbili kaenda sehemu mbali ka pack gari yake na mwili wake umekutwa chini amefariki was very sad hakuna foul yoyote hatujui kilitokea nini mwili wake ukazikwa baada ya kupewa ruhusa kuwa hakuna jeraha lolote ilikuwa sad hatukuweza kumsaidia mpaka leo hatujui alikuwa na nini mawazo yake maana alikuwa na kazi nzuri na good family.
 
Joseph Patrick Ngonyani mkazi wa Kijiji cha Makuyni kilichopo Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro amejiua kwa kujinyonga ikiwa zimebaki siku 29 afunge ndoa.

Uchunguzi wa chanzo cha kifo chake bado unaendelea.

Godlisten Malisa ameandika haya katika ukurasa wake wa Facebook kuhusu kifo cha Joseph Ngonyani (rafiki yake):
Mwezi August mwaka huu ulimvalisha pete mchumba wako na ukatuomba support marafiki zako kwa ajili ya ndoa yenu uliyopanga kuifunga mwezi December mwaka huu. Tulikutakia heri na kuahidi ushirikiano. Lakini leo nimeshtushwa na taarifa ya kifo chako cha ghafla. Nimeambiwa umejinyonga. What a shocking news.!

Rafiki na mdogo wangu #JosephNgonyani nini kimekusukuma kufanya uamuzi huu mgumu namna hii? Zilibaki siku chache tu kuelekea ndoa yako. Itakuaje sasa kwa mchumba wako? Je mipango yote mliyopanga ndio imeishia hapa? Kwanini hukutishirikisha ikiwa kuna jambo gumu uliloshindwa kulimudu? Daah. Just rest in peace bro. Nimeishiwa maneno.!

Wanaume tunapitia mengi sana. Baada ya kuweka taarifa ya dogo #JosephNgonyani kujinyonga, ndugu Mathew Mfinanga ameamua kushare sehemu ya mapito yake. Ni magumu sana, lakini jambo la muhimu tusiache kuongea. Kama unapitia changamoto ukaongea na watu 100 wasipokuelewa, basi kuna mmoja atakuelewa. Na Mungu atamtumia huyo mmoja kubadili story ya maisha yako.

Wanaume wengi hufikia hatua ya kujiua kwa kutokuongea, au kuona wakiongea watakua wamejidhalilisha. Please talk to save ur life. Taarifa ya taasisi ya afya ya akili nchini Marekani (National Institute of Mental Health) inaonesha kuwa 77% ya watu wote wanaojiua ni wanaume. Hizi takwimu zinatisha. Moja ya sababu ya wanaume "kukimbilia" kujiua ni kushindwa kuongea wanapopitia magumu.

Wanawake hawajiui kirahisi kwa sababu wanaongea sana. Katika kuongea kwao wanaweza kupuuzwa au kusaidika, lakini la muhimu wameongea. Kuongea kunapunguza mzigo, kunakupa nafasi ya kufikiria tena, kunakuwezesha kupata mawazo mapya, kunasaidia kujipanga upya. Kujiua ni ubinafsi. Ni kuacha mzigo mkubwa kwa wale waliokua wanakutegemea. Ni kuacha alama ya maumivu yasiyokoma kwa wanao, mke na ndugu zako. Kujiua sio suluhisho. Wanaume tuongee, tuongee, tuongee.!

Mchangiaji mmoja pia ametoa ushuhuda wake kuhusu alivyopitia hali ya sonona (See atached image) :
Wanawake hawajiui kirahisi kwa sababu wanaongea sana. Katika kuongea kwao wanaweza kupuuzwa au kusaidika, lakini la muhimu wameongea. Kuongea kunapunguza mzigo, kunakupa nafasi ya kufikiria tena, kunakuwezesha kupata mawazo mapya, kunasaidia kujipanga upya. Kujiua ni ubinafsi. Ni kuacha mzigo mkubwa kwa wale waliokua wanakutegemea. Ni kuacha alama ya maumivu yasiyokoma kwa wanao, mke na ndugu zako. Kujiua sio suluhisho. Wanaume tuongee, tuongee, tuongee.![emoji818][emoji817][emoji1545]
 
Yupo jamaa mmoja alikuwa rafiki yangu nilisoma nae chuo na nishawai kukaa group moja japo mi nilikuwa chairman ila alikuwa mtu yuko active sana nilimkubali ila ishu zake anaficha mpaka ilipobuma .

Ilikuwa ivi jamaa alikuwa na demu wake wanapendana sana na hapo chuo kusema la ukweli kasoma mpaka third year hakuwai hata kutongoza kwa maelezo yake alimpenda demu sana ila mshkaji kwao life la kawaida sana ,kama tegemezi basi kipind tukiwa chuo alikuwa na hustling Sana kila dili yye hata dalali yupo anamake money anatuma kwa bi mother wake na kumuhudumia demu..basi miaka kadhaa mbele baada ya chuo zilitokea ajira akasema hatoenda alikuwa kashaanza biashara na alipiga mwaka mmoja awe kashamuoa demu wake anajulikana mpaka home kwa huyo demu yaani kama kwao maana wote Wana asili moja ni watu wa mbeya ...

Basi jamaa ule mwaka aliyumba kiasi cha kuingia madeni kibao mpaka biashara ikafa ndani ya mwaka mmoja kingine akasema hapo hapo demu alianza kuleta nyodo ,bahati mbaya demu kashaanzisha mahusiano na jamaa mwingine..

Basi washkaji wake wakamsanua kwamba demu kashachumbiwa yeye akajipa moyo labda masnitch ..kumbe kweli mpaka demu kaolewa na jamaa hapa dar harusi kubwa kabisa .,jamaa kaenda home kwa kina demu wakawambia eti kwa nn alikuwa anamchezea na sio kumuoa jamaa akawaeleza zile ishu bado wakamtolea nje maana demu kashaolewa na kweny simu kablockiwa na demu.

No way jamaa alifanya attempt ya kunywa sumu watu wakamuwahi haswa washkaji na ishu wakasema iwe kimya hata mwenyekitu asijue basi jamaa tangu hapo Kawa kama kapumbaa yaani kama kachizisha kimtindo ,kapooza ila demu kashaolewa Kuna kipind vilitulia akawa anapiga dili coz chuo alikuwa na performance nzuri tu sasa akiwa mishe posta ile kashapoteza kama mwaka na kitu tangu ya tukio ,bahati mbaya akakutana na demu yule akiwa na jamaa na demu akiwa na mimba jamaa ilikuwa siku mbaya kwake Tena ile hali ikaanza kumrudia Tena..

Akaona arudi kwao mbeya ila yupo town sasa yuko fresh anapiga ishu zake tu za maana namkubali ni hustler
 
Wazee hili laifu sio poa hasa ukiwa mzaliwa wa kwanza...kwa kifupi mimi pia napita hardtime sana

Sina kazi (jobless)

Kodi yangu inaisha December (kichwa kinauma machozi yanatoka)

Umri umesogea miaka 26 mates wenzangu wengi wana maisha na darasani nilikuwa bora kuliko wao.nimeomba makazi ya majeshi yote mwaka jana mpka nimekataa tamaa

Kula yangu mzozo,unaumwa ila unapona kwa nguvu za Mungu...

Kushinda week mfukoni huna mia ni kawaida

Kwa kifupi depression is real ukiona unaaamka unakula unavaa mshukuru Mungu

Mungu anisaidie nivuke salama nakiri sometimes najifikiriaga sana kujipoteza(kujitoa uhai) sema namuonea huruma mama na madogo zangu.
Usikate tamaa endelea kupambana,usichague kaz.
 
Mambo ni mengi sana kwa Wanaume.
Ila kuwa na marafiki wa aina tofauti tofauti pia kuna saidia.
 
Njia ya kukufanya ubaki Salama ni kukaa mbali na Uzinzi na Ulevi

na tusilazimishe Mambo wakati wa Mungu ndo wakati sahihi kujiua kisa Mwanamke ni Upumbavu mkubwa Sana pia lazima uende Motoni hiyo haina mjadala.
 
Kwa upande mwingine aliyejinyonga ana lawama upande mwingine tusimlaumu maana hatujui.
1.Kuna wengine wanajinyonga sababu ya matatizo ya akili na ndio maana wanaojaribu kujiua wakinusurika wanapelekwa kwanza kupimwa afya ya akili.Kuna magonjwa mengine yanamfanya mtu kuwaza kujiua tu mfano ugonjwa wa sonona na Schizophrenia.
2.Kwa upande wa lawama kama ana akili timamu kujiua ni kitendo cha ubinafsi na usiri.

Wanawake hawajiui kama wanaume kwa sababu wao ni waongeaji mno.Kwa kawaida wanawake huwa wakifiwa wanalia sana.Kile kitendo cha kulia kinapunguza sumu mwilini ya kifikra wanaume wao kule kunyamaza sumu inabakia mwilini.

Kwa mdada ambaye ilikuwa aolewe amshukuru mungu sana maana amemuonyeshe angeolewa na mwanaume ambaye hakuwa sahihi kabisa huyu angeweza hata kumu ua.
Kwa upande mwingine aliyejinyonga ana lawama upande mwingine tusimlaumu maana hatujui.
1.Kuna wengine wanajinyonga sababu ya matatizo ya akili na ndio maana wanaojaribu kujiua wakinusurika wanapelekwa kwanza kupimwa afya ya akili.Kuna magonjwa mengine yanamfanya mtu kuwaza kujiua tu mfano ugonjwa wa sonona na Schizophrenia.
2.Kwa upande wa lawama kama ana akili timamu kujiua ni kitendo cha ubinafsi na usiri.

Ushauri kwenye familia au ukoo wenu akitokea mtu amejiua jambo la kufanya haraka sana ni kufanya maombo kama ni wakristo na kama ni waislam ni kufanya dua na maulidi kufuta hiyo laana maana shetani yuko kazini jambo hiyo litajirudia siku ingine kwa kizazi kinachofuatia ao hicho hicho hiyo ni kazi ya shetani ili kukata huo mnyororo lazima kitu kifanyike.

Hapa nchini kuna kabila ambalo lina sifa ya watu kujiua.Hii inaitwa majigambo kwa lugha fasaha hilo kabila silitaji mwenye kujua atalijua mtemi wao alijinyonga kwa kutokutaka kukamatwa na Wajerumani.Sasa kitendo alichokifanya hadi leo kinatembelea watu wa kabila hilo.
Nisameheni kama nimemkwaza mtu huo ndio ukweli
 
Wazee hili laifu sio poa hasa ukiwa mzaliwa wa kwanza...kwa kifupi mimi pia napita hardtime sana

Sina kazi (jobless)

Kodi yangu inaisha December (kichwa kinauma machozi yanatoka)

Umri umesogea miaka 26 mates wenzangu wengi wana maisha na darasani nilikuwa bora kuliko wao.nimeomba makazi ya majeshi yote mwaka jana mpka nimekataa tamaa

Kula yangu mzozo,unaumwa ila unapona kwa nguvu za Mungu...

Kushinda week mfukoni huna mia ni kawaida

Kwa kifupi depression is real ukiona unaaamka unakula unavaa mshukuru Mungu

Mungu anisaidie nivuke salama nakiri sometimes najifikiriaga sana kujipoteza(kujitoa uhai) sema namuonea huruma mama na madogo zangu.
Labda nikutie moyo tu, nioneshe tajiri mmoja tu Africa mwenye umri kama wako ambaye utajiri wake sio wa kurithi.

Waliosema life start after 40 hawakuwa wajinga.

Sasa hapo mwanamke atakayekubali kuwa na mahusiano na wewe huyo ndio Mke wa kweli wa kuja kumuowa achana na wajinga wanaokwambia tafuta pesa.
 
Nachokupendea mara nyingi wit. comments zako zinakuwa za ukweli.
Ila nasubiri siku ambayo utageukia mbele kwenye hiyo avatar yako (Kama Ni wewe huyo); hapo utakuwa umedhihirisha ukweli ako.[emoji144][emoji2960]
Apia kabisa [emoji14][emoji14]
 
Laiti angeambiwa kuwa, hakuna dhambi kubwa kama ya kukata tamaa. Tujaribu kushirikisha magumu yetu na watu wengine wanaoaminika.
 
Back
Top Bottom