Lord denning
JF-Expert Member
- Jun 3, 2015
- 15,819
- 33,255
Kila siku nasema kuwa akili ni nywele.
Ukiwa na akili timamu, utajua tatizo ulilonalo ni lipi na utaweka na kutekeleza mipango sahihi ya kulitatua hilo tatizo.
Wenzetu Kenya waligundua wana tatizo la mipango miji, kwa maeneo mengi kujengwa vibaya bila mpangilio na kufanya wananchi wengi kuishi kwenye maeneo ambayo hayana hadhi na staha kwa binadamu wa kawaida.
Hivyo wamekuja na mpango wa kubomoa maeneo hayo na kuyajenga upya. Saivi Kibera imeanza kuvinjwa na kujengwa upya. Mukuru imeanza kujengwa flats nzuri kwa ajili ya makazi ya wananchi wa kawaida.
Kwa upande mwingine huku kwetu bongo kama kawaida yetu, Tuna tatizo la makazi holela na ujenzi usio na mpangilio ila Wizara ya Ardhi wako na cliniki za ardhi. Eti kutatua migogoro ya ardhi ambayo kiuhalisia imesababishwa na wao kutotimiza wajibu wao wa kuifanya nchi yetu kupangwa na kujengwa vizuri. Mbaya zaidi wamelala tu huku kila siku maeneo ambayo hayajajengwa vizuri kwa mpangilio yanazidi kuongezeka nchini.
Kila siku nitasema. Akili ni nywele na bila kuwaondoa CCM tutazidi kuwa vituko hadi kiama.
Ukiwa na akili timamu, utajua tatizo ulilonalo ni lipi na utaweka na kutekeleza mipango sahihi ya kulitatua hilo tatizo.
Wenzetu Kenya waligundua wana tatizo la mipango miji, kwa maeneo mengi kujengwa vibaya bila mpangilio na kufanya wananchi wengi kuishi kwenye maeneo ambayo hayana hadhi na staha kwa binadamu wa kawaida.
Hivyo wamekuja na mpango wa kubomoa maeneo hayo na kuyajenga upya. Saivi Kibera imeanza kuvinjwa na kujengwa upya. Mukuru imeanza kujengwa flats nzuri kwa ajili ya makazi ya wananchi wa kawaida.
Kwa upande mwingine huku kwetu bongo kama kawaida yetu, Tuna tatizo la makazi holela na ujenzi usio na mpangilio ila Wizara ya Ardhi wako na cliniki za ardhi. Eti kutatua migogoro ya ardhi ambayo kiuhalisia imesababishwa na wao kutotimiza wajibu wao wa kuifanya nchi yetu kupangwa na kujengwa vizuri. Mbaya zaidi wamelala tu huku kila siku maeneo ambayo hayajajengwa vizuri kwa mpangilio yanazidi kuongezeka nchini.
Kila siku nitasema. Akili ni nywele na bila kuwaondoa CCM tutazidi kuwa vituko hadi kiama.